Hivi kweli tumefika huku??

Hivi kweli tumefika huku??

Like seriously. .waweza kukuta jamaa alikuwa na business ideas. .Lakini ikawa ana kwama kupata capital. ..so imejitokeza opportunity kama hiyo Unadhani angeiacha Thubutu '' Hata wewe usingediriki kufanya hivyo' .....

Ila kumuacha dahh!!! Hakufanya vyema amemkatili sana ''Ijapokuwa huyo dada Alifanya unyama mkubwa sana kwa mumewe. ...so let's assume kuwa hayo ni maamuzi ya Fate ''so Pali kuwa hakuna namna ya kuepusha hayo yasiweze kujiri
Angemuacha tu,bila kumdhulumu pesa zake nyingi....
 
Salaam wanajukwaa!

Jana nikiwa safarini natoka mkoani kurejea Dar-es-salaam,tulisafiri watu kama wanne hivi,mdada mmoja wa makamo,na wanaume 3,wote hatukuwa tunafahamiana. Lakini kama ujuavyo safari ikiwa ndefu sana,story huwa kitu cha kawaida.

Basi baada ya kimya cha muda mrefu,dereva akaanzisha story za hapa na pale,akajikuta anasimulia habari ya maisha yake ya mahusiano,na kumtuhumu mkewe namna alivyokuwa akitoka na wanaume wengine,walivyoachana na baadaye kurudiana,(ni story ndefu sana ya huyu jamaa lakini sitaieleza sana hiyo,japo jamaa alipita nyakati ngumu sana)

Kilichonifanya niandike hii mada ni huyu dada abiria mwenzetu,alivyojiachia kusimulia mikasa yake na namna alivyomuanika mumewe (japo ni kweli hatumjui mume wake,lakini hapana...)

Anaanza kwa kulaumu wanaume namna tulivyo wadanganyifu,nikichoka alipokuwa akielezea udanganyifu huo, anaanza!

"Mimi nimeolewa miaka 9 iliyopita,mume wangu alikuwa na udhaifu sana kitandani,nilivumilia miaka 4 nikashindwa,nilitafuta mwanaume mwingine,hakuwa na kazi,nilimsaidia sana yule kaka, huwezi amini nilikuwa namuibia mume wangu pesa,nampelekea huyu mwanaume aanze biashara,wakati anatafuta kazi,maana alikuwa amesoma...

Nilichukua mkopo bila mume wangu kujua,milioni 25 nikamwambia tujenge nyumba mkoa jirani,ili ikiisha tuhamie huko,mimi nimuache mume wangu (hapo watu wote kwenye gari tupo kimya tunamsikiliza kwa makini,moyoni nikiwa najisemea,masikini dada anaonyesha namna alivyo mjinga)

Anasema jamaa akaenda kununua kiwanja na kujenga kingolwira Morogoro,jamaa akamwambia nyumba imefikia level nzuri tu,ila pesa imeisha,bado finishing na fensi. Bila aibu mdada anajisemea " Nilimzunguka mume wangu, saving account yangu ambayo mume alikuwa anaijua ulikuwa na milioni 18,nilichukua ile pesa yote nikampa mpnz wangu amalizie fensi.

"Cha ajabu baada ya nyumba kukamilika nilimwambia anipeleke niione ili nitafute namna ya kuachana na mume wangu,alianza kunipiga chenga,nilimuomba pesa mume wangu Milioni tano niende kijijini kwetu kwa ajili ya kumalizia nyumba ya wazazi,akanipa,tukaenda na mpnz wangu Zanzibar ili niongee naye vizuri,na nilijua ninachofanya makusudi ili mume wangu anifukuze"

"Basi mume wangu alivyojua kuwa sikwenda kijijini alikasirika sana,akaniambia niende kwetu nikapumzike,nikafurahi sana nikijua ndo tiketi ya kwenda kuanza maisha na mpnz wangu,maana nyumba tayari tulikuwa nayo na alikuwa ameshapata kazi..."

"Wanaume mlivyokuwa na roho mbaya,yule kaka kumbe alikuwa anajenga Dar,na alikuwa na mwanamke mwingine,anampeleka kumuonyesha nyumba hiyo hiyo na kumwambia wakioana ataishi naye hapo,haki ya Mungu nilisikia roho inatoka....(khaaaa)

Analalamika kuwa jamaa aliingia mitini,mdada mpaka sasa ameachana na mume wake,na mkopo bado anaendelea kulipa na amepanga kimara chumba na sebule,na anamlaani mpnz wake aliyemdanganya kuwa akiachana na mume wake yeye atamuoa...

Hakika maisha haya yana mengi,mahusiano na ndoa... Yamejaa visa na mikasa,mengi ya kujifunza. Baada ya dada kushuka kimara watu wakamsema sana kwa kumtukana "mpumbavu bora hata asisimulie" wasijue atakuwa mgonjwa mahututi kisaikolojia,kutokana na ulevi wa penzi...hivyo kusimulia kunamfanya angalau apate nafuu

Dada kama uko hapa jukwaani ninakupa pole,lakini pia samahani kwa kuweka story yako hapa,inaweza kuwasaidia wengine wanaotaka kukimbia ndoa zao ili wakaishi na wapenzi wao kwa kigezo cha waume kutowafikisha vileleni,tafuteni namna nyingine ili waume zenu wawe bora kuliko kukimbilia nje,kuna madhara makubwa sana.
Unaweza kuta huyo dada kajitungia tu story ili safari iwe fupi au ili msimtongoze mpaka amefika mwisho wa safari yake kawaacha madume matatu bado mnafikiria hadithi yake...yeye kaenda zake kwa mumewe.
 
Kabisa ni Ujinga mkubwa ...imagine hapo kama alizaa na mumewe. ..wakati huu itakuwa ana wa pitisha watoto wake kwenye hali ngumu kwaajili ya Ujinga wake ...
Yawezekana hata wa darasa la saba asifanye alichofanya yeye
 
Ujue namfahamu vizuri huyo dada. Ni kweli yupo humu na ni mchangiaji mzuri wa JLW. Na mimi ni yule dereva wa lile gari ulilopanda.

Sema nini mwanangu hujafanya poa kusimulia hiyo story humu jukwaani. Hapa mabaharia wote waliosoma hiyo simulizi wameazimia kukuvua vyeo vyote vya kibaharia.
 
Unaweza kuta huyo dada kajitungia tu story ili safari iwe fupi au ili msimtongoze mpaka amefika mwisho wa safari yake kawaacha madume matatu bado mnafikiria hadithi yake...yeye kaenda zake kwa mumewe.
Noup,kwa saikolojia ndogo sana unamjua mtu anayesimilia hadithi ya kusadikika na anayeeleza uhalisia,ukienda msibani hauhitaji kuelekezwa wafiwa,(utawajua tu)

Huyu dada alichokuwa anatafuta ni huruma tu,kwa sababu dereva alikuwa anaelezea yaliyompata kwenye ndoa yake (ya kusikitisha sana)

Dada akaanza kufunguka kuwa wanaume ni mashetani zaidi,kufuatia kudhulumiwa na mtu aliyedai "alimpenda sana" akisahau kuwa yeye alikuwa shetani zaidi kwa mume wake!

Na "facial expression" yake unagundua ni mtu anayepitia majuto sana kutokana pengine na akiyofanya,angekuwa anasogeza story ilikuwa easy sana kujua!

Lakini kubwa zaidi,hakuna hata mmoja aliyekuwa na mambo ya kihuni mle ndani,sikuona hata jicho la kukonyeza hata dereva alionekana wazi kuwa mwenye busara zake

Hivyo mdada hakuwa hata na sababu za kujihami kiasi cha kufikiria story kama hivi
 
Ujue namfahamu vizuri huyo dada. Ni kweli yupo humu na ni mchangiaji mzuri wa JLW. Na mimi ni yule dereva wa lile gari ulilopanda.

Sema nini mwanangu hujafanya poa kusimulia hiyo story humu jukwaani. Hapa mabaharia wote waliosoma hiyo simulizi wameazimia kukuvua vyeo vyote vya kibaharia.
Bahati nzuri ni kwamba mimi sio mwanachama wa hiyo kitu mnaita "baharia" kwa sababu sijawahi hata kuelewa mnamaanisha nini?

Pili kusimulia ni kuwafanya wengine wajifunze, (wanawake wenye hulka kama ya yule dada) wasije sema hatukuwaambia,wanaweza kujitoa kwa wapenzi wao na kuwapa kadi zao za bank,lakini matokeo yake ni kama hayo...

Yaani in short ni kwamba tunajifunza kutokana na makosa ya wengine,kama kweli ni wewe dereva basi utakubaliana nami kwamba kwa hali ile mdada anahitaji kufanyiwa counseling ya nguvu sana ili aishi miaka aliyopangiwa na Mungu wake,vinginevyo atakufa siku si zake...
 
Kuna siku jilikuwa natoka dodoma, nikachukua abiria wanne waliokuwa wanaenda moro, wakaka 3 na mdada mmoja, ile safari ilikuwa fupi sana,tulijikuta kila mtu akihadithia matatizo yake ya mahusiano, yaani asilimia kubwa ya watu wana matatizo sana kwenye mahusiano japo tunatofautiana sana katika kuyakabili
 
Jamabi Mungu kama ameamua kumpa fundisho huyo dada aliyekuwa anasaliti ndoa yake jamaa (mzinzi mwenzake) angeweza kupinga mpango wa Mungu kweli???

Maana mimi najiuliza maswali mengi sana lwenye hilo
Ni mduara, huyo nae zamu yake itafika ya kupewa fundisho..
To every action there is a reaction.
 
Back
Top Bottom