Umeona kijana mzuuuuri upo nae kituoni. Kijana yupo next to you kakulia bati mbaya nawe kamoyo kanataka muongee huwezi jua bwana. Basi mtoto wa kike unajitosa kwa sauti ya huba na jicho legevu... samahani anko una saa hapo? Saa ngapi? Of course kidume kitajibu. Kisha unamwachia asante ikifuatiwa na tabasabu mwanana.... baada ya hapo unajisemesha yaani usafiri wa shida leo... ntachelewaaa! Baada ya hapo kwa walio wengi kuna maongezi, lol na siti moja mnaweza kukaa na nauli waweza kulipiwa! Kama unaona halipi unaachana nae ukishuka una add number to rejected list...! Umetongoza, hujatongoza?!