Hofu ya Mbowe na CHADEMA juu ya Zitto

Hofu ya Mbowe na CHADEMA juu ya Zitto

sultani --------- zzk muacheni jamani ameshapata cheo anachokipenda unchallenged supreme leader
Ila kweli mkuu dogo anapenda sana uongozi ndiyo maana wamempa kiongozi mkuu mana wanamjua kitabia chake cha ulafi wa uongozi. Akipewa nchi huyu atakuwa kama Adolf Hitler atake kutawala dunia nzima, mwache na ACT yake tuone kama ataweza kufanikisha lengo lake
 
CHADEMA hawakupaswa kumfukuza Zitto kwanza ijapokuwa ni kweli alishaharibu na alistahili kufukuzwa. Ila wengeuangalia mustakabali wa upande hasi wa kumfukuza, kuhusu CDM baada ya kufanya vle.

Mm naona kwmb wangebebana nae hivyohivyo angalau uchaguzi mkuu upite kwanza then ndo wamfukuze. Tatizo nalo ni kwamba, wanasheria wa CDM wana papara sana na hawana ushawishi mkubwa ndani ya chama.
Kuishi na mzoga ndani utawezaje kuvumilia maizi nafunza na harufu kali.tupa nje mafisi yajinafasi.zzk ni mhaini ndani ya cdm.hafai na asidhani watu wanamfagilia ktk mikutano yake.anazidi kuoza huyu
 
Usaliti hauvumiki, unaweza ukavumilia uchoyo hata wizi lakini si kwa usaliti
 
Kuishi na mzoga ndani utawezaje kuvumilia maizi nafunza na harufu kali.tupa nje mafisi yajinafasi.zzk ni mhaini ndani ya cdm.hafai na asidhani watu wanamfagilia ktk mikutano yake.anazidi kuoza huyu

Chadema walikosea wangemvua nyazfa zote za uongozi lakini wangemwacha na uanachama wake.. ukweli ni kwamba ushawishi wa zitto kwenye medani za kisiasa ni mkubwa labda kuliko kiongozi yeyote wa CDM kwa sasa. Na ijulikane kuwa vijana wengi walijiunga na cdm kwa ajili ya zitto. Huo ndio ukweli japo unauma. Sasa yeye anasonga wakati viongozi cdm wanashikana mashati kwa kosa walilofanya la kumfukuza zitto... yetu macho!
 
Kama unaakiri timamu huwezi kuongea upumbavu ambao hauna maana wwe ni kati yao ambao mnatumiwa huna jipya zaidi ya uraghai tu ulishawahi kusikia mbowe au slaa wametoa matamko kuhusu zitto.
 
CHAMVIGA :
Akizungumza mjini Morogoro zitto alisema
"Kuungana ni jambo jema...na tunawatakia kila la
kheri UKAWA...sisi hatugombani na mtu bali na
umaskini. Chama chetu ni cha
wanyonge...tukikuta mnyonge na tajiri
wanapigana sisi tutamsaidia mnyonge kwanza
baadae ndio tutauliza nani mchokozi (makofii).
Kuna watu wanasema hawa wakina zitto
wamekuja kugawa kura za upinzani....nataka
niwahakikishie wana Morogoro ACT haijaja
kugawa kura za upinzani....Mwaka 2010 asilimia
42 tu ya watu waliojiandikisha ndio walipiga
kura....ina maana 58% ya waliojiandikisha
hawakupiga kura na inamaana hawakuwa na
chama chochote kile.ACT imekuja kukonga nyoyo
na kuwashawishi hawa 58% hivyo hatugawi kura
za mtu yoyote."
Hayo ni baadhi ya maelezo ya Ndugu Kabwe
katika hotuba yake ya Jana kwa wana morogoro.
Nionavyo.
Mwacheni Zitto afanye siasa zake Watanzania
wataamua".
 
Kama unaakiri timamu huwezi kuongea upumbavu ambao hauna maana wwe ni kati yao ambao mnatumiwa huna jipya zaidi ya uraghai tu ulishawahi kusikia mbowe au slaa wametoa matamko kuhusu zitto.

Ndugu kusoma hujui hata picha nayo huoni??
 
Usaliti hauvumiki, unaweza ukavumilia uchoyo hata wizi lakini si kwa usaliti

Na hivi ndivyo alivyowajibu


Morogoro. Kiongozi wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amesema hawezi kulumbana na viongozi wa chama chake cha zamani cha Chadema kwa kuwa anachofanya sasa ni kutafuta wanachama wa chama chake kipya.

Zitto alisema hayo jana mjini Morogoro wakati wa mkutano wa ziara ya uzinduzi wa chama hicho uliofanyika katika kiwanja cha ndege mjini hapa.

Akihutubia huku akishangiliwa na wananchi, Zitto aliwataka kumpima na kumchuja yeye kwa matendo yake na kwamba kwa sasa jitihada zake amezielekeza mikoani kupata wanachama.

“Nimekuwa nikisikia maneno maneno mengi kutoka kwa viongozi wangu wa zamani lakini nawaheshimu na sitoweza kuwajibu kwani siasa za chuki kwa sasa zimepitwa na wakati, ninachofanya ni kukijenga chama,”alisema Zitto.

Kiongozi huyo alisema Morogoro ni moja ya mkoa unayoifanya nchi kukosa maendeleo kutokana na viwanda vingi kubinafsishwa na hivyo kutokuwa na faida kwa wananchi.

“Morogoro ni mkoa wa sita katika kuchangia pato la Taifa na takribani Sh2.2 trilioni zimekuwa zikipatikana kwa ajili ya maendeleo ya watu wa mkoa huo,” alisema Zitto.

Mwenyekiti wa chama hicho, Anna Mghwira aliwataka wanawake nchini kuacha kushiriki siasa za vurugu na malumbano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Mghwira alisema ni vyema wakaangalia namna gani nchi inakua kiuchumi na watoto na vijana wanapata elimu iliyo bora ambayo itawafanya kufanya kazi kwa uzalendo.

Aliwataka wananchi kuwa na taratibu za kuwakumbuka mashujaa wa Taifa hasa kwa mambo mema na mzuri waliyoyafanya wakati wa uhai wao.

Mpaka sasa chama hicho cha ACT kimefanya mikutano yake ya uzinduzi katika mikoa ya Ruvuma, Njombe, Iringa na Morogoro na leo kitakuwa mkoani Dodoma kikiendelea kutafuta wanachama.
 
Kama huamini katika hilo basi wafuasi watiifu wa Mbowe wasingekuwa wanahangaika humu kumchafua Zitto bali wangekuwa deep kumwaga sera za chama chao

ally kanah tafadhari jibu swali ni kwanini CDM ilipoteza viti vya udiwani wakati zito yupo na viti vya ubunge kuchukuliwa na nccr mageuzi mbele ya huyo zito wako?
 
Kigoma hawachagui chama, wanachagua mtu

basi kigoma ni ya ajabu sana labda ndiyo maana wachumi huichukulia kigoma kama moja ya mikoa iliyo nyuma kimaendeleo ukiilinganisha na mikoa mingine. kwa sababu sera hutengenezwa na chama hivyo usipo chagua chama hujielekezi kwenye sera yoyote.
 
Nina swali. Kama Zitto alikuwa na ufuasi mkubwa kama mnavyosema, ilikuwaje 2010 majimbo mengi Kigoma yalichukuliwa na NCCR-Mageuzi?? Huo ufuasi uko wapi ni kwa maneno au matendo?

Aiseee!!!Una umri gani?Upo darasa la ngapi?
 
ally kanah tafadhari jibu swali ni kwanini CDM ilipoteza viti vya udiwani wakati zito yupo na viti vya ubunge kuchukuliwa na nccr mageuzi mbele ya huyo zito wako?

Ndugu mimi si msemaji wa Zitto...mm hapa nimeelezea tu hofu ya Mbowe Slaa na wahafidhina wa chadema dhidi ya Ndugu Kabwe

Na ndio maana nikasema sasa wahafadhina wa chadema wanacheza mziki wa Zitto na ushahidi wa hilo jaribu tu kupitia mabandiko mbali mbali humu jukwaani na kwenye mitandao mingine ya kijamii..

Badala ya wahafidhina wa Chadema kutumwagia sera za chama chao wao wamekaa tu kuzusha uongo na porojo kwa mtu ambaye wala hatujasikia kwenye mikutano yake akipeleka mashambulizi dhidi ya chama chake cha zamani wala viongozi wake wa zamani
 
Ndugu mimi si msemaji wa Zitto...mm hapa nimeelezea tu hofu ya Mbowe Slaa na wahafidhina wa chadema dhidi ya Ndugu Kabwe

Na ndio maana nikasema sasa wahafadhina wa chadema wanacheza mziki wa Zitto na ushahidi wa hilo jaribu tu kupitia mabandiko mbali mbali humu jukwaani na kwenye mitandao mingine ya kijamii..

Badala ya wahafidhina wa Chadema kutumwagia sera za chama chao wao wamekaa tu kuzusha uongo na porojo kwa mtu ambaye wala hatujasikia kwenye mikutano yake akipeleka mashambulizi dhidi ya chama chake cha zamani wala viongozi wake wa zamani


ni kweli huenda si msemaji wa zito,lakini kufuatia bandiko lako inaonyesha zito ni muhimu sana kiasi bila zito basi hakuna cdm ndipo niliporejea matokeo ya uchaguzi mkuu uliopitana kuona pamoja na zito matokeo ndiyo yalikuwa hayo labda uniambie zito ndiye aliye sababisha na hapo hoja ya usaliti inapata ushahidi.
 
Zito ni mwanasiasa smart kuliko mwanasiasa yoyote nchi hii,nyie na saccos yenu ya wachaga mtabaki mnaropoka tu na mwaka huu ndo mwisho kutafuna ruzuku,laana ya ubaguzi n udini itawatafuna poppote pale Kafulila alishasema Chadema hakuna demokrasia ila kuna harufu yake.

Hakuna mwanasiasa muislamu katika nchi hii aliyewahi kuwa smart..Zitto ni smart kwenye kundi la wajinga wenzie
 
ni kweli huenda si msemaji wa zito,lakini kufuatia bandiko lako inaonyesha zito ni muhimu sana kiasi bila zito basi hakuna cdm ndipo niliporejea matokeo ya uchaguzi mkuu uliopitana kuona pamoja na zito matokeo ndiyo yalikuwa hayo labda uniambie zito ndiye aliye sababisha na hapo hoja ya usaliti inapata ushahidi.

Inawezekana akawa muhimu ama akawa si muhimu kwa chadema hapo nakubaliana 100% na wewe ila mashaka yangu yanakuja kwanini mara baada ya kumfukuza na Zitto kuanza maisha mengine baada ya yale ya awali ya chadema sasa wahafidhina wa chadema wamekuwa kazi yao kubwa ni kumfuatilia Zitto kumzushia uongo na kila aina ya siasa majitaka na hatukuwahi kumsikia Zitto akikisakama chama chake cha zamani wala viongozi wake
 
Chadema walikosea wangemvua nyazfa zote za uongozi lakini wangemwacha na uanachama wake.. ukweli ni kwamba ushawishi wa zitto kwenye medani za kisiasa ni mkubwa labda kuliko kiongozi yeyote wa CDM kwa sasa. Na ijulikane kuwa vijana wengi walijiunga na cdm kwa ajili ya zitto. Huo ndio ukweli japo unauma. Sasa yeye anasonga wakati viongozi cdm wanashikana mashati kwa kosa walilofanya la kumfukuza zitto... yetu macho!

Wengi tulishajua ufisad wa ccm sio zitto
 
Back
Top Bottom