Mnabuduhe
JF-Expert Member
- May 8, 2015
- 352
- 594
Mwenye uelewa kutoka history anieleweshe kama wazungu wana makabila kama Tanzania tulivyo na makabila 120 or so! Na kama siyo, kwa nini hii imetokea Africa na siyo Ulaya/ Marekani/ Asia???
Hakuna Taifa lisilo na Makabila! Isipokuwa Makabila hupotea kwa Kuoleana na Kujichanganya na makabila mengine!
Kuwa na Makabila ishara ya Ukale na ushahidi kuwa bado jamii hizo hazijajichanganya na jumuia ya watu wengine na kuathiriwa au kupoteza uasili wao.
Ndio maana unakuta kuna matangazo au habri tunasikia kuna makabila yapo hatarini kupotea kwa sababu kama hizo hapo juu.
Amerika ya Kaskazini kuna Jamii ya watu mpaka leo ina makabila yao(Natives America) Comache,Navajo ambao mpaka leo wanalinda koo zao na Mila zao wakitawala kwa mila na desturi zao.
Ulaya pia waliwahi kuwa na makabila hasa karne za nyuma kidogo hasa wakati wa Utawala wa dora ya Kirumi - Belgae,Cantiaci,Catuvellauni,Dobunni,Dumnonii,durotriges,Regnenses,Textoverdi na n.k.
Chanzo:- Mitandaoni.
