Hivi Wazungu wana makabila?

Hivi Wazungu wana makabila?

Sema zamani inawezekana zamani na wenyewe walikuwa na makabila ila kwa sasa hamna kama huku Tanzania kiswahili kinavyoharibu au kuhua lugha za asili,,,, watu wengi kwa sasa kwa mfano Tanzania wanazaliwa hawajui lugha zao za asili
 
Kuna jamaa alinambia hicho kitu hakuna. Ukabila ulishapotea miaka mingi kutokana na muingiliano wa watu kutoka jamii tofauti. Ila kuna nyumba za kuhidhi mambo ya kale(museum), ndio wamehidhi tamaduni za makabila yote huko na historia zao.

Source. Mwana tu, so unaweza kunikosoa.
Nadhani uko sahihi. Nimejaribu kusoma hii link. Ni kama ulivyoongea.
whatever happened to european tribes?
 
Yalikuwepo ila kwa sababu ya muingiliano sana wanaonekana kitu kimoja, mfano Tanzania watoto wanaozaliwa wanakielewa zaidi Kiswahili kuliko lugha za asili, baba msukuma kamwoa mchaga sasa hapo mtoto ataishia kuzungumza Kiswahili, sasa wenzetu hizo muingiliano ina miaka hata maelfu
 
Labda kwa zamani ila wenzetu wameacha tamaduni ya majina ya ukoo africa ukimwambia mtu full name yako bila mwakifamba shayo bado ujamaliza kuna kipindi cv kuna mpk kabila mzungu izo waliweza mapema tuitane na vyetu vyetu viwe na majina peter frank basi lkn utasikia mtu ajalizika we peter frank wa wap
 
Lakini hizo ni kama nchi tofauti tofauti zikaungana ndio maana inaitwa UK "United Kingdom" fikiria kama Tz kila mkoa unakuta kuna makabila ambayo ni wenyeji wa hiyo mikoa mfano: mbeya kuna wanyakyusa na wasafwa, Kilimanjaro kuna wapare na wachagga etc

Ubeligiji kuna flemish and walloon. Hii ni kulingana na lugha wanayo ongea. Flemish - dutch speeking and walloon - french speeking.
 
Ukiwa London utasikia accent yao ni tofauti na mtu wa York. Mtu wa Liverpool akiongea tofauti na mtu wa Birmingham. Kuna accent nyingine kama za New Castle unaweza ukatoka kapa.
Kama makabila yao unayajua tunaomba uyataje sio kutupa maelenzo ya rafudhi zao kwamfano hapa tanzania tuna wakara wako kisiwa cha ukerewe wanyambo wako karangwe wapare Wapo Kilimanjaro nk
 
Wazungu walishafuta hayo mnayoyaita Makabila, ni lazima uelewe Kabila ni neno la dharau na maana yake ni mtu ambaye hajatastaarabika bado, yaani hajaweza kujenga Taifa, na ndiyo maana neno Kabila hutumika Afrika Kusini kwa Sahara, native Americans, aborigines hao ndiyo Wazungu hutumia neno Kabila lkn wengine wote walishafuta!
Isitoshe Tanzania haina Makabila 120 kama mnavyoanini na hayo yote unayoyaita Makabila Tanzania yalianzishwa na Wazungu/ Waarabu kabla ya Wageni kuja kwa mfano kulikuwa hakuna Wanyamwezi, Wahaya, Wagogo, Wachaga n.k. kama tuwajuavyo leo hii!

Hivyo neno Kabila ni neno la dharau kwa Mwafrika kama vile nigger tu!
mmmh!!!! "Mungu ibariki Tanzania na watu wake"
 
Neno "tribes" ni la kiingereza..... Wazungu wa London ni tofauti na WA Wales japo wote wanajiita waingereza. kuna wezi "thieves".....kuna wanga "wizards"...wanabaguana huko katalunya, wanapigana risasi hovyo huko USA majuzi mtu mzima Steve kaua makumi ya raia bila sababu
hahahaha!!!!!!!! hi ni Tanzania.
 
Makabila wanayo ila wao walijitaidi kwa watu wa jamii moja kuunda taifa mfano taifa mfano uholanzi, sweden na ureno japo kuna mataifa mengine yenyewe yaliundwa kwa ndoa za watoto wa kifalme na kuwa na taifa moja kama spain ilivyo ni muunganiko wa wajamii( kabila) ya kubwa wa spain , basque, catalonia, na kila sehemu wana lugha yao na tamaduni zao japo lugha kuu ni ki spanish vivyo hivyo kwa switzerland muunganiko wa jamii za kifaransa , kiitalia, kigerman , ki roman ambao n sawa na makabila tu kwa kwao kwaio kila canton (state)(mkoa) wana lugha yao na tamaduni zao.
 
Hawana Makabila, ukiangalia nchi zao zimeundwa kutokana na ufalme wa eneo husika.

Mfano Belgium, France, UK, Holland, Spain n.k pia ukiangalia nchi zao nyingi ni ndogo kuliko mikoa ya Tanzania. Mfano San Marino in Km2 61, Lienchtenstein ina km2 160, Malta ila Km2 316. Dodoma pekee in km2 2,576.

Ina maana kama wazungu wasingeigawa kwa namna walivyoigawa, Mikoa mingi Tanzania ingekuwa nchi.
 
  • Thanks
Reactions: JMF
Hakuna nchi ambayo haina au haikua na makabila.tatizo ni kwamba wenzetu historia yao inaanza karne nyingi zlizopita wakat uku kwetu ni juzi tu miaka ya karibuni.Na ata sisi miaka 500 ijayo aya makabila ya leo yatakua yamefutika yote kitakachobaki ni lugha ya kiswaili kama lugha rasmi na wakati huo inawezekana hii mikoa ikawa ni mikoa yenye serikali zinazojitegemea na kutengeneza nchi moja yenye majimbo kamili yanayounganishwa na lugha 1 ya kiswaili.aya makabila mengi unayoyaona leo tanzania ni watu waliotoka uko nchi zingine wakaamia hapa wakatengeneza lugha na wengine walikuja na baadhi ya maneno na wakazaana wao kwa wao had kabila likakomaa kwenye eneo walikofikia lakin kwasababu sasa kuna mwingiliano mkubwa na makabila mengine nakukua kwa lugha ya kiswail ni hakika uko badae nasisi huu msamiati wa makabila utakua haupo.
 
  • Thanks
Reactions: JMF
Mimi ni mkatoliki ninayeijuwa vizuri system ya kanisa,

Kwanza kwenye mfumo wa kanisa katoliki maelezo uliyoyatowa hapo utachekwa huwezi kwenda kuinjilisha huko

Kwanza ulipata upadrisho lini? Na uko chini ya jimbo gani? Na je unahudumu shirika gani?
Huyu jamaa anayejiita padri ni mpumbavu kupindukia yaan anaweza kuwa mpumbavu namba moja humu JF
 
Back
Top Bottom