Ombi Kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kufuatilia kwa ukaribu Baraza la ardhi Sumbawanga

aronstephy

JF-Expert Member
Jun 23, 2015
300
618
Mabaraza yaliyowekwa na hii wizara ili kutatua migogoro kwenye ardhi na sio migogoro ya kifamili kwa sehemu kubwa yamefanyika kuwa kero kwa wananchi haswa wenye uhalali wa umiliki wa ardhi kwa viongozi husika kuendekeza rushwa sanaa.(Sijui posho zao haziwatoshi)

Kumekuwa na ucheleweshaji wa hukumu na pia kumekuwa na ukiukwaji mkubwa sana wa sheria katika kutekeleza majukumu yao.Kuna kesi zimeshatolewa hukumu na mahakama za hakimu mkazi na hata mahakama ya rufaa lakini zinapopelekwa kwenye haya mabaraza kumekuwa na uzubaifu mkubwa wenye kutengeneza mianya mingi ya rushwa na hata kudhurumu mali za wananchi wanyonge walioshinda kwa uhalali kesi zao kwenye mahakama za mwanzo na hata za rufaa.

Nakuomba Mh Jerry Silaa peleka jopo la wataalam wako kwenye Baraza la ardhi mkoa wa Rukwa (kuanzia kata mpaka ya wilaya) wakawasaidie wananchi wanyonge wanaoibiwa haki zao na majizi yanatumia pesa na ushawishi walionao kwenye jamii kupoka maliza za wanyonge. Mwezi uliopita tu ulitoka kutoa maelekezo namna wanatakiwa kunya kazi ila bado wamekuwa kikwazo haswa. Kesi ya kusikilizwa mwezi mmoja inasikilizwa miezi mitatu na ukizingatia asaiv ni msimu wa kilimo.

Natanguliza Shukrani kwa Wizara husika nikijua hapa wapo wadau na wahusika watakao lifanyia kazi.
 
Mabaraza yaliyowekwa na hii wizara ili kutatua migogoro kwenye ardhi na sio migogoro ya kifamili kwa sehemu kubwa yamefanyika kuwa kero kwa wananchi haswa wenye uhalali wa umiliki wa ardhi kwa viongozi husika kuendekeza rushwa sanaa.(Sijui posho zao haziwatoshi)

Kumekuwa na ucheleweshaji wa hukumu na pia kumekuwa na ukiukwaji mkubwa sana wa sheria katika kutekeleza majukumu yao.Kuna kesi zimeshatolewa hukumu na mahakama za hakimu mkazi na hata mahakama ya rufaa lakini zinapopelekwa kwenye haya mabaraza kumekuwa na uzubaifu mkubwa wenye kutengeneza mianya mingi ya rushwa na hata kudhurumu mali za wananchi wanyonge walioshinda kwa uhalali kesi zao kwenye mahakama za mwanzo na hata za rufaa.

Nakuomba Mh Jerry Silaa peleka jopo la wataalam wako kwenye Baraza la ardhi mkoa wa Rukwa (kuanzia kata mpaka ya wilaya) wakawasaidie wananchi wanyonge wanaoibiwa haki zao na majizi yanatumia pesa na ushawishi walionao kwenye jamii kupoka maliza za wanyonge. Mwezi uliopita tu ulitoka kutoa maelekezo namna wanatakiwa kunya kazi ila bado wamekuwa kikwazo haswa. Kesi ya kusikilizwa mwezi mmoja inasikilizwa miezi mitatu na ukizingatia asaiv ni msimu wa kilimo.

Natanguliza Shukrani kwa Wizara husika nikijua hapa wapo wadau na wahusika watakao lifanyia kazi.
Mabaraza ya Ardhi yote, ya Kata na Wilaya yana Usumbufu mkubwa sana kupita kiasi ktk nchi hii.Ni vyema Mabaraza hayo yakarejeshwa chini ya Mahakama ya Tz iliyopo ktk Wizara ya Sheria na Katiba. Mabaraza hayo ya Ardhi yaondolewe kutoka ktk Wizara ya Ardhi ambako kuna matatizo yaliyojaa tele.
Chini ya Mahakama za kawaida. iundwe Idara ya Ardhi Katika Mahakama zote za Mwanzo na kwenye Mahakama zote za Wilaya na Kwenye Mahakama Kuu kama ambavyo ilivyo sasa.
 
Mabaraza ya Ardhi yote, ya Kata na Wilaya yana Usumbufu mkubwa sana kupita kiasi ktk nchi hii.Ni vyema Mabaraza hayo yakarejeshwa chini ya Mahakama ya Tz iliyopo ktk Wizara ya Sheria na Katiba. Mabaraza hayo ya Ardhi yaondolewe kutoka ktk Wizara ya Ardhi ambako kuna matatizo yaliyojaa tele.
Chini ya Mahakama za kawaida. iundwe Idara ya Katika Mahakama zote za Mwanzo na kwenye Mahakama zote za Wilaya na Kwenye Mahakama Kuu kama ambavyo ilivyo sasa.
Hii itakuwa suluhisho mno.Maana maauzi mengi ya kimahakama juu ya ardhi bado husubilia tena maamuzi ya baraza sehemu ambayo janja janja zimekuwa kubwa mno.
 
Back
Top Bottom