Hizi ni hoja zilizoibuka mara tu baada ya Kikwete kumaliza hotuba yake! Wewe una hoja gani?

No comment. Tuna tatizo la kufanya mambo kwa kwa kurupuka. Kikwete alikurupuka kuanzisha mchakato huu. Hakujiandaa
 
Serikali 2 zitaendeleza hisia za Utanganyika kwa kasi
Mkuu wa Nchi kamaliza kuhutubia Bunge la Katiba.
Kimsingi kaegemea upande wa msimamo wa Serikali 2
ambao ndio msimamo wa CCM chama anachoongoza.
Hata hivyo kasisitiza kuwa iwapo tunataka Serikali 3
basi tuzingatie hofu zilizopo ikiwemo masuala ya Uraia,
uwezo wa kifedha wa Serikali ya Muungano nk.
Ni dhahiri kero za Muungano zilizodumu kwa zaidi ya
miaka 50 haziwezi kutatuliwa na muundo ule ule
uliozitengeneza.
Jawabu l...a muungano wa Tanzania ni muundo wa
Serikali tatu wenye Serikali ya Muungano yenye nguvu
na rasilimali. Tunaloweza kuongeza ni kuweka mfumo
wa Tawala za Mikoa wenye kupanua demokrasia zaidi
kwa kuchagua wakuu wa mikoa na kufuta wakuu wa
wilaya.
Ni dhahiri Uraia itakuwa ni 'deal breaker' kwenye suala
la muundo wa Muungano. Hili litajibiwa kwa kuwa na
Nchi moja, dola moja na Serikali tatu hayo ni maoni ya Zitto.

Maoni yangu ni kwamba kwa nini muundo wa serikali 3 ambao haujawahi tumika hapa nchini Kikwete atishe watu kwa mambo mengi kiasi kile? Mi nadhani kila mfumo unajengwa kwa kulindwa na Sheria zilizopo ndani ya katiba.
Zanzibar ilipojitangaza kuwa nchi hii ilivunja katiba ila JK akakaa kimya sasa huu muundo wa serikali 2 hautadumu.
Tuwe makini tusijehitaji katiba yakweli ndani ya miaka mitano ijayo.
 
Nakubaliana na JK! Watu wanataka Katiba iwaletee maisha bora ndio maana wengi hawakuzungumzia juu ya Muungano! Washabiki wakuu wa Muungano wa Serikali 3 ni wale walafi tu wa madaraka, hawana lolote!
 
Baada ya kusikiliza hotuba ya J.K nimegundua kwamba hakukuwa na nia ya dhati ya kuandika katiba mpya bali CCM walikuwa wanapima uelewa wa wananchi kuhusu kero za muungano.

Sidhani kama kulikuwa na nia dhabiti ya kupata feedback ya kweli ya kile wanachokitaka watanzania going forward.

Hakukuwa na sababu ya kupoteza muda na pesa kwa misimamo ambayo Rais na CCM walishajua wanachokitaka

Nimesikitishwa sana na udhaifu mkuu wa kiuongozi.Na upotevu wa pesa za kodi kwa decisions ambazo mkuu wa nchi kashaweka upfront.

Kama maoni ya tume hayafai why wasting the time and resources?

After all idea ya katiba mpya haikuwa ajenda ya CCM.

Tanzania nakusikitikia!

He made it clear kwamba mfanye hivyo yy akishatoka ofisini. Tanzania is a sad country with very sorry leaders
 
Ametupa kauli mbiu yenye kusema,Tanzania kwanza.Hotuba yake was the best I ever heard,na amesema wazi kabisaa kwamba jukumu ni la wabunge woote kuhakikisha waandika katika ya watanzania.mlitegemea azomewe,hajazomewa mmeanza kusimanga,hamna heri binadamu wa leo.khaa
 
Kikwete ni raisi wa hovyo na alipaswa kuzomea.

Kikwete anapewa heshima lakini hajieshimu.

Wapinzani na nyinyi mbadilike!Kwanini jana mlikaa na kumsikiliza mtu anaeongea kama mwenyekiti wa chama?!

Wapinzani mlipaswa ama kumzomea au kutoka nje ya bunge na si kuja kulalamika huku kwenye mitandao.

Wapinzani msiwe "soft" hii itakuwa katiba ya CCM.

Kikwete alistahili kuzomewa kwani hajieshimu na anatumia cheo chake kwa faifa ya CCM.

In short,Kikwete hakustahili kwenda kujadili rasimu ndani ya bunge.

Huyu ni raisi wa hovyo na mnafiki kupindukia asiostahili kuheshimiwa kama raisi.

Jiheshimu uheshimiwe na si vinginevyo.

nyinyi ndio wakwanza kuiponda chadema sasa mwambieni zitto wenu hawatatulie matatzo
 
Halafu kwanini siku zote watu wanaodai serikali tatu upande wa bara ndio walewale wanaodai na serikali za majimbo. Unaweza kuona kwa undani watu wa aina hii ni separatists of the nation at heart, yule mwanasheria mkuu wa kenya keshawaambia indirectly na najua alikuwa akilenga hapo kwenye majimbo si kila kitu lazima kuiga.

Vingine vipo hivyo kwa sababu ya hali halisi ya jamii zenyewe zilivyo pengine kutokana na miungano ya matiafa au kwenye ukabila uliokithiri lakini watu bado tu wamekazana na serikali za mikoa, kuendeleza mwenendo ule ule wa kujenga fikra za regional and reducing national loyalty.
 
Kwa masikitiko makubwa nikiungana na Watanzania kote nchini na duniani Rais wetu JK umetutia aibu sana hasa kwa hotuba yako iliyojaa maelekezo kwa wabunge wa bunge la katiba wafanye nini na nini wasifanye,lakini ni wazi mbinu zako watu wameshazijua vizuri kuwa huitakii mema Nchii hii hasa uliposema wanaotaka Serikali tatu wangoje kwanza uondoke madarakani.


Hapa kwahili jambo tunatakiwa sana tumshirikishe Mungu ili wale wote wenye nia ovu kama JK washindwe mapema na mchana kweupe tena waziwazi hasa anapotaka Zanzibar iwe nchi ndani ya nchi,yaani kama ilivyo Lesotho ndani ya Afrika Kusini.

Mungu huwa hashindwi jambo maana kamuumba JK nasisi pia .


YEREMIA 32;27
Tazama ,mimi ni Bwana ,Mungu wa wote mwili;je! Kuna neno gumu lolote nisiloliweza?
 
kinachoshangaza ni hapo anaposema wanaotaka serikali tatu idadi ni ndogo kuliko wanaotaka 2, kajuaje? au kamtumia prof maji marefu maana shek yahaya hayupo.

Mpango huo uliandaliwa mapema,sheria ilitungwa wabunge wote na wawakilishi wawe kwenye bunge idadi yao anaijua na msimamo wa ccm uko wazi ni serikali 2.Pia uteuzi wake miongoni mwa wajumbe 200 makada wa ccm kibao.
 
Leo nimeshuhudia majibu mepesi kwa maswali magumu mno...
Ikiwa matatizo ya muungano bado yapo hata wakati tunasherehekea miaka 50, je si wakati muafaka wa kujaribu serikali 3?

Haya mambo ya "kujaribu" kwenye suala la Katiba ni hatari sana!
 
Kwa masikitiko makubwa nikiungana na Watanzania kote nchini na duniani Rais wetu JK umetutia aibu sana hasa kwa hotuba yako iliyojaa maelekezo kwa wabunge wa bunge la katiba wafanye nini na nini wasifanye,lakini ni wazi mbinu zako watu wameshazijua vizuri kuwa huitakii mema Nchii hii hasa uliposema wanaotaka Serikali tatu wangoje kwanza uondoke madarakani.


Hapa kwahili jambo tunatakiwa sana tumshirikishe Mungu ili wale wote wenye nia ovu kama JK washindwe mapema na mchana kweupe tena waziwazi hasa anapotaka Zanzibar iwe nchi ndani ya nchi,yaani kama ilivyo Lesotho ndani ya Afrika Kusini.

Mungu huwa hashindwi jambo maana kamuumba JK nasisi pia .


YEREMIA 32;27
Tazama ,mimi ni Bwana ,Mungu wa wote mwili;je! Kuna neno gumu lolote nisiloliweza?

Afadhali usingenukuu bibilia!!! Mtu wa Mungu hawezi kuwa na mawazo ya kibaguzi kama yako hasa ukizingatia dunia hii site tunapita tu. After all tuseme Bunge linapitisha serikali 3 jifikirie bila jazba ni kitu gani kitaongezeka katika hali yako uliyonayo sasa hivi kimaendeleo n.k. kama we we ni mwanasiasa mwenye matarajio ya cheo fulani kwenye mfumo was serikali 3 fine lakini hat a hivyo matarajio hayo yanaweza kuwa ndoto ya mchana pia.
 
Katiba tayari CCM wanayo, naona sasa hivi wanafikiria juu ya caver waweke picha ipi kati ya ile inayowaonesha wakitolosha Tembo wetu au Wakificha Mabillion yetu kule Ughaibuni.

Mimi hata kura ya kukubali au kukataa sipigi tena.
Haina faida yoyote, kwasababu watatuambia pia kuwa waliopiga kura ni 20000,waliokubali Muundo wa serikaki 2 ni 10000 na waliokataa ni 10000, yaani asilimia Hamsini kwa Hamsini, Jinsi Vichwa vyao vinavyojua Hesabu.

Kuishi Nchi hii, chini ya Utawala wa Magamba bora Ukawe Shoga Uganda, uku ukiishi kwa kuhesabu siku zako zilizosalia ukiwa Uraiani.
 
Fara wewe,maoni ya setikali tatu yametoka kwa wananchi,si hao waroho wa madaraka,na si lazima kuwe na maraisi watatu,rais mmoja tu wa muungano hakafu tanganyika na zanzibar wawawikilishwe na mawaziri wakuu
 
Mpango huo uliandaliwa mapema,sheria ilitungwa wabunge wote na wawakilishi wawe kwenye bunge idadi yao anaijua na msimamo wa ccm uko wazi ni serikali 2.Pia uteuzi wake miongoni mwa wajumbe 200 makada wa ccm kibao.

Ndio maana Lissu alisha sema yote hayo hayakufanyika bahati mbaya ndio maana sheria ya mabadiliko ya katiba iliruhusu bunge la katiba liwe na wabunge wote na wawakilishi ambao kimsingi aliapa kuitete katiba wanayoivunja bunge sheria ile ilinyima uwakilishi wa wananchi wengi bungeni pengine wengi zaidi ya wabunge hata 900 kwa uwiano wa idadi ya Watanzania milioni 44 mkuu haya yote yalishapangwa hakuna katiba mpya hapo kwa Masirahi ya CCM kuendelea kubaki madalakani milele amina.
 
Back
Top Bottom