Hoja funga mwaka: Ni kitu gani kisifanyike 2017 ndani ya utawala wa Rais Magufuli?

Raisi na misafara yake watumie magari ya vitz na spacio ili kuendeleza Sera ya kubana matumizi.
 
Mahakama ya mafisadi ipate wateja!Kuna yale makundi aliyilenga wakati wa kampeni,tukajua ndio wakwanza kufikishwa huko!
Nasema 2017,afukue makaburi!
 
Ajifunze kutokana na kukosolewa, Asijisifie kuwa ameondoa watumishi hewa kwani ni uchi wa familia yao(CCM), Apunguze misifa ya kijinga kwa upande wake na viongozi wake wanamuangusha, amuombe Mwenyezi Mungu azidi kumshushia maadui au upinzan ili aendelee kujiimarisha...Yeye siyo Mungu....
 
Bunge lioneshwe live maana wapo mle sababu ya wananchi, kwa nini watufiche wananchi kinachoendelea bungeni?

Atafute hizo pesa za kuonesha bunge
 
Wakuu wa mikoa na wilaya wamekua miungu watu kazi yao kusweka watu ndani,kazi hawawezi wamebaki kufabya siasa badala ya kazi za maendeleo
 
Mimi nalia na ukimya kwenye kutangaza makusanyo ya kodi TRA. Mbona mwezi November hatujaambiwa tumekusanya ngapi? Au zisipofika trilioni hatuambiwi kitu?

Pia mwanzoni pale tulipewa na breakdown ya matumizi, huu utaratibu uendelee.
 
Aanzishe mchakato wa katiba mpya, kama sio katiba mpta yote basi afanye ammendment ya zile parts zinazolalamikiwa sana ( lakini i know hii hoja ueye kama yeye hawezi kuianzisha, wabunge wapeleke hoja hii bungeni)
Bila katiba mpya au ammendment ya zile zinazolalamikiwa basi tutaendelea kulia eer day n night..
 
Asitumie muda mwingi kupambana na uhuru wa kupata habari.

Apambane na umasikini,ukosefu wa ajira,ufisadi na matatizo mengi aliyoyaahidi wakati wa kampeni kwamba atayatatua 2020 siyo mbali yeye anatumia muda mwingi na Polisi wake kupambana na wanaomkosoa.
 
Rais asafiri.. Akamuulize Trump kwanini anajaza mamilionea Kwenye serikali yake na siyo ma proffessa
 
Kuna baadhi ya vichwa upinzani awateue Kwenye nafasi mbali mbali e.g. Halima Mdee, Mnyika, Nasari.
 
Uhuru wa kutoa habari uwepo kwa 100% bila kusumbuliwa mtu yeyote. Vyama vya siasa viruhusiwe kuendesha mikutano na kufanya mambo yake bila bughla.
 
Wakuu nataka mfunguke tukielekea kumaliza mwaka nadhani rais Magufuli atapitia hapa na achukue maoni kwa ajiri ya kuanza mwaka mpya 2017.

Nini kinakuchukiza ndani ya utawala wa rais magufuli ambacho unataka ajirekebishe mwaka 2017?.

Binafisi Mimi swala lililonichanganya mwaka huu ni kitendo cha kubadilisha matumizi ya Rambi rambi ya wahanga wa bukoba hili swala limeniuma sana, likitokea janga jingine naona kama itakuwa ngumu watu kuchangia.

Je kwako ni nini?

Iwe ni mambo anayoyafanya yeye au wateule wake au serikali kwa ujumla hata ikiwezekana huko uliko mtaani au kijijini ongea kwa Uhuru..

Sema mambo usiyapenda yaendelee mwaka mpya 2017 hapa .

NB : Mod naomba mfatilie mjadala na kuondoa threads yeyote itakayoletwa hapa kukiuka na kutoka nje malengo ya tunacho discuss,ili wasilete hapa uchama ni kwa maslahi ya taifa tu.

Lengo langu Rais apitie hapa na kuchukua maoni ya wananchi wanachokitaka kuelekea 2017 maana sasa hivi hata waliopo vijijini tupo nao humu wengi.
Mapambano yaendelee dhidi ya wapiga dili mpaka wanyooke,bila kujali kelele za wanafiki !
 
Ziendelee kudumu fikra za mwenyekiti wa chama!!!!!!maana hata tukitoa ushauri is nothing kwake!!!!!
 
Back
Top Bottom