shizukan
JF-Expert Member
- Jan 16, 2011
- 1,158
- 563
Moja kati ya tabia zetu (Watanzania) zinazonishangaza ni namna yetu ya kusalimiana. (Na pengine salamu zenyewe)
Mfn:
A na B wameongozana pamoja, wanamkuta C kakaa nje ya nyumba yake. A anamsalimia C : Habari za saa hizi? Anajibiwa: Nzuri wkt huo huo B anamsalimia C : Habari za leo? Naye anajibiwa : Nzuri.
Kinachonishangaza: Kulikuwa na umuhimu gani kwa B kuuliza swali ambalo A ameshauliza? Nia ya B ni kutaka kujua hali ya C au anakamilisha tu mazoea?
Turudi kwenye salamu zetu: SHIKAMOO
Katika kulifuatilia hili neno kwa waliokistudy kiswahili kama fani majibu yao kwangu yalikuwa: shikamoo = nipo chini ya miguu yako. Matumizi ya neno shikamoo yalianzia ktk zama zile ambazo Waarabu walikalia maeneo ya Pwani ya A.Mashariki. Na cha kushangaza ni kwamba hawakuambiana shikamoo wao kwa wao(kwa umri) , bali wa hadhi ya chini ndio alimwambia shikamoo aliyemzidi hadhi.
Rudi ktk jamii yetu ya sasa: Shikamoo imekuwa muhimu kuliko maudhui ya salamu. Ni imani yangu kuwa lengo la kusalimiana ni kujuliana hali. Lkn cha kushangaza, ukimsalimia mzee namna hii: U hali gani mzee? utaonekana una dharau na huna adabu.Tunafarijika sana kuambiwa shikamoo bila kupata nafasi ya kuwaeleza walio mbele yetu juu ya hali zetu.
Kingine na cha mwisho (kwangu, naamini wengine mtakuwa na mengi) ni haya mazoea ya kuitikia: NZURI!
Haya mazoea nayo yananiacha hoi. Unakwenda kwa mtu na umuulizapo hali yake atakwambia nzuri. Mbele huko katika mazungumzo si ajabu akakwambia, "usinione naongea hapa, nina homa kali ndugu yangu...na jana usiku kucha nimekohoa kama mbwa aliyemeza mjusi". Sasa hebu jiulize, ile 'nzuri' ilimaanisha nini? Je, msingepata wasaa wa kuendelea na stori ungeyajua yote haya ya mtu kukohoa kama mbwa aliyepaliwa na mate akibweka umbea (R.I.P Mr.Ebbo)?
Twende kazi wana JF...
Mfn:
A na B wameongozana pamoja, wanamkuta C kakaa nje ya nyumba yake. A anamsalimia C : Habari za saa hizi? Anajibiwa: Nzuri wkt huo huo B anamsalimia C : Habari za leo? Naye anajibiwa : Nzuri.
Kinachonishangaza: Kulikuwa na umuhimu gani kwa B kuuliza swali ambalo A ameshauliza? Nia ya B ni kutaka kujua hali ya C au anakamilisha tu mazoea?
Turudi kwenye salamu zetu: SHIKAMOO
Katika kulifuatilia hili neno kwa waliokistudy kiswahili kama fani majibu yao kwangu yalikuwa: shikamoo = nipo chini ya miguu yako. Matumizi ya neno shikamoo yalianzia ktk zama zile ambazo Waarabu walikalia maeneo ya Pwani ya A.Mashariki. Na cha kushangaza ni kwamba hawakuambiana shikamoo wao kwa wao(kwa umri) , bali wa hadhi ya chini ndio alimwambia shikamoo aliyemzidi hadhi.
Rudi ktk jamii yetu ya sasa: Shikamoo imekuwa muhimu kuliko maudhui ya salamu. Ni imani yangu kuwa lengo la kusalimiana ni kujuliana hali. Lkn cha kushangaza, ukimsalimia mzee namna hii: U hali gani mzee? utaonekana una dharau na huna adabu.Tunafarijika sana kuambiwa shikamoo bila kupata nafasi ya kuwaeleza walio mbele yetu juu ya hali zetu.
Kingine na cha mwisho (kwangu, naamini wengine mtakuwa na mengi) ni haya mazoea ya kuitikia: NZURI!
Haya mazoea nayo yananiacha hoi. Unakwenda kwa mtu na umuulizapo hali yake atakwambia nzuri. Mbele huko katika mazungumzo si ajabu akakwambia, "usinione naongea hapa, nina homa kali ndugu yangu...na jana usiku kucha nimekohoa kama mbwa aliyemeza mjusi". Sasa hebu jiulize, ile 'nzuri' ilimaanisha nini? Je, msingepata wasaa wa kuendelea na stori ungeyajua yote haya ya mtu kukohoa kama mbwa aliyepaliwa na mate akibweka umbea (R.I.P Mr.Ebbo)?
Twende kazi wana JF...