Hivi ni kweli Wizara ya Ardhi imeshindwa kutatua kero za wapangaji nchini?

Liky

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
428
251
Zaidi ya asilimia 80 ya wananchi hasa mijini wanaishi nyumba za kupanga. Kwa mji kama DSM ambapo bado kuna uhitaji mkubwa wa makazi bora, watu hutumia zaidi ya robo ya vipato vyao kulipia kodi za nyumba kila mwezi, lakini cha kushangaza, serikali haioni unyeti wa kuingilia na kusimammia sehemu hii. Hapa nina hakika serikali ingeweza kukusanya kodi ya kutosha kabisa kutoka kwa wenye nyumba iwapo wangeweka utaratibu mzuri wa usimamizi.

Tunaelekea kumaliza miaka 5 ya awamu ya kwanza ya JPM, lakini waziri Lukuvi na wizara yake wamekuwa wakiimba tu mapambio juu ya kanuni za upangishaji nyumba. Ugumu uko wapi kuleta sheria na kanuni zake ili kuwaondolea kero wananchi wanaopanga nyumba? Watu wanalazimishwa kulipa kodi mpaka ya mwaka mzima kisa tu hakuna kanuni husika.

Tutengeneze sheria, kama mtu akiamua kupangisha nyumba yake basi akubali kufuata kanuni za serikali, moja wapo ni kutolazimisha mtu kulipa kodi ya miezi 6/mwaka.

Kuna issue ya madalali wa nyumba, ambao kwanza wengi wao huku uswahilini hawajasajiliwa, maana yake wanafanya kazi bila utaratibu maalum. Matokeo yake wamejitengenezea utaratibu usio haki wala halali wa kudai kodi ya mwezi mmoja kama mtu ataamua kupanga nyumba husika. Wizara ya Ardhi kama wangekuwa wanatimiza wajibu wao, leo hii tungekuwa na muongozo wa kuwasajili na kutengeneza viwango vya malipo halali kwao pamoja na kukusanya kodi kutoka kwenye vipato vyao.

Haiwezekani mtu apewe kodi ya mwezi mmoja ambayo hata haikatwi kodi mahali popote na serikali kisa tu alisimama katikati ya mwenye nyumba na mpangaji.

Waziri Lukuvi, hizi ni petty issues kwako, ambazo ukiamua tu ndani ya muda mchache solution inapatikana na impact inakuwa kubwa.
 
Liky,

Umeandika na kukumbusha jambo la maana sana. Sekta ya upangishaji na ulipaji wa kodi za nyumba Tanzania inaendeshwa kwa ubabaishaji sana na wapangaji ni waathirika wakubwa. Inatakiwa kuwe na mwongozo.
Mi huwa nashangaa, kuna tatizo gani katika kufikiri kwa watu tuliowapa hizi nyadhifa? Yani kuna mapato yanapotea wazi wazi na hakuna mtu anashtuka
 
Ifikie mahala sasa hii biashara isifanywe tu kiholela na kila mtu, kuwe na standard maalum ya nyumba za kupangishwa na pia kuwe na controlling..

NHC iwe na kitengo maalum cha kufuatilia standard za nyumba za biashara na viwango vya gharama za upangishaji kila mahala..Kusiwe tena na madalali bali kuwe na madalali waliosajili na lazima wawe na website itakayoweka picha za nyumba zote baada ya ukaguzi wa NHC ionyeshwe ina nini na nini kwa maana ya kiwango chake na bei yake..

Serikali ipige marufuku raia kujenga majumba baadala yake kazi hiyo ifanywe na Estate agencies kwenye maeneo elekezi na wananchi wakopeshwe nyumba na waruhusiwe kuishi huku wanalipa with reasonable price, hii itaondoa ujenzi holela na usiofuata taratibu na pia miji yetu itakuwa imepangiliwa na nyumba standard na mitaa itakuwa ya kisasa..
 
Mkuu waangalie pia na upande hotel, lodge na hivi vigesti bubu, haiwezekani kahotel flani kako pale karibu na road interchange kachumba kadogo, ac fake, tv chenga, simu ni PBX wanatoza elfu 40??


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ifikie mahala sasa hii biashara isifanywe tu kiholela na kila mtu, kuwe na standard maalum ya nyumba za kupangishwa na pia kuwe na controlling..

NHC iwe na kitengo maalum cha kufuatilia standard za nyumba za biashara na viwango vya gharama za upangishaji kila mahala..Kusiwe tena na madalali bali kuwe na madalali waliosajili na lazima wawe na website itakayoweka picha za nyumba zote baada ya ukaguzi wa NHC ionyeshwe ina nini na nini kwa maana ya kiwango chake na bei yake..

Serikali ipige marufuku raia kujenga majumba baadala yake kazi hiyo ifanywe na Estate agencies kwenye maeneo elekezi na wananchi wakopeshwe nyumba na waruhusiwe kuishi huku wanalipa with reasonable price, hii itaondoa ujenzi holela na usiofuata taratibu na pia miji yetu itakuwa imepangiliwa na nyumba standard na mitaa itakuwa ya kisasa..
Nakubaliana nawe, japo hapo kupiga marufuku watu kupangisha nyumba kidogo naona itakuwa harsh. Watu waruhusiwe kufanya hiyo biashara ila tu wafuate utaratibu utakaowekwa. Hilo la kupanga viwango vya kodi kulingana na standard ni la msingi sana. Unakuta nyumba ya zamani kabisa, Chumba, sebule, jiko na choo eti inapangishwa 350,000 Tshs kwa mwezi, kisa ipo Sinza, K.nyama au Kinondoni.
 
Mkuu waangalie pia na upande hotel, lodge na hivi vigesti bubu, haiwezekani kahotel flani kako pale karibu na road interchange kachumba kadogo, ac fake, tv chenga, simu ni PBX wanatoza elfu 40??


Sent from my iPhone using JamiiForums
Hasa Dom haya mambo yapo sana unakuta kagesti kaovyo tuu lakini bei 30 k,ambako kwa Dar standard hiyo ni10k, ukitafuta ya 10k Dom ni kichekesho sakafu inamashimo,Milango haifungi vzr,vitanda vya ovyo mashuka hayafuliwi hata wiki yaani kinachonikera zaidi kukuta vyumba vya kulala havina socket za kuchajia simu ila vina umeme
Pakuchajia mpk receiption tuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli hii kitu ni shida sana, pamoja na kwamba sipo upande huo ila naona madhira wanyopata wapangaji.

Wanakuja soon wapangishaji na madalali kukomenti, utasikia...


a. Nyumba ni yangu tusipangiane, kwani mlinisaidia kujenga.
b. Au tusiingiliane mjenge zenu.
 
Kweli hii kitu ni shida sana, pamoja na kwamba sipo upande huo ila naona madhira wanyopata wapangaji.

Wanakuja soon wapangishaji na madalali kukomenti, utasikia...


a. Nyumba ni yangu tusipangiane, kwani mlinisaidia kujenga.
b. Au tusiingiliane mjenge zenu.
Hahaha! Mi mwenyewe kiukweli nina kibanda changu Mwanza huko napangisha, lakini siwataki hata kusikia madalali. Halafu unatizama na utu kama mtu anakupa kodi ya miezi3 mi bado naona ni reasonable kabisa
 
Mi huwa nashangaa, kuna tatizo gani katika kufikiri kwa watu tuliowapa hizi nyadhifa? Yani kuna mapato yanapotea wazi wazi na hakuna mtu anashtuka
Mda huo wamekomaa kurasimisha makazi holela kwalengo la kupata kodi ya mwananchi maskini wakati kodi zipo nyingi tu! 1.Ukinunua LUKU wanakata kodi why nyumba ya kupanga
2. Ukiweka mafuta kwenye vyombo vya moto wanakata kodi why nyumba ya kupanga.
3.Vocha nk kodi!
Waziri na naibu wake wamebakiza kazi ya kusuruhisha migogoro tu mwingine kupekua mafairi it is fine! Ila nadhani mnawatendaji wengi wakuwapa majukum mengine.
Mnakosesha nchi mapato mengi sana nataka niwape mfano mdogo sana
Dar es salaam tusajiri kisheria vyumba vyakupanga acha nyumba na appatments wala magorofa ya kariakoo nk.
Vyumba vya uswahirini ni tsh.40,000/=× vyumba 50,000

Harafu watoze 10% tu yabei kwa maana ya tsh.4000 tu kwa chumba
Maana yke ni 4000×50,000=200milions × mwaka kwa maana ya 200mln ×12=2Bilion 400milions

Kumbuka hivi ni vyumba single na kwa bei hyo nani dar pekee nahii bei ya 40 elf nikaribu kila mkoa
Kifupi tunapoteza karibu ya tsh.3 hadi hadi nne. Kwa mwaka kupitia wizara hii badara ya kumuacha mh Rais kutengeneza vitambulisho naomba wamsaidie km wanahitaji mawazo na mbinu waseme tuwasaidie.
Wachumi wa wizara hii watuambie wanamsaidiaje waziri na nchi kwa ujumla.
 
Mimi wananifanya niamini ya yule jamaa kiboko ya kange Lugora mr Msiba kwamba ndani ya serikari kunawatu wengi wanamhujum Rais

Wachache sana wanamuunga mkono, kundi kubwa la mawaziri niwaongeaji tu ila inpact hakuna.
 
Zaidi ya asilimia 80 ya wananchi hasa mijini wanaishi nyumba za kupanga. Kwa mji kama DSM ambapo bado kuna uhitaji mkubwa wa makazi bora, watu hutumia zaidi ya robo ya vipato vyao kulipia kodi za nyumba kila mwezi, lakini cha kushangaza, serikali haioni unyeti wa kuingilia na kusimammia sehemu hii. Hapa nina hakika serikali ingeweza kukusanya kodi ya kutosha kabisa kutoka kwa wenye nyumba iwapo wangeweka utaratibu mzuri wa usimamizi.

Tunaelekea kumaliza miaka 5 ya awamu ya kwanza ya JPM, lakini waziri Lukuvi na wizara yake wamekuwa wakiimba tu mapambio juu ya kanuni za upangishaji nyumba. Ugumu uko wapi kuleta sheria na kanuni zake ili kuwaondolea kero wananchi wanaopanga nyumba? Watu wanalazimishwa kulipa kodi mpaka ya mwaka mzima kisa tu hakuna kanuni husika.

Tutengeneze sheria, kama mtu akiamua kupangisha nyumba yake basi akubali kufuata kanuni za serikali, moja wapo ni kutolazimisha mtu kulipa kodi ya miezi 6/mwaka.

Kuna issue ya madalali wa nyumba, ambao kwanza wengi wao huku uswahilini hawajasajiliwa, maana yake wanafanya kazi bila utaratibu maalum. Matokeo yake wamejitengenezea utaratibu usio haki wala halali wa kudai kodi ya mwezi mmoja kama mtu ataamua kupanga nyumba husika. Wizara ya Ardhi kama wangekuwa wanatimiza wajibu wao, leo hii tungekuwa na muongozo wa kuwasajili na kutengeneza viwango vya malipo halali kwao pamoja na kukusanya kodi kutoka kwenye vipato vyao.

Haiwezekani mtu apewe kodi ya mwezi mmoja ambayo hata haikatwi kodi mahali popote na serikali kisa tu alisimama katikati ya mwenye nyumba na mpangaji.

Waziri Lukuvi, hizi ni petty issues kwako, ambazo ukiamua tu ndani ya muda mchache solution inapatikana na impact inakuwa kubwa.
Usinikumbushe hilo la kumpa dalali hela ya mwezi mmoja, mpaka leo elfu 50 yangu inaniuma sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ifikie mahala sasa hii biashara isifanywe tu kiholela na kila mtu, kuwe na standard maalum ya nyumba za kupangishwa na pia kuwe na controlling..

NHC iwe na kitengo maalum cha kufuatilia standard za nyumba za biashara na viwango vya gharama za upangishaji kila mahala..Kusiwe tena na madalali bali kuwe na madalali waliosajili na lazima wawe na website itakayoweka picha za nyumba zote baada ya ukaguzi wa NHC ionyeshwe ina nini na nini kwa maana ya kiwango chake na bei yake..

Serikali ipige marufuku raia kujenga majumba baadala yake kazi hiyo ifanywe na Estate agencies kwenye maeneo elekezi na wananchi wakopeshwe nyumba na waruhusiwe kuishi huku wanalipa with reasonable price, hii itaondoa ujenzi holela na usiofuata taratibu na pia miji yetu itakuwa imepangiliwa na nyumba standard na mitaa itakuwa ya kisasa..
Hili balaa lianze mkoa wa mtwara, nyumba kupanga bei ghalii mnoooo ukilinganisha na ubora wa nyumba yenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom