Hivi vyama vya ushirika huwa wanalipa mshahara kiasi gani?

Hivi vyama vya ushirika huwa wanalipa mshahara kiasi gani?

Isenye

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2024
Posts
486
Reaction score
2,069
Kuna chama kimoja cha ushirika mkoani mbeya nilifanya nao interview ya nafasi ya uhasibu.sasa katika interview waliniuliza mshahara ambao ningependa kulipwa,mimi nikawaambia uwe kati ya 1.7m-2.2m.
Jana wamenipigia kuniambia kuwa nimepata ile nafasi na natakiwa kuanza kazi mara moja,nikamwambia huyo mwenyekiti wa bodi aliyenipigia nitaanzaje kazi wakti sijaona terms za mkataba na mshahara mnaotaka kunipa,eti yeye akasema mshahara ni mzuri tu nisiwe na wasiwasi,hii imenitia wasiwasi kidogo.
So naomba kuwauliza wajuvi hawa watu wa vyama vya ushirika huwa wanalipa mshahara kiasi gani kwa watu wenye bachelor degree?
 
Huko ni njaa kali sana
Wanalipa kwa kutumia scales za halmashauri,tegemea kulipwa tgs D.
Halafu hivyo vyama vina migogoro isiyoishaga,tegemea pia kufungwa maana upigaji ni mkubwa mno
 
Ngoja waje mkuu.
Sema vyama vya ushirika ni vichache sana hivyo kuwapata wanaofahamu huwa sio wengi. Subiri waajiri watafika na kupiga kambi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom