Hivi mbunge wa Segerea kazi yake nini?

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Sep 11, 2010
4,271
2,401
Nauliza hivi kwa mshangao sana. Ni kuhusu suala la maji. Yapo maeneo maji wanapata kila siku. Kuanzia Bima kwenda hadi relini kule maji ni kila wakati. Mshangao kwao ni maji yakikatika.

Maeneo ya Segerea kuelekea Kisukuru na Bonyokwa huko kuna changamoto sana ya maji. Huku yakitoka inabidi tushangae. Kwa nini? Au mifumo ya kuleta maji katika maeneo hayo tajwa ni miwili tofauti?

Kwa nini basi pasifanywe mgao kati ya maeneo haya? Huku tunanunua maji ya magari. Ni ghali kweli wakati mabomba tumefungiwa na dawasa. Msimu huu wa mvua tunaponea ya mvua. Mbunge na madiwani mnafanya kazi gani?

Au hayo magari ya kusomba maji ni miradi yenu? Tunahitaji na tunataka maji ya uhakika kama maeneo mengine
 
Huyo mbunge inaonekana Kisukuru na Kimanga hapamuhusu hivi!

Kila siku makamu wa Raisi anakuja kitaani barabara ni mbaya kichizi ila mbunge yupo! Barabara kuanzia Bima mpaka Kimanga ni mbaya na chafu hasa kipande cha bima mpaka Mawenzi.

Kuna barabara ya Maji Chumvi kuja kwa Swayi mpaka kuunga Kimanga ni mbaya mno japo ni njia kubwa sana inatumiwa na watu kama shortcut ya Segerea na Kinyerezi
Nauliza hivi kwa mshangao sana. Ni kuhusu suala la maji. Yapo maeneo maji wanapata kila siku. Kuanzia Bima kwenda hadi relini kule maji ni kila wakati. Mshangao kwao ni maji yakikatika.

Maeneo ya Segerea kuelekea Kisukuru na Bonyokwa huko kuna changamoto sana ya maji. Huku yakitoka inabidi tushangae. Kwa nini? Au mifumo ya kuleta maji katika maeneo hayo tajwa ni miwili tofauti?

Kwa nini basi pasifanywe mgao kati ya maeneo haya? Huku tunanunua maji ya magari. Ni ghali kweli wakati mabomba tumefungiwa na dawasa. Msimu huu wa mvua tunaponea ya mvua. Mbunge na madiwani mnafanya kazi gani?

Au hayo magari ya kusomba maji ni miradi yenu? Tunahitaji na tunataka maji ya uhakika kama maeneo mengine
 
Huyo mbunge inaonekana Kisukuru na Kimanga hapamuhusu hivi!

Kila siku makamu wa Raisi anakuja kitaani barabara ni mbaya kichizi ila mbunge yupo! Barabara kuanzia Bima mpaka Kimanga ni mbaya na chafu hasa kipande cha bima mpaka Mawenzi.

Kuna barabara ya Maji Chumvi kuja kwa Swayi mpaka kuunga Kimanga ni mbaya mno japo ni njia kubwa sana inatumiwa na watu kama shortcut ya Segerea na Kinyerezi
Wakati wa JPM barabara ya kutoka Chang'ombe kupitia kwa Swai hadi maji chumvi ilikuwa ijengwe kwa kiwango cha lami tena barabara pana lakini baadhi yenu wakazi wa huko mkaweka pingamizi mahakamani barabara isijengwe kwa kuwa baadhi ya nyumba zingebomolewa, Serikali ikaamua kuhamishia fungu la huo mradi kwenda kujenga barabara ya kutoka Gongolamboto kupitia Bongolandege hadi Kinyerezi darajani.
 
Wakati wa JPM barabara ya kutoka Chang'ombe kupitia kwa Swai hadi maji chumvi ilikuwa ijengwe kwa kiwango cha lami tena barabara pana akini baadhi yenu wakazi wa huko mkaweka pingamizi mahakamani barabara isijengwe kwa kuwa baadhi ya nyumba zingebomolewa, Serikali ikaamua kuhamishia fungu la huo mradi kwenda kujenga barabara ya kutoka Gongolamboto kupitia Bongolandege hadi Kinyerezi darajani.
Ni kweli pingamizi liliwekwa na dingi yangu mdogo ndio alisimamia hilo ila hakukuwa na sababu ya kuvunja nyumba kwa maana ni barabara ya mtaani hii! Ina maana wangevunja wangepaswa kutulipa fidia ule ujinga wa kuvunja nyumba ya million 100 kisha uwalipe watu 25m waende kimbiji ndio hatukuutaka.

Fedha ilikuwa inatolewa na Worldbank na
ramani ya mipango miji ilikuwa inasema barabara kubwa ya highway ijengwe kuanzia Mazda ikiambaa na bomba la dawasco mpaka bonde la mchicha kisha ipande jeshini. Ingine irudi maji chumvi! Kule ndiko kulipaswa kuvunjwe kwa kufuata vigezo maana waliojenga hovyo ndio waliingilia hifadhi ya barabara.

Barabara ya mtaa wangejenga hata ya kiwango cha Zege isingekuwa tabu ila tu nyumba kuvunja ndio hatukutaka sababu viwanja vyetu eneo lote vimepimwa hatujajenga scattered kama Upogoroni!
 
Huyo mbunge inaonekana Kisukuru na Kimanga hapamuhusu hivi!

Kila siku makamu wa Raisi anakuja kitaani barabara ni mbaya kichizi ila mbunge yupo! Barabara kuanzia Bima mpaka Kimanga ni mbaya na chafu hasa kipande cha bima mpaka Mawenzi.

Kuna barabara ya Maji Chumvi kuja kwa Swayi mpaka kuunga Kimanga ni mbaya mno japo ni njia kubwa sana inatumiwa na watu kama shortcut ya Segerea na Kinyerezi
Hii barabara ya shortcut kumbe unaipata? Nasikia ni mradi wa watu. Wanachonga na kumwaga vifusi na siku mbili ubovu unarudi. Ni njia kubwa sana ila hakuna mikakati yoyote. Wenzao ubungo sijui wamewezaje miundombinu.
 
Hii barabara ya shortcut kumbe unaipata? Nasikia ni mradi wa watu. Wanachonga na kumwaga vifusi na siku mbili ubovu unarudi. Ni njia kubwa sana ila hakuna mikakati yoyote. Wenzao ubungo sijui wamewezaje miundombinu.
Inapita street kabisa yani😅 naijua kama sala ya baba yetu
 
Nauliza hivi kwa mshangao sana. Ni kuhusu suala la maji. Yapo maeneo maji wanapata kila siku. Kuanzia Bima kwenda hadi relini kule maji ni kila wakati. Mshangao kwao ni maji yakikatika.

Maeneo ya Segerea kuelekea Kisukuru na Bonyokwa huko kuna changamoto sana ya maji. Huku yakitoka inabidi tushangae. Kwa nini? Au mifumo ya kuleta maji katika maeneo hayo tajwa ni miwili tofauti?
Kwa katiba yetu iliyopo mleta mada unajua kazi ya mbunge?

Tangu lini mbunge akawa na fungu la kujengea miundombinu ya maji jimboni kwake?
 
Kuna eneo fulani huku Kinyerezi njia ya kuelekea Saranga Dawasco wamesambaza mabomba ila maji kutoka ni mtihani, juzi kati yakatoka kama siku mbili mfululizo ukawa kama mjadala mtaani, kuna mzee akasema au yana sumu, maana kutoka siku mbili ni miujiza.
 
Kuna eneo fulani huku Kinyerezi njia ya kuelekea Saranga Dawasco wamesambaza mabomba ila maji kutoka ni mtihani, juzi kati yakatoka kama siku mbili mfululizo ukawa kama mjadala mtaani, kuna mzee akasema au yana sumu, maana kutoka siku mbili ni miujiza.
Inafika hatua maji yakitoka watu wanashangaa
 
Back
Top Bottom