HOJA MBADALA: Tuhamasishe CCM imsimamishe Membe 2015?

HOJA MBADALA: Tuhamasishe CCM imsimamishe Membe 2015?

Inatakiwa nyinyiemu wote watoswe kwa umoja wao, they have eaten enough for the owner to see
 
Kiongozi, mimi sioni tofauti ya kifalsafa kati ya Kikwete na Membe. Tabia za Membe za sasa zinafanana na tabia za Kikwete kabla hajawa rais. Sioni Membe kama anauwezo wa kuunda timu ya kuongoza nchii hasa ukizingatia minyukano iliyomo ndani kwa ndani huko CCM
 
MLANGO WA MAENDELEO YA NCHI YETU YA TANZANIA TULIO INGILIA MWAKA 1967 - KISIASA, KIUCHUMI NA KIJAMII - NDIO HUO HUO TUTAKAO UTOKEA MWAKA 1985-1995-2005 NA VIZAZI VIJAVYO.

Mkuu samahani naomba nitoke nje ya topic kidogo, hivi huwa unamaanisha nini na haya maneno? Niko very interested kupata maana yake manake huwa nafanya assumptions zangu lakini siridhiki na majibu yangu. Halafu kama vile tulikuwa wote Ilboru au sijui nakufananisha?
 
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?
Kuna hili moja kubwa limeniingia kichwani sasa hivi.. SWALA la MUUNGANO..

1. Je, kwa kumpendekeza Membe ataweza vipi kumaliza swala hili la Muungano ikiwa Undani wa hoja yao ni madaraka tu. Madai yote wanayoyafanya ni kutokana na kwamba Marais wetu wametoka Bara.

Hivyo inawatia shaka sana maana alipokuwa Mwinyi rais hawakuona wala kuhisi Wametawaliwa. Hivyo rais akitoka Zanzibar hizi fujo na makelele yote hutayasikia maana kwao rais na waziri mkuu (Jamhuri ya Muungano) kutoka bara bara ni rais wa Tanganyika sio wa Wazanzibar.

2. Je. ktk muundo wa katiba mpya, kuna haja na sababu ya kuondolewa nafasi ya makamu wa rais ili Waziri mkuu ndiye awe wa mapokezano na apewe mamlaka atakayopunguziwa rais?..
 
Mtazamo wangu juu ya Mh. Membe kama chaguo la ccm kwa nafasi ya Urais-2015 nilishautoa hapa toka 27th December 2011 13:56:

Hii inathibitisha ni kiasi gani hujui kufanya uchambuzi. Nakushauri siku nyingine kabla ya kuandika fanya utafiti kwanza maana utadharirika ktk jamii kwa kutaka kujionesha unayajua mambo.

Ili upate
 
Watanganyika bwana. Hivi nchi hii haina watu wengine wenye uwezo wa kuiongoza nchi hii na kuipeleka kwenye neema?. Mpaka turudie wale wale tu?. Hebu fuatilia uhusiano wa Membe na JK ndipoi utashikwa na kizunguzungu.
 
Mkuu Mwanakijiji,Subiri kashfa ya pesa za Libya ndio utawajua vizuri wanasiasa wetu wana sura gani ni mapema mno kumjadili huyu nyoka wa mdimu.Ni bora mchawi Lowasa tumkabidhi mwana.
Hivi pesa ya libya hata kama kweli hicho kitu kipo iliathiri vipi maisha ya mwananchi wa kawaida kama kupanda kwa gharama za umeme kwa kujitakia?
 
Hivi pesa ya libya hata kama kweli hicho kitu kipo iliathiri vipi maisha ya mwananchi wa kawaida kama kupanda kwa gharama za umeme kwa kujitakia?
Pesa ya Libya ililenga kumnufaisha mwananchi mwenye kipato cha chini kupitia ajira kwa pesa hiyo kutumika kama mtaji,sasa fikiria hayo mabilioni yangeelekezwa katika uwekezaji wa kiwanda cha cement Lindi leo watu wangapi wangefaidika kiuchumi na kijamii.Ujenzi wa kiwanda cha cement ungetimiza ndoto ya mfuko wa cenment tsh 5,000/=,ebu fikiria hiyo pesa haikuwa mkopo hivyo isingekuwa mzigo wa madeni kwa taifa,gharama za ujenzi zingepungua(leo kupanga nyumba ni janga),sekta ya viwanda ingekua,uwezo wa mwananchi kujikimu ungeongezeka na vyanzo vya kodi kuimarika.Membe ni mbabaishaji alilenga kuchukua pesa ya Libya kwa manufaa yake ndio maana alikuwa anashupalia haitambui NTC ili awaibie walibya.Alisukumwa na nini mpaka aende katika kipindi cha dakika 45 mara tatu kuelezea sakata lile lakini leo mzozo wa mpaka na Malawi hana muda huo.Atupishe 2015 tuchague kiongozi wetu hatutaki tena kupoteza muda kwa viongozi wanaobebwa na vyombo vya habari na makuwadi wao wa siasa.
 
Bado mzee mwanakijiji unafikiria mgombea urais kutoka ccm???ukimtoa magufuli nani mwingine anaweza akaongea mbele ya watanzania wakamwamini????membe mnafiki mara nyingi hayuko tayari kusimamia kile ambacho yeye anakiamini,hii ni mbaya kuwa na rais wa mtindo huu kwa mfano,chenji ya rada alikomaa kweli na kufikia hatua hata kutaka kutaja waliohusika kwenye deal ya rada lakini kikwete alivyosema tu hakuna rushwa kwenye ununuzi wa rada akanywea,kama mzalendo angeasimamia kauli yake na mwisho wa siku watanzania wangeona ni mtu ambaye anaweza kuwatoa kwenye tope walilozama miaka 50,membe bernard kamilius hana msimamo hata kidogo,labda magufuli naweza mpa kura yangu akipitishwa,!!!!!!!!!!!
 
Huyu anayelalamikiwa kusaini mkataba bila kuusoma? Sikiliza hiyo video.

[video=youtube_share;_TFVLnRSOtg]http://youtu.be/_TFVLnRSOtg[/video]
 
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?

Hii Kali
CCM wakimsimamisha Membe ndo mwisho wao, sema mmnamuogopa Lowasa. Japo ni fisadi lakini krosi zake zinaweza wasumbua sana, hasa pale anapopiga kona na kuwahi langoni na kuiogonga kichwa mwenyewe.

CCM, itasalia salama pale watakaposema sasa rafu zimetosha, tutumie demokrasia ya ukweli kumpata mgombea wao yeyote wa uraisi. CCM wakitumia demokrasia ya kweli bila rushwa wala mizengwe kumpata mgombea wao. Urais wataupata na ccm itazaliwa upya.
 
sasa ndugu zangu, unajuaa tatizo la CCM ni makundi ambayo mpaka sasa hivi yanaendelea katafuna chama kwani unaposema tuhamasishe membe apite urais 2015, usiwasahau akina SITA na LOWASA, nasema hivyo kwa sababu mgombea urais wa CCM 2015 anateuliwa na NEC kupitia wajumbe wake, tumeona kambi ya LOWASA ikifanya kweli kwenye uchaguzi wa mwaka huu, mathalani UWT na sasa UVCCM. Hahaaaaa! kiongozi hapendekezwi kwa maneno ni mchakato mrefu.
KWA HIYO MEMBE ANA KAZI KUBWA SANA YA KUJIJENGA KWA WANA CCM NA SIO VINGINEVYO.
HATA TUKIONGEA SANA NA KUMPAMBA SANA LAZIMA AJIIMARISHE.

NI HAYO TU KWA LEO
 
wizara ya mambo ya nje ni kichaka kinachotumiwa na ccm kuwahifadhi watu dhaifu ili waje wawe viongozi., wakiwa kwenye wizara hiyo utendaji wao hauonekani moja kwa moja kwa watu kwa kuwa wizara hiyo haigusi moja kwa moja maisha ya raia. rejea maraisi wote wa tz waliotokea wizara hiyo then wakawa marais uone how valid my argument is
 
Kwa mtazamo wangu binafsi CCM wakiacha kumsimamisha Membe kugombea urais hakutakuwa na mabaki ya CCM. Kadhalika wakijaribu kuyaua makundi haya mawili CCM nayo itakufa. Nafafanua:

Lowasa hauziki kwenye chama chochote na chama kitakachomchukuwa kitakuwa kichekesho. Kwa mantiki hii CCM hana cha kupoteza asipomweka Lowasa kugombea. Cost za kumpitisha Lowasa katika CCM ni kubwa kuliko faida kisiasa. Kukazia point hii labda niulize ni lini Lowasa alikemea rushwa na ufisadi unaolimaliza chama chake? Je dhana ya kujivua gamba Lowasa anaiongeleaje? Hata yote ndiyo yanayokitafuna chama na kadhalika yanamtafuna Lowasa. CCM ikimchagua agombee ndio utakuwa mwisho wa CCM maana wapinga rushwa na ufisadi watapiga kura ya hasira itakayokifuta CCM.

So far Membe anauzika ndani na nje ya CCM. Ili Membe, ambaye si tajiri kama Lowasa ashinde, lazima CCM wakubali mapinduzi ndani ya chama. Kitu ambacho walafi wa chama chake hawatakipenda. CCM wana mtihani mkubwa, kukumbatia mafisadi na kuwapa nchi au kuokoa chama kwa kuwapa uongozi kundi la Membe.

Jaribio lolote la kuua makundi haya ni sawa na kukubali kwamba ufisadi na rushwa ndio sera ya CCM. Makundi haya ni njia sahihi ya chama kujisafisha.
 
BM hatoshi.Hana weledi na ushawishi kwa wananchi!Ndani ya CCM na Vyama mbadala watu hao wapo ingawa sioni watu wakiwajadili
 
sasa ndugu zangu, unajuaa tatizo la CCM ni makundi ambayo mpaka sasa hivi yanaendelea katafuna chama kwani unaposema tuhamasishe membe apite urais 2015,

NI HAYO TU KWA LEO
Hayo makundi Mzee Mwanakijiji kayaona kwa chadema peke yake na ndiyo sababu kubwa anayosema kwamba hawataweza kushinda uchaguzi ama hawatakiwi kushinda uchaguzi(not ready to lead),sikujuwa sababu ya yote hayo ni Membe.
 
Membe wa nini hata hatufanyi tujiandae vilivyo.Tunataka Lowasa ili tuone utaalamu wake wa political asssnation utakavyovurugwa na MOVEMENT FOR CHANGE. Tunamtaka mkuu wa genge la wagombea watoa rushwa wakuu walozoea kuwaliza wana ccm wenzao. Akiteuliwa Membe atasababisha Lowasa aendelee kutamba kuwa bado yuko fiti kumbe kundi lake linashinda wenzao kugawa mshiko
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?
 
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?

View attachment 69116 ndio mtu pekee afaaye kuwa Rais wa nchi hii
 
Back
Top Bottom