Hivi ni kwanini Serikali hii ya Rais Magufuli inawahofia mno wapinzani?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,159
Nimekuwa nikiwasikiliza wanasiasa wa Chama tawala cha CCM, katika majukwaa ya kisiasa na nilichokishuhudia ni viongozi hao kujigamba kuwa, vyama vya upinzani vya nchi hii vipo mahututi na vinasubiri kuzikwa tu, kutokana na juhudi kubwa inayofanywa na Mheshimiwa Rais ya kufanya maendeleo mbalimbali nchini, kama vile, ujenzi wa reli ya SGR, ujenzi wa Stiegler's Gorge na ununuzi wa nduge za dreamliners, ujenzi unaoendelea hapa nchimi wa barabara za lami na mengine mengi mazuri yanayofanywa na serikali hii ya awamu ya tano, na kuwa wapinzani hawana hoja za kuwaambia watanzania, kwa maana hiyo wanachosubiri ni vyama vyao kufa tu

Wamediriki baadhi yao kutamka kuwa wananchi watakaoendelea kuchagua wapinzani, akili zao siyo nzuri!

Hata hivyo maneno hayo ya majukwaani yana tofauti kubwa sana na vitendo vinavyofanywa na viongozi wa serikali kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Kama ni kweli serikali hii ingelikuwa inajiamini kiasi hicho cha kuwafanyia mazuri matupu wananchi wake, ni kwanini basi hawawaachi wananchi hao wakachambua mchele na pumba kwenye sanduku la kura??

Mbona figisu figisu zimekuwa nyingi mno katika zoezi zima la chaguzi za serikali ya mitaa zinazoendelea??

Hivi serikali hii ya awamu ya tano, imefikia kiwango hiki cha kufanya hila hizi ninazoweza kudiriki kuziita za kipuuzi kiasi hiki??

Tunashuhudia upendeleo wa wazi kabisa wa shughuli za kisiasa hapa nchini, ambapo Rais Magufuli alitangaza, kuvipiga marufuku vyama vya upinzani kutofanya shughuli zozote za kisiasa hadi mwaka 2020, wakati yeye na chama chake cha CCM, tukiwaona kila kukicha wakifanya kampeni nchi nzima!

Tumeshuhudia "uhuni" wa hali ya juu, ukifanywa na watendaji wa serikali wa kata, kuwanyima haki yao viongozi wa vyama ya upinzani kugombea kwenye serikali za mitaa, kwa sababu za kitoto kabisa, kama vile kuzikimbia ofisi zao, kwa nia tu ya "kuwakacha" viongozi wa uoinzani, wanaorejesha fomu zao walizozijaza za kuomba uongozi wa serikali ya mitaa

Tumeshuhudia pia wasimamizi hao wa uchaguzi wakiwa-disqualify viongozi wa upinzani kwa sababu za kitoto kabisa, kama vile kudai kuwa wamejaza kimakosa, fomu zao kwa kuandika vyama vyao wanavyotoka, kama vile kuandika unatoka chama cha ACT wazalendo au Chadema, kuwa umejaza kifupi, wakati wenzao wa kutoka chama tawala wakijaza kuwa wametoka chama cha CCM na kuambiwa kuwa wamejaza kwa usahihi wa asilimia 100!

Hebu niwakumbushe kidogo tu siku za nyuma wakati kampeni za kwanza kabisa kufanyika mwaka 1995, baada ya kurejesha mfumo wa vyama vingi, mashabiki wa mgombea urais wa chama cha NCCR Mageuzi, walizoea kumbeba mgombea wao wa urais, Augustine Mrema, kuonyesha kuwa wanampenda, ndipo Jeshi letu la Polisi likawa linawapiga wafuasi hao wa NCCR Mageuzi, ndipo Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, akaingilia kati kuwa kama washabiki wao wameamua kumbeba mzoga mzoga kama maiti mgombea wao, nyinyi Polisi shida yenu ni ninii??

Waache wenyewe mashabiki wao waendelee kumbeba kama mzoga na wala msiwabugudhi mashabiki wao

Hivi hawa CCM wameshawahi kuusikia ule msemo maarufu wa kiswahili unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza?

Kama nyinyi CCM mnajiamini kiasi hicho, kwanini hamuachi uwanja wa ushindani ulio sawa, badala ya kufanya hizi hila za kitoto kabisa??
 
Chama cha upinzani kinachong’ang’ania kuhakikisha madarakani kinaficha madudu mengi. Kwenye Demokrasia ya kweli mfano Marekani Republican hawaezi kujisifu kuwa watawala wa miaka 50 mfululizo au Conservative kuwa madarakani kwa miaka 20.
Ninachokiona mimi ni kuwa hiki kiburi cha hawa watawala wetu kuweza kutusubabishia matatizo makubwa ya kiuchumi nchi hii,

Mfano halisi ni hali mbaya ya uchumi wa nchi ya Zimbabwe ilivyo sasa, ambayo imesababishwa na kiburi cha aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe, kuamini kuwa anao ubavu wa kupambana na mabeberu!

Tunaona dhahiri tunavyoifuata njia hiyo hiyo waliyopitia wazimbabwe, kwa watawala wetu kila kukicha tukiwaona wakiwatukana hao wanaiwaita mabeberu, ambapo kila kukicha tunawaona wakitembeza bakuli la "kimatonya" kuwaomba misaada hao hao mabeberu!
 
Nchi hii chini ya hiki chama kizee inaongoza kwa ghiliba na usanii, wanahofia wakiwaruhusu wapinzani watawambia wananchi uhalisia.
Watanzania tumebaki kuimba mapambio na kulishwa matango pori!
Kwa kila siku tunaambiwa uchumi umekuwa, wakati sio kweli. Mara tunajenga miundo mbinu yetu kwa pesa za ndani wakati deni la taifa limekuwa kwa kasi ya ajabu.
Pesa zinazo kopwa zinapelekwa wapi?
Nchi haina vipaumbele, zaidi ya kutegemea akili ya MTU mmoja! Hata hivyo wenye akili wameshajua ukweli.
 
Nchi hii chini ya hiki chama kizee inaongoza kwa ghiliba na usanii, wanahofia wakiwaruhusu wapinzani watawambia wananchi uhalisia.
Watanzania tumebaki kuimba mapambio na kulishwa matango pori!
Kwa kila siku tunaambiwa uchumi umekuwa, wakati sio kweli. Mara tunajenga miundo mbinu yetu kwa pesa za ndani wakati deni la taifa limekuwa kwa kasi ya ajabu.
Pesa zinazo kopwa zinapelekwa wapi?
Nchi haina vipaumbele, zaidi ya kutegemea akili ya MTU mmoja! Hata hivyo wenye akili wameshajua ukweli.
 
Nchi hii chini ya hiki chama kizee inaongoza kwa ghiliba na usanii, wanahofia wakiwaruhusu wapinzani watawambia wananchi uhalisia.
Watanzania tumebaki kuimba mapambio na kulishwa matango pori!
Kwa kila siku tunaambiwa uchumi umekuwa, wakati sio kweli. Mara tunajenga miundo mbinu yetu kwa pesa za ndani wakati deni la taifa limekuwa kwa kasi ya ajabu.
Pesa zinazo kopwa zinapelekwa wapi?
Nchi haina vipaumbele, zaidi ya kutegemea akili ya MTU mmoja! Hata hivyo wenye akili wameshajua ukweli.
Wananchi wote wa nchi hii tunapaswa tuamke na kuona kuwa njia anayotipeleka huyu Rais wetu anatupoteza na anaielekeza shimoni nchi yetu
 
Nimekuwa nikiwasikiliza wanasiasa wa Chama tawala cha CCM, katika majukwaa ya kisiasa na nilichokishuhudia ni viongozi hao kujigamba kuwa, vyama vya upinzani vya nchi hii vipo mahututi na vinasubiri kuzikwa tu, kutokana na juhudi kubwa inayofanywa na Mheshimiwa Rais ya kufanya maendeleo mbalimbali nchini, kama vile, ujenzi wa reli ya SGR, ujenzi wa Stiegler's Gorge na ununuzi wa nduge za dreamliners, ujenzi unaoendelea hapa nchimi wa barabara za lami na mengine mengi mazuri yanayofanywa na serikali hii ya awamu ya tano, na kuwa wapinzani hawana hoja za kuwaambia watanzania, kwa maana hiyo wanachosubiri ni vyama vyao kufa tu

Wamediriki baadhi yao kutamka kuwa wananchi watakaoendelea kuchagua wapinzani, akili zao siyo nzuri!

Hata hivyo maneno hayo ya majukwaani yana tofauti kubwa sana na vitendo vinavyofanywa na viongozi wa serikali kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Kama ni kweli serikali hii ingelikuwa inajiamini kiasi hicho cha kuwafanyia mazuri matupu wananchi wake, ni kwanini basi hawawaachi wananchi hao wakachambua mchele na pumba kwenye sanduku la kura??

Mbona figisu figisu zimekuwa nyingi mno katika zoezi zima la chaguzi za serikali ya mitaa zinazoendelea??

Hivi serikali hii ya awamu ya tano, imefikia kiwango hiki cha kufanya hila hizi ninazoweza kudiriki kuziita za kipuuzi kiasi hiki??

Tunashuhudia upendeleo wa wazi kabisa wa shughuli za kisiasa hapa nchini, ambapo Rais Magufuli alitangaza, kuvipiga marufuku vyama vya upinzani kutofanya shughuli zozote za kisiasa hadi mwaka 2020, wakati yeye na chama chake cha CCM, tukiwaona kila kukicha wakifanya kampeni nchi nzima!

Tumeshuhudia "uhuni" wa hali ya juu, ukifanywa na watendaji wa serikali wa kata, kuwanyima haki yao viongozi wa vyama ya upinzani kugombea kwenye serikali za mitaa, kwa sababu za kitoto kabisa, kama vile kuzikimbia ofisi zao, kwa nia tu ya "kuwakacha" viongozi wa uoinzani, wanaorejesha fomu zao walizozijaza za kuomba uongozi wa serikali ya mitaa

Tumeshuhudia pia wasimamizi hao wa uchaguzi wakiwa-disqualify viongozi wa upinzani kwa sababu za kitoto kabisa, kama vile kudai kuwa wamejaza kimakosa, fomu zao kwa kuandika vyama vyao wanavyotoka, kama vile kuandika unatoka chama cha ACT wazalendo au Chadema, kuwa umejaza kifupi, wakati wenzao wa kutoka chama tawala wakijaza kuwa wametoka chama cha CCM na kuambiwa kuwa wamejaza kwa usahihi wa asilimia 100!

Hebu niwakumbushe kidogo tu siku za nyuma wakati kampeni za kwanza kabisa kufanyika mwaka 1995, baada ya kurejesha mfumo wa vyama vingi, mashabiki wa mgombea urais wa chama cha NCCR Mageuzi, walizoea kumbeba mgombea wao wa urais, Augustine Mrema, kuonyesha kuwa wanampenda, ndipo Jeshi letu la Polisi likawa linawapiga wafuasi hao wa NCCR Mageuzi, ndipo Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, akaingilia kati kuwa kama washabiki wao wameamua kumbeba mzoga mzoga kama maiti mgombea wao, nyinyi Polisi shida yenu ni ninii??

Waache wenyewe mashabiki wao waendelee kumbeba kama mzoga na wala msiwabugudhi mashabiki wao

Hivi hawa CCM wameshawahi kuusikia ule msemo maarufu wa kiswahili unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza?

Kama nyinyi CCM mnajiamini kiasi hicho, kwanini hamuachi uwanja wa ushindani ulio sawa, badala ya kufanya hizi hila za kitoto kabisa??
Tatizo kilakitu tunazani ni mabavu hatakuomba tutumie mabavu hatufiki tukikumbuka wavuvi vyavu halali zilichomwa huu ulikuwa muda wetu sasa kwakua wanahisi mambo mengi hayakuwa sahihi sasa nawao wameshuka kwenye cheo chaungu nakuvaa ubinaadamu wameingiwa nahofu kubwa wanajaribu mabavu.
 
Back
Top Bottom