Uchaguzi 2020 Hoja fikirishi: CHADEMA kwanini mnadai Uhuru wa Vyombo vya Habari huku mkivinyima haki, kufukuza na kuvidhalilisha!?

Dam55

JF-Expert Member
Oct 8, 2015
5,592
11,831
Nasikitika kusema kwamba sera hii sasa inakosa mashiko kabisa kwa hiki kilichotokea leo hii.

Ni ngumu sana kuamini watu wanao pigania Uhuru wa vyombo vya habari kushindwa kuwa wavumilivu na kuviacha vyombo hivyo vifanye kazi kwa Uhuru na utashi wao.

Kama kweli CHADEMA inapigania Uhuru wa Vyombo vya Habari basi wangeacha TBC warushe mkutano wao kwa Uhuru bila ya kushinikizwa kufanya hivyo kwa matakwa ya CHADEMA.

Ifahamike kuwa TBC ni chombo Cha habari Cha Taifa hivyo basi hakiwezi kurusha matamko yoyote yenye viashiria vya kueneza Chuki na uvunjifu wa amani. Ni lazima wafanye uchambuzi wa kipi kinayakiwa kiwafikie watanzania sasa matamko ya viongozi wa CHADEMA hayakuwa mazuri.

Mfano ni Tundu Lissu alikuwa akisema haya.
"Kama wanategemea tutajitoa kwenye Uchaguzi huu, hilo wasahau. Kwenye kila mkutano wetu wa kampeni, wananchi nchi nzima muanze mikutano kwa maandamano ya amani kudai wagombea wetu warudishwe bila masharti yoyote. Watanzania msikubali kukaa kimya tena,"

"Tunaziomba Jumuiya za Kimataifa zituunge mkono katika jambo hili la kupigania wagombea wa vyama vya upinzani ambao wameunguliwa kwasababu za kihuni maana jambo hili ni kinyume pia na sheria za kimataifa.."

Rais Magufuli aliwaambia wasimamizi wa Tume ya uchaguzi, ambao ni wateule wake, “Siwezi kuwalipa mishahara mikubwa na magari mazuri, halafu mkatangaze wapinzani kuwa washindi kwenye uchaguzi.” Haya ni matokeo ya maelekezo hayo!


Screenshot_20200828-182423.png
Screenshot_20200828-182456.png

Sasa Chombo Cha habari Cha Taifa hakiwezi kutangaza kauli za namna hiyo popote pale dunia sio kwa Tanzania tu pekee.

Mhe Mbowe alienda mbali zaidi na kusema kuwa hawana haja ya kunadi Ilani ya uchaguzi badala yake wanatakiwa wananchi wakadai haki, alipoanza kudai kuwauliza watu kuwa wangapi wapo tayari kwenda kudai haki ndipo hapo TBC wakakata matangazo walipo rudi hewani mhe Mbowe akawapa dk 15 waondoke kwenye mkutano wao.

Je huu Uhuru wa vyombo vya habari tunao upogania ni upi hapa ikiwa hawataka kuviacha vyombo vya habari vitangaze kulingana na weledi wao ? Kwanini walitaka TBC watangaze kwa matakwa ya CHADEMA tu?.
IMG_20200828_182231.jpg


Katika hili CHADEMA mnajiharibia wenyewe.
IMG_20200828_182213.jpg


Je hiki walicho kifanya leo CHADEMA hakijawanyima haki watanzania kupata habari? Huu sio ukandamizaji wa vyombo vya habari?
 
Nilikuwa nafuatilia kupitia TBC, bora hata walivyowafukuza. Kila yule jamaa akitupiwa mawe, walikuwa wanakata sauti.

Ajabu, Rais anapowatukana watumishi wake mbele ya Camera, huwa hawakati sauti yake ya matusi anayorusha dhidi ya wateule wake.

Nadhani matusi ya Rais ndiyo yanafaa, ila yeye haipendezi akitukanwa. Mimi binafsi huwa nakwazika sana kuona wateule wanatukanwa mbele ya waTanzania wote.

Anyway, kuna nukuu kwenye Biblia inasema hivi.

na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.

Jamaa anapenda kuwapimia wenzake matusi, awe anavumilia akitupiwa matusi na wengine.
 
TBCMMM walistahili kufukuzwa!Yaani JPM asisemwe mabaya yake?Hii ndio kampeni,unaeleza utakayofanya lakini pia unaeleze mapungufu ya mshindani wako!Sasa kwanini kila JPM akiguswa walikuwa wanakata matangazo?Fukuza kabisa hao TBCcM
Wanatakuwa wafanye kazi kwa Uhuru siyo kwa matakwa ya CHADEMA
 
Nasikitika kusema kwamba sera hii sasa inakosa mashiko kabisa kwa hiki kilichotokea leo hii.View attachment 1550952

Ni ngumu sana kuamini watu wanao pigania Uhuru wa vyombo vya habari kushindwa kuwa wavumilivu na kuviacha vyombo hivyo vifanye kazi kwa Uhuru na utashi wao.
Kama kweli CHADEMA inapigania Uhuru wa vyombo vya habari basi wangeacha TBC warushe mkutano wao kwa Uhuru bila ya kushinikizwa kufanya hivyo kwa matakwa ya CHADEMA.

Ifahamike kuwa TBC ni chombo Cha habari Cha Taifa hivyo basi hakiwezi kurusha matamko yoyote yenye viashiria vya kueneza Chuki na uvunjifu wa amani. Ni lazima wafanye uchambuzi wa kipi kinayakiwa kiwafikie watanzania sasa matamko ya viongozi wa CHADEMA hayakuwa mazuri.
Mfano ni Tundu Lissu alikuwa akisema haya.
"Kama wanategemea tutajitoa kwenye Uchaguzi huu, hilo wasahau. Kwenye kila mkutano wetu wa kampeni, wananchi nchi nzima muanze mikutano kwa maandamano ya amani kudai wagombea wetu warudishwe bila masharti yoyote. Watanzania msikubali kukaa kimya tena,"
"Tunaziomba Jumuiya za Kimataifa zituunge mkono katika jambo hili la kupigania wagombea wa vyama vya upinzani ambao wameunguliwa kwasababu za kihuni maana jambo hili ni kinyume pia na sheria za kimataifa.."
Rais Magufuli aliwaambia wasimamizi wa Tume ya uchaguzi, ambao ni wateule wake, “Siwezi kuwalipa mishahara mikubwa na magari mazuri, halafu mkatangaze wapinzani kuwa washindi kwenye uchaguzi.” Haya ni matokeo ya maelekezo hayo!


View attachment 1550921View attachment 1550922

Sasa Chombo Cha habari Cha Taifa hakiwezi kutangaza kauli za namna hiyo popote pale dunia sio kwa Tanzania tu pekee.

Mhe Mbowe alienda mbali zaidi na kusema kuwa hawana haja ya kunadi Ilani ya uchaguzi badala yake wanatakiwa wananchi wakadai haki, alipoanza kudai kuwauliza watu kuwa wangapi wapo tayari kwenda kudai haki ndipo hapo TBC wakakata matangazo walipo rudi hewani mhe Mbowe akawapa dk 15 waondoke kwenye mkutano wao.

Je huu Uhuru wa vyombo vya habari tunao upogania ni upi hapa ikiwa hawataka kuviacha vyombo vya habari vitangaze kulingana na weledi wao ? Kwanini walitaka TBC watangaze kwa matakwa ya CHADEMA tu?.View attachment 1550947

Katika hili CHADEMA mnajiharibia wenyewe.View attachment 1550950

Je hiki walicho kifanya leo CHADEMA hakijawanyima haki watanzania kupata habari? Huu sio ukandamizaji wa vyombo vya habari?
Chadema haikuwanyima haki watanzania TBC ilikuwa ikifanya uchambuzi wa vyama vyote badala ya kutuacha tuusikilize mkutano, kwani ukisema ukweli wa kilichotokea kuna hasara gani! Maneno yaliyosemwa ni marudio ya tuliyoyasikia TBC muhusika alipoyasema huko nyuma, usituaminishe kuwa amesingiziwa.
 
Chadema haikuwanyima haki watanzania TBC ilikuwa ikifanya uchambuzi wa vyama vyote badala ya kutuacha tuusikilize mkutano, kwani ukisema ukweli wa kilichotokea kuna hasara gani!
Tatizo liko wapi? hata kama wakitoa uchambuzi huoni kama walikuwa wakitimiza majukumu yao na wanapaswa waachwe wafanye kazi yao kwa uhuru?
 
..walichukuwa wanafanya TBC ni kitu kibaya sana.

..kwasababu kingeweza kuwa ndio utaratibu rasmi wa vyombo vya habari ktk kutangaza kampeni za upinzani.

..kwa kweli ilikuwa inakera sana. nadhani walichokifanya kiwaudhi watu wengi, hata wasioiunga mkono CDM.

..waTz siyo wajinga kwamba hawawezi kuchuja mambo yanayosemwa na CDM na kuchukua hatua sahihi.
 
Nilikuwa nafuatilia kupitia TBC, bora hata walivyowafukuza. Kila yule jamaa akitupiwa mawe, walikuwa wanakata sauti.

Ajabu, Rais anapowatukana watumishi wake mbele ya Camera, huwa hawakati sauti yake ya matusi anayorusha dhidi ya wateule wake.
Wewe baba yako anapomtukana mama yako huwa unaingilia? Mama yako akimtukana baba yako utajitajidi uzuie hayo matusi yasiendelee
 
Nasikitika kusema kwamba sera hii sasa inakosa mashiko kabisa kwa hiki kilichotokea leo hii.View attachment 1550952

Ni ngumu sana kuamini watu wanao pigania Uhuru wa vyombo vya habari kushindwa kuwa wavumilivu na kuviacha vyombo hivyo vifanye kazi kwa Uhuru na utashi wao.
Kama kweli CHADEMA inapigania Uhuru wa vyombo vya habari basi wangeacha TBC warushe mkutano wao kwa Uhuru bila ya kushinikizwa kufanya hivyo kwa matakwa ya CHADEMA.

Ifahamike kuwa TBC ni chombo Cha habari Cha Taifa hivyo basi hakiwezi kurusha matamko yoyote yenye viashiria vya kueneza Chuki na uvunjifu wa amani. Ni lazima wafanye uchambuzi wa kipi kinayakiwa kiwafikie watanzania sasa matamko ya viongozi wa CHADEMA hayakuwa mazuri.
Mfano ni Tundu Lissu alikuwa akisema haya.
"Kama wanategemea tutajitoa kwenye Uchaguzi huu, hilo wasahau. Kwenye kila mkutano wetu wa kampeni, wananchi nchi nzima muanze mikutano kwa maandamano ya amani kudai wagombea wetu warudishwe bila masharti yoyote. Watanzania msikubali kukaa kimya tena,"
"Tunaziomba Jumuiya za Kimataifa zituunge mkono katika jambo hili la kupigania wagombea wa vyama vya upinzani ambao wameunguliwa kwasababu za kihuni maana jambo hili ni kinyume pia na sheria za kimataifa.."
Rais Magufuli aliwaambia wasimamizi wa Tume ya uchaguzi, ambao ni wateule wake, “Siwezi kuwalipa mishahara mikubwa na magari mazuri, halafu mkatangaze wapinzani kuwa washindi kwenye uchaguzi.” Haya ni matokeo ya maelekezo hayo!


View attachment 1550921View attachment 1550922

Sasa Chombo Cha habari Cha Taifa hakiwezi kutangaza kauli za namna hiyo popote pale dunia sio kwa Tanzania tu pekee.

Mhe Mbowe alienda mbali zaidi na kusema kuwa hawana haja ya kunadi Ilani ya uchaguzi badala yake wanatakiwa wananchi wakadai haki, alipoanza kudai kuwauliza watu kuwa wangapi wapo tayari kwenda kudai haki ndipo hapo TBC wakakata matangazo walipo rudi hewani mhe Mbowe akawapa dk 15 waondoke kwenye mkutano wao.

Je huu Uhuru wa vyombo vya habari tunao upogania ni upi hapa ikiwa hawataka kuviacha vyombo vya habari vitangaze kulingana na weledi wao ? Kwanini walitaka TBC watangaze kwa matakwa ya CHADEMA tu?.View attachment 1550947

Katika hili CHADEMA mnajiharibia wenyewe.View attachment 1550950

Je hiki walicho kifanya leo CHADEMA hakijawanyima haki watanzania kupata habari? Huu sio ukandamizaji wa vyombo vya habari?

Cdm hawahitaji kutangazwa na TBC, bali wanahitaji uhuru wa vyombo vya habari, na TBC sio chombo huru cha habari. TBC wakatangaze vyama vingine na sio cdm tafadhali. Cdm imefika hapo ilipo bila msaada wowote wa kutangazwa na TBC.
 
Back
Top Bottom