Opuk Jater
Senior Member
- Dec 25, 2018
- 145
- 130
Habari Wanandugu,
Katika kitu ambacho huwa kinanishangaza katika nyakati hizi ni maandishi na matamshi ya baadhi ya herufi na silabi. Huwa najiuliza kuwa Watanzania tunakwama wapi kwenye herufi "R" na "L" kuanzia kuyaandika mpaka kutamka?
Miaka ya nyuma kulikuwa na kichaka cha kujificha kuwa kuna Makabila ambayo hayana herufi "R" kwenye lugha zao za nyumbani, hasa mikoa ya kusini (Lindi & Mtwara).
Lakini siku hizi siyo kushindwa kutamka bali yanabadilishwa kabisa. Utakuta mtu na elimu yake anakuandikia "RAKINI" badala ya "LAKINI", Eti " KALILI" badala "KARIRI", kuna muda unamsikiliza mtu mpaka unashindwa kumwelewa kama anaongea kiswahili au anatumia lugha nyingine.
Tena kuna hawa Wachungaji na Manabii ukiwaskia wakiongea ndiyo wanazikazia " L" badala ya "R". Halafu hapo bado haujahamia kwenye vyombo vya habari.
Sasa cha ajabu siwani wakiwa wanabadili matumizi ya R na L wakiwa wanazungumza Kiingereza. Kwa hiyo huu ugonjwa ni ulimbukeni uliotujaa au ni wa makusudi?
MAONI KUTOKA KWA WADAU
Katika kitu ambacho huwa kinanishangaza katika nyakati hizi ni maandishi na matamshi ya baadhi ya herufi na silabi. Huwa najiuliza kuwa Watanzania tunakwama wapi kwenye herufi "R" na "L" kuanzia kuyaandika mpaka kutamka?
Miaka ya nyuma kulikuwa na kichaka cha kujificha kuwa kuna Makabila ambayo hayana herufi "R" kwenye lugha zao za nyumbani, hasa mikoa ya kusini (Lindi & Mtwara).
Lakini siku hizi siyo kushindwa kutamka bali yanabadilishwa kabisa. Utakuta mtu na elimu yake anakuandikia "RAKINI" badala ya "LAKINI", Eti " KALILI" badala "KARIRI", kuna muda unamsikiliza mtu mpaka unashindwa kumwelewa kama anaongea kiswahili au anatumia lugha nyingine.
Tena kuna hawa Wachungaji na Manabii ukiwaskia wakiongea ndiyo wanazikazia " L" badala ya "R". Halafu hapo bado haujahamia kwenye vyombo vya habari.
Sasa cha ajabu siwani wakiwa wanabadili matumizi ya R na L wakiwa wanazungumza Kiingereza. Kwa hiyo huu ugonjwa ni ulimbukeni uliotujaa au ni wa makusudi?
MAONI KUTOKA KWA WADAU
------------Hizo ni athari za lugha ya nyumbani na sio rahisi kubadilisha kama unavyofikiri.Lugha yoyote inayokuja kwako kama lugha ya pili lazima itaathiriwa na lugha ya kwanza.Nailo ni swala la ulimi sio akili.Hata wazungu kwenye nchi wanazozungumza kingereza wanatofautiana lafudhi kati ya nchi na nchi wakati lugha ni ile ile.kwaiyo hiyo ni kawaida sana kwenye jamii yetu na kamwe hatuwezi kufanana ulimi.
nuruyamnyonge, Haya si makosa ya kisarufi, useme kwa mfano, kusema anakujaga ni makosa, Kiswahili sahihi ni kusema anakuja.
Haya ni makosa ya kuchanganya herufi.
Kwa mfano, Magufuli mtu atamke "Magufuri" au "Mzee wa Kiraracha" mtu atamke "Mzee wa Kilalacha".
Hivyo basi, utaona ni vigumu kuweka kanuni katika makosa ambayo kimsingi si ya kisarufi (grammatical), bali ni ya kimatamshi (phonetical).