HLRC kuiburuza serikali mahakamani kuhusu NSSF

Mimi nafikiri kabla HLRC kufikisha suala hili mahakamani inawapasa wafanye utafiti kwanza kwani suala hili limepitishwa kisharia kabisa bungeni na wawakilishi wa wananchi wote ndanimwe wafanyakazi.

Jiulizeni je wao hawakuliona hilo?

Jiulizeni Je wawakilishi hao wanakatwa kodi ikiwemo hizo za social security?

Nasisistiza utafiti ni muhimu sana kabla kufika mahakamani.
 
Definitily hautakua mzigo wa private sector. Does that mean utakua mzigo wa "jamii"? Who is "jamii" by the way? Halafu, utakapokua 65 yrs old na umechangia toka ukiwa 25 yrs old (40 yrs ago then) na NSSF au PPF au XXX whatever wamekwisha "invest" pesa yako yote kwa uDOM na daraja la kigamboni na mishahara ya wafanyakazi serikalini na gharama za chaguzi kuu na group endowment schemes za wakurugenzi wake na yafananayo na hayo; utakuwa mzigo wa nani?
Inawezekana kweli wanaamini kama unavyoamini wewe kuwa hizo pesa ni za serikali si zangu ndio maana hawakuniomba maoni yangu kabla ya hii sheria eeh? Kweli SOCIAL SECURITY ya mtanzania ni MUNGU tuu hakuna kingine!!

ukiwa 65yrs old, na umeshakula mafao yako unakuwa mzigo kwa private sector au jamii?
 
Sijakupata vizuri Polisi, hapo kwenye shs 36,000. Hata hivyo hoja yangu ilikuwa kwenye criteria za kupata pension. Sijui kwenye haya mabadiliko ya sasa hivi wamefanya vipi, lakini ilivyokuwa ni kwamba ili mwanachama a-qualify kupata pension anatakiwa awe amechangia kwenye mfuko huo si chini ya miaka 10, na pia awe amefikia umri wa kustaafu. Kama umechangia kwa miaka 10 na zaidi lakini ukaondoka kwenye ajira kabla ya umri wa kustaafu (55 or 60 yrs) basi ulikuwa unaangukia kwenye withdrawal benefit.

Kumbukuka hii mifuki ina mafao (benefits) 7 hadi nane, na kila moja lina criteria zake.

Kuhusu unemployment benefit, its true kwa Tanzania hakuna kitu cha namna hiyo na hili fao la withdrawal kwa kiasi limekuwa ndio kimbilio la watu wanaoondoka kwenye ajira kabla ya umri wa kustaafu. Na limekuwa kwa kasi kubwa hasa baada ya kufanya reforms kwenye public sector - ambapo wafanyakazi wengi walipunguzwa, au/na mashirika kuuzwa.

Mkuu sina jibu sahihi. Kuna mambo mengi ambayo hayapo wazi ikiwemo hilo la kwako. Copy & paste za sheria za wenzetu ndo inatutafuna
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Jamani chama cha magamba na serikali yake wanatafuta hela za uchaguzi mwaka 2015....wamecalculate kwamba life expectancy ya mtanzania ni miaka 45...so wana uhakika wa kujichotea mapesa ya watu watakaofariki kabla ya ya kufikisha miaka 55 na kutumia kununualia kapelo za kijani kanga pikipiki tisheti kwa ajili ya kampeni...they are very strategic... ni serikali pumbafu tu ndio inaweza kufikiri kuimpliment sheria kama hii....nin wasiwasi kama wabunge wetu wanajua wanachokifanaya dodoma...bahati mbaya dhaifu nae huwa anasaini tu bila kusoma kilichoandikwa
 
We shetani suala hapa sio maandalizi. Soma topic, acha umajinuni.

Mkuu kama nimesema ubaya, shuhudia huo ubaya wangu. Kama nimesema vema, matusi ya nini? Mifuko ya jamii haiwezi na wala haitatoa SOCIAL SECURITY. Mifuko ya jamii inatoa PENSIONS. Social security inatolewa na SERIKALI kama vile matibabu ya bure au bima ya afya kwa wazee, wasiojiweza, walemavu, yatima n.k. Pia hutolewa kwa vijana wasiokuwa na ajira yaani unemployment benefits, kwa askari ana jamaa zao waliothirika vitani na mambo kama hayo na yanatokana na KODI ya wananchi. PENSIONS ndo inatolewa na mifuko ya jamii kutokana na michango ya WANACHAMA. Please note:
SOCIAL SECURITY - KODI YA WANANCHI
PENSIONS - MICHANGO YA MWANACHAMA
Acha kujifanya unajua wakati hujui, keng*e wewe
 
Wakati fulani nilkuwa kusema hapa CDM wanatakiwa kutumia matukio ya kila siku kujijenga kuliko kukomaa na fedha za EPA........hii hoja nakwambia wafanyakazi wote inagusa na inaweza kuwa kampeni ajenda ya kuing'oa CCM nimeudhika sana.....wapi CHADEMA nilitegemea uongozi wa CDM ungeiitisha press conference kuwa pamoja na sheria hii kupita kihalali bungeni lakini tumegundua wananchi(wafanyakazi) hawaitaki hivyo sisi kama wawakilishi wao tunaipinga sheria hii na tunaandaa mikutano na maandamano ya kuipinga. Nakwambia ungeona umati wa watu ambao ungejitokeza njia ya mahakama itatuchelewesha maana itapigwa kalenda hadi tusahau
 
Hiyo link sio sahihi. Ni ya watumishi wa serikali ambao kwa hapa Tanzania wapo chini ya GEPF. Kuna tofauti kubwa sana kati ya Pension fund and provident fund. Kwa wenzetu hata watumishi wa serikali hawapeleki michango provident kwa vile mafao ni madogo wanapeleka pension scheme maalum ndio maana ina hizo sheria. Kama hufahamu serikali huwa haipeleki michango kwenye pension scheme licha ya makato ila wanalipa kwa fungu la bajeti wakishajua idadi ya watu wanaostaafu mwaka huo.
Dah ama kweli nyie wagumu sana kuelewa poicha nzima mnaliwa vipi.. Nikuulize NSSF ni chombo cha serikali au sio? Ni mpango wake ni private pension plan au umepitishwa na serikali?. mbona mnajipinga wenyewe kwa kila hatua au hamfahamu kilichopo mbele yenu..

Serikali ipo juu ya watumishi wa Umma na mashirika binafsi maadam kuanzishwa kwa NSSF kumetokana na serikali na sheria kutungwa na bunge. Ndio maana HLRC wanaona uvunjaji wa sheria kwa mtazamo wa zile pension schemes wakati NSSF sio private corporate ni mali ya serikali (shirika la Umma) linalomilikiwa na serikali na linatakiwa kutoa huduma sio kufanya biashara.

Private Pension plan zipo za kila aina huku kuna za walimu (Teachers Pension Plan) na hata mashirika kama la simu Bell lina Pension plan zake. Mabenki na financial institution kibao zinafanya biashara kupitia michango ya watu ktk malipo ya uzeeeni lakini haya ni mashirika binafsi - Corporates. Hawa huchagua Board of Directors, wana vikao, na mikutano yao na siku shirika likienda chini insurance company za benki kubwa ndio huwajibika kulipa madeni na sio serikali..Hakuna kitu kinajadiliwa bungeni wala kusubiri saini ya rais ili iwe sheria.. they are private. Ukirudi kwa NSSF unakuta story tofauti kabisa..Hili ni serikali kupitia shrika la Umma linaloendesha biashara ya uwekezaji for profit kama private corporate kinyume kabisa..

Tatizo sio kwamba NSSF inashughulika na kina nani.. iwe watumishi wa mashirika binafsi au ya Umma swala ni NSSF yenyewe ni shirika gani na linamilikiwa na kudhaminiwa na nani kama sio serikali?..Mashirika yote haya nyumbani ni ya serikali na ndio maana sheria zake zinapitishwa bungeni, hizi ni SOCIAL SECURITY programs zinayoandaliwa na serikali kutokana na michango na earnings ya raia waajiriwa na hapa ndipo mliposhindwa kuona ndani..

Kwa hiyo HLRC wana kesi kwa sababu sheria za chombo chochote cha serikali ktk maswala ya social security ni lazima sheria zipitishwe na bunge, na wakati mwingine huhitaji kura za maoni ya wananchi kubadilisha sheria hizo wengine huweka 2/3 ya population lakini katika hili la NSSF hatukuona utaratibu huo ukifanywa isipokuwa tunaona kwamba sheria imepita na kuwekwa saini na rais. Tuna ushahidi to support hizi claims ? sina hakika maadam walipitisha bungeni, kisha rais akaweka saini na hivyo kuwa sheria kuna cha ziada kilizokiukwa?.. Na maadam katiba inampa mamlaka makubwa sana rais kuchezea sheria na taratibu sijui kama kuna sheria itakayo pindua maamuzi ya rais ikiwa bunge lilikwisha pitisha..Mahakama ni sehemu tu ya utawala ule ule ulotunga sheria hizi..

Mkuu wangu NSSF na hizo PPF zina operate kama private pension plan wakifanya biashara na fedha ya watu na mlaliwa kweli vile. Kifupi serikali inafanya biashara badala ya MSSF kuwa private co, au basi ingekuwa mfuko unaotoa huduma ya uzeeeni na sio biashara..Badala ya Insurance companies kuwa wadhamini wa scheme hii unakuta serikali ndio wamiliki na wadhamini ikifa sisi ndio tutaingia ktk deni hilo.. Mawili NSSF ikienda chini tutalazimika Watanzania wote kulipia au wanachama wake kuzikwa maana utaenda ishitaki wapi serikali inapofanya biashara?..

Hizi vyombo vyote vya serikali vinavyofanya biashara wakati uongozi wake na board of directors ni watu waliochaguliwa wengine wabunge na mawaziri ni mchezo mchafu sana kwa Taifa..Ni rahisi ksuema mtaishitaki NSSF lakini wakati huo huo hamkujua kama ni mradi wa serikali ambayo ndio mnataka kuiweka kizimbani..
 
Hao HLRC na nyie wooote mtakaoenda mahamakamani ndio mtakuwa mmefunga rasmi huu mjadala.( au mmesahau msamiati wa cku hzi?). Hahaah, joking.

Ukweli ULIO WAZI ni kwamba, kwenye hii kesi lazima HLRC waangukie pua. Hivi mnajua hilo fao la withdrawal halipo katika sheria yoyote ya PPF au NSSF?. Mlizoeshwa kulambishwa sukari,mkaona raha kumbe mnafadhiliwa!

Mtazoea tu..na hakuna maandamano hapo..NANI kakuambia mtanzania anayekaa ofisini au aliyeko kwa kazi ya Boss anaandamanaga?. Mtapiga kelele nyuma ya keyboard na maofisini kwenu kisha UPEPO utapita.lol!

I support fully operaationalizaon of Pension system in tz, SSRA Wamechelewa sana.
section 44 ya PPF amendment act inatoa wewe
 
We should use Bunge platform before kimbilia mahakamani , a study lazima ifanyike na kujua nini kilifanyika kwenye Bunge la April 13 kama kifungu hicho kilikuwepo kwenye mswada ama kilichomekewa .......remember issue ya sheria ya gharama za uchaguzi na kifungu cha 10.

hivi kwa wabunge itakuwaje wale ambao hawana 55 + watasubiria mafao yao? why walipitisha ? we need to do something in between kabla ya Court ....

Thanks for your idea above. There must be a reason why such law might have been enacted by the PMs. Of course it is for the gvt's interest against the very tighten economy of poor individual Tanzanians. Shame to our PMs! No one will understand this...
 
Kituo cha kutetea haki za binadamu nchini Tanzania kimesema kinaandaa taratibu za kuiburuza serikali mahakamani kwani kumkatalia mwanachama kuchukua hela zake kwa vile hajafikisha miaka 60 ni ukiukwaji wa haki za binadamu.Hii ni kwa sababu hakuna makubaliano yaliyofanyika kati ya mifuko husika na wanachama ili kuleta sheria hii ambayo ni mbaya na haramu hasa kwa wafanyakazi wa sekta binafsi.
HLRC imeomba ushirikano wa wafanyakazi wote kufanikisha azma hii.

Source:Habari BBC Jioni.

My take:
Sheria hii ya NSSF ni kitanzi kwa wafanyakazi kote nchini hasa wa sekta binafsi kutokana na ukweli kwamba makampuni mengi binafsi yamekuwa yakiwaachisha mara kwa mara wafanyakazi wake huku kukiwa hakuna utetezi wowote wa serikali.Ni vigumu sana wafanyakazi kuunga mkono sheria hii kutokana na ukweli kwamba mtu akiacha kazi akiwa na miaka 30 itampasa kusubiri miaka 25 ili apate mafao yake.Huo ni uendawazimu.

Mi siwaelewi hawa HLRC, mbona wametajwa kuwa nao ni wamojawapo waliochangia sheria hii? "Kikao hiki pia
kiliwashirikisha wadau mbalimbali miongoni mwao wakiwemo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Chama cha
Waajiri Tanzania (ATE), Chuo Kikuu Mzumbe, Tanzania Higher Learning Institution Trade Union (THTU), Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF), Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Mfuko wa Pensheni kwa Mashirika ya Umma (PPF), Mfuko wa Akiba kwa Watumishi wa Serikali (GEPF), Mfuko wa Hifadhi za Jamii (NSSF) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)."
 
Nadhani hawa jamaa wa SSRA hawakufikiria vya kutosha na vile vile hawakushirikisha wadau ambao ni wachangiaji badala yake wameshirikisha serikali ambao ni wakopaji tu. Mathalani mimi nasimamia ujenzi wa bara bara ya lami Singida to Babati. Hii project ina miaka mitatu kwa sasa na kunavibarua wazoefu wanalipiwa nssf....mwishoni wa mwaka huu barabara itakabidhiwa na ajira ya vijana hawa itafikia ukingoni...je hawa nao wasubiri mpaka watimize miaka 55? nina inawezekana kabisa wasipate ajira nyingine kwani hawana shule iliyojitosheleza ila tumewachukuwa kwa sababu ni waaminifu ningependa mama IRENE ISAKA anieleze mwanachama kama huyu ambaye hajachanga michango jumla ya miezi 180 ili aweze kupata pensheni na ana umri wa miaka 30 atasubiri kwa miaka mingine 25? na je atapewa pesa yake tu au atakuwa kwenye pensheni?
 
Kituo cha kutetea haki za binadamu nchini Tanzania kimesema kinaandaa taratibu za kuiburuza serikali mahakamani kwani kumkatalia mwanachama kuchukua hela zake kwa vile hajafikisha miaka 60 ni ukiukwaji wa haki za binadamu.Hii ni kwa sababu hakuna makubaliano yaliyofanyika kati ya mifuko husika na wanachama ili kuleta sheria hii ambayo ni mbaya na haramu hasa kwa wafanyakazi wa sekta binafsi.
HLRC imeomba ushirikano wa wafanyakazi wote kufanikisha azma hii.

Source:Habari BBC Jioni.

My take:
Sheria hii ya NSSF ni kitanzi kwa wafanyakazi kote nchini hasa wa sekta binafsi kutokana na ukweli kwamba makampuni mengi binafsi yamekuwa yakiwaachisha mara kwa mara wafanyakazi wake huku kukiwa hakuna utetezi wowote wa serikali.Ni vigumu sana wafanyakazi kuunga mkono sheria hii kutokana na ukweli kwamba mtu akiacha kazi akiwa na miaka 30 itampasa kusubiri miaka 25 ili apate mafao yake.Huo ni uendawazimu.

Ninyi hamjui, hii ni janja ya serikali dhaifu kuwazuia madokta hasa wale wazee specialist wasiondoke nchini kwa kuhofia kupoteza mafao waliyokwisha yatumikia kwa muda mrefu. ....serikali imetambua kuwa ule usemi wa mheshimiwa rais wa asiyetaka kufanya kazi serikalini na mshahara mdogo atafute pa kufanya kazi umeamsha hasir miongoni mwa ma chief wa hospitali nyingi na vyuo vikuu vya hapa nchini na wengi wanakusanya nauli tayari kwa kuondoka kwenye ajira ya serikali
 
Sometimes hawa wazee huwa nawashangaa sana. Twaweza kuja ambiwa kwamba watumishi ndo walopendekeza sheria hii. Ukiangalia kwa undani, viongozi wetu maofisini ni wazee na hawaoni kuwa wanapoteza chochote juu ya hili. Kundi litakaloathirika kwa kiasi kikubwa ni vijana wa leo (wazee wa kesho!!). Nadhani sasa umefika wakati waathirika wa madhira yote ya serikali waonyeshe kwa uwazi kuwa hili hawakubaliani nalo. Kwa bahati nzuri hawa watetezi wa haki za binadamu ndo wameshalianzisha. Mimi nawambieni nchi hii imetafunwa vya kutosha na wazee wetu na sasa tuwaambie imetosha
 
Katika Vitu vitakavyo Idhoofisha na angusha Serikali hii.... This will be the Strongest one.... Its ridiculous.............!
 
(Hapo kwenye red hapo, ndipo ulipoHARIBU...we mama , we,we,we kaa kimya,.............Hakuna Mtanzania, haswa mfanyakazi yeyote nchi hii, utakayemweleza huo hayo madudu akakuelewa.
 
Back
Top Bottom