Hivi kweli tumefika huku??

Hivi kweli tumefika huku??

Ni dhambi ndiyo ila ukumbuke mtu akitubu husamehewa. Jamaa tayari keshatoka kimaisha kiulaini kabisa bila jasho. Kazi anayo huyo aliyepanga chumba na sebule. Wanaume wadanganyifu hata wanawake pia na unapaswa kuwa makini. Alichofanyiwa huyo mwanamke ndicho alichokuwa anakitafuta wala asilalamike. Malipo ni hapa hapa duniani
Kama malipo ni hapa hapa na jamaa aliyejengewa nyumba na mdada naye ajiandae kulizwa?
Maana yeye asipotendewa vibaya atakuwa hajalipwa,amepata faida tu?
 
Unaweza kuta huyo dada kajitungia tu story ili safari iwe fupi au ili msimtongoze mpaka amefika mwisho wa safari yake kawaacha madume matatu bado mnafikiria hadithi yake...yeye kaenda zake kwa mumewe.
Kama alitunga hiyo story basi huyo dada ni akili kubwa. Ila kuna wakina sie hata ulete story ipi hatukuachi hivi hivi.
 
Chama cha Mabaharia na waomba mumtendee Haki huyo mwanaume Aliyekula hela za huyo dada na kujenga nyumba kisha aka muweka mwanamke mwingine

Pia mumpandishe cheo haraka sana. Anastahiki kupewa uenyekiti wa Kanda ya Tanzania mashariki
Shida ni kwamba uyo mwanamke pia atamsumbua baharia, apo ni hakuna kuoa, kuoa nikujipunguzia marks za ubaharia
 
Kama malipo ni hapa hapa na jamaa aliyejengewa nyumba na mdada naye ajiandae kulizwa?
Maana yeye asipotendewa vibaya atakuwa hajalipwa,amepata faida tu?
Kulipwa kupo kwa namna nyingi na siyo mpaka adhulumiwe nyumba.
 
Karucee u mwendakuzimu
Huwezi kuwa na akili kubwa
Kuwaza na kuwazua kijamii
Kumnanga mkima mwenzio
Kisa tu kaloba stepu stejini
Kacheza rege ilhali ni blues!
Kudos Madame Karucee

Bazazi
Women can be so dumb when in love.

And that's why we almost always get caught when cheating.

If a man respects you as his woman, strives hard to provide for you, why can't you just be patient if he is not good in bed?

No man can cater to all your needs at the same time. He cannot be financially, emotionally and sexually at his peak all the time you are together.

No man is perfect.
 
Women can be so dumb when in love.

And that's why we almost always get caught when cheating.

If a man respects you as his woman, strives hard to provide for you, why can't you just be patient if he is not good in bed?

No man can cater to all your needs at the same time. He cannot be financially, emotionally and sexually at his peak all the time you are together.

No man is perfect.
Mawazo mazuri ila magumu kutekelezeka kwa kizazi chenu cha . com
 
Mkuu wewe acha tu ...ndio maana wajuzi wa lugha wa kasema kufa kufaana ... naona dada zetu wameamua ku-hang na hiyo nahau
Asee tabu tupu ... mpoto alisema kuni ya ziada huwa inaicheka inayoteketea motoni
 
Salaam wanajukwaa!

Jana nikiwa safarini natoka mkoani kurejea Dar-es-salaam,tulisafiri watu kama wanne hivi,mdada mmoja wa makamo,na wanaume 3,wote hatukuwa tunafahamiana. Lakini kama ujuavyo safari ikiwa ndefu sana,story huwa kitu cha kawaida.

Basi baada ya kimya cha muda mrefu,dereva akaanzisha story za hapa na pale,akajikuta anasimulia habari ya maisha yake ya mahusiano,na kumtuhumu mkewe namna alivyokuwa akitoka na wanaume wengine,walivyoachana na baadaye kurudiana,(ni story ndefu sana ya huyu jamaa lakini sitaieleza sana hiyo,japo jamaa alipita nyakati ngumu sana)

Kilichonifanya niandike hii mada ni huyu dada abiria mwenzetu,alivyojiachia kusimulia mikasa yake na namna alivyomuanika mumewe (japo ni kweli hatumjui mume wake,lakini hapana...)

Anaanza kwa kulaumu wanaume namna tulivyo wadanganyifu,nikichoka alipokuwa akielezea udanganyifu huo, anaanza!

"Mimi nimeolewa miaka 9 iliyopita,mume wangu alikuwa na udhaifu sana kitandani,nilivumilia miaka 4 nikashindwa,nilitafuta mwanaume mwingine,hakuwa na kazi,nilimsaidia sana yule kaka, huwezi amini nilikuwa namuibia mume wangu pesa,nampelekea huyu mwanaume aanze biashara,wakati anatafuta kazi,maana alikuwa amesoma...

Nilichukua mkopo bila mume wangu kujua,milioni 25 nikamwambia tujenge nyumba mkoa jirani,ili ikiisha tuhamie huko,mimi nimuache mume wangu (hapo watu wote kwenye gari tupo kimya tunamsikiliza kwa makini,moyoni nikiwa najisemea,masikini dada anaonyesha namna alivyo mjinga)

Anasema jamaa akaenda kununua kiwanja na kujenga kingolwira Morogoro,jamaa akamwambia nyumba imefikia level nzuri tu,ila pesa imeisha,bado finishing na fensi. Bila aibu mdada anajisemea " Nilimzunguka mume wangu, saving account yangu ambayo mume alikuwa anaijua ulikuwa na milioni 18,nilichukua ile pesa yote nikampa mpnz wangu amalizie fensi.

"Cha ajabu baada ya nyumba kukamilika nilimwambia anipeleke niione ili nitafute namna ya kuachana na mume wangu,alianza kunipiga chenga,nilimuomba pesa mume wangu Milioni tano niende kijijini kwetu kwa ajili ya kumalizia nyumba ya wazazi,akanipa,tukaenda na mpnz wangu Zanzibar ili niongee naye vizuri,na nilijua ninachofanya makusudi ili mume wangu anifukuze"

"Basi mume wangu alivyojua kuwa sikwenda kijijini alikasirika sana,akaniambia niende kwetu nikapumzike,nikafurahi sana nikijua ndo tiketi ya kwenda kuanza maisha na mpnz wangu,maana nyumba tayari tulikuwa nayo na alikuwa ameshapata kazi..."

"Wanaume mlivyokuwa na roho mbaya,yule kaka kumbe alikuwa anajenga Dar,na alikuwa na mwanamke mwingine,anampeleka kumuonyesha nyumba hiyo hiyo na kumwambia wakioana ataishi naye hapo,haki ya Mungu nilisikia roho inatoka....(khaaaa)

Analalamika kuwa jamaa aliingia mitini,mdada mpaka sasa ameachana na mume wake,na mkopo bado anaendelea kulipa na amepanga kimara chumba na sebule,na anamlaani mpnz wake aliyemdanganya kuwa akiachana na mume wake yeye atamuoa...

Hakika maisha haya yana mengi,mahusiano na ndoa... Yamejaa visa na mikasa,mengi ya kujifunza. Baada ya dada kushuka kimara watu wakamsema sana kwa kumtukana "mpumbavu bora hata asisimulie" wasijue atakuwa mgonjwa mahututi kisaikolojia,kutokana na ulevi wa penzi...hivyo kusimulia kunamfanya angalau apate nafuu

Dada kama uko hapa jukwaani ninakupa pole,lakini pia samahani kwa kuweka story yako hapa,inaweza kuwasaidia wengine wanaotaka kukimbia ndoa zao ili wakaishi na wapenzi wao kwa kigezo cha waume kutowafikisha vileleni,tafuteni namna nyingine ili waume zenu wawe bora kuliko kukimbilia nje,kuna madhara makubwa sana.
stori bora sana na yenye funzo ndani yake kwa wote wenye tabia kama hii ya huyo mwanadada
 
Kuna siku ulihadithia kisa fulan cha mapenz
Nikajua ni ke
Nikasema yes ngoja nimzamie pm
Kusoma comment inayofuata umecoment kiume duh
Nikajipa muda
Nikakusoma tena oooh kumbe ni dume
Oyoyoyoyooooo nikasitisha safari
Ulikua umeweka avatar ya kike

Nlikua niingie cha kike
Seriously kabsaaa nlishakupangia namna ya kukupiga sound mzee baba

But sorry aise, duuh hizi ID fake shida Sana
Hahaha hahahahsshshshshsh hahsshsh... sikuwahi kuweka avatar ya kike mzee baba ... but Kuna wakati server za jf huwa zina zingua unaweza kushangaa avatar ya mtu unaye mjua imebadilika na kuwa avatar ya mtu ya mtu mwingine. ..Mara nyingi hii huwa inatokea kwa sisi tunao tumia jf app
 
Wanawake sio viumbe vinavyostahili kuwezeshwa,... Wakiwa na uwezo tu utajuta,.. Ni viumbe hatari kuliko simba. Mi napinga kbs kumwezesha mwanamke,.. Wana roho mbaya sana hawa viumbe
 
Back
Top Bottom