Muacici
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 208
- 11
Mara nyingi huwa jambo hili linanishangaza sikukuu za kidini hasa za kikristo utakuta ofis za serikal(wizara,shule even hospitals)kupamba maua na wakati mwengine na kwaya zinapigwa.Na hiyo inayoitwa television ya taifa(TBS1)inaadhimisha krismas wiki mbili kabla na baada na inabadili mfumo wa vipindi vyake na kuwa wa KIKRISMASKRISMAS!Sijasema Krismas isisherehekewe kitaifa lkn pawepo na usawa baina ya Dini zote.
Wazo lako Chungu-tamu sio baya, ila naomba uelewe kuwa hakuna sehemu yoyote kwenye sheria za nchi panasema wakristo waweke maua etc kwenye ofisi, kwahiyo usihusianishe sherehe hizo na serikali. Mambo haya yanafanywa na waumini walioko kwenye ofisi hizo, hivyo hata waislamu wangependa kufanya hivyo hakuna angewazuia. Ila kuiga mambo ya dini fulani nalo sio wazo zuri huenda waislamu hawana utamaduni huu, hivyo hawaoni haja ya kuiga wakristo na ndio maana viongozi wa kiislamu hata siku moja hawajalilalamikia hili. Nafikiri hasa maneno machache yatakusaidia kubadili mtazamo wako, maana wazo kama hili linaweza kuwa kubwa na likahatarisha hata usalama wa raia. Tuwe makini na posts zetu.