Hivi kwanini wasichana wengi warembo hawapendi kula ugali?

Hivi kwanini wasichana wengi warembo hawapendi kula ugali?

Ktk vyakula vizuri na vyenye kujenga mwili ugali hauko kwenye list,sana sana ugali uko kwenye list ya vyakula vya kukomaza mwili....sasa unataka wasichana wale ugali wa kazi gani?
 
Hahahahaaaa ushaanza sasa ule ujinga wako.
Mauno yanahusiana vipi na nguna?

Sasa Mbona Unakuwa Mkali Tena Wakati Tumeanza Vizuri Tu? Halafu Leo Umekaa Kihasira Hasira au Mambo Yetu Yale Ya Bwawa La MINDU Kufurika Yameshaanza?
 
Ukisema umefanya utafiti, si unatakiwa kutuletea majibu, ama?

Hizi nadhani ni emotions zaidi.
 
Habari watanganyika wenzangu?

Kuna utafiti nimeufanya na sample size yangu nimeichukulia maeneo ya mijini hasa Dar ktk utafiti wangu nimegundua kuwa wasichana wengi warembo hawapendi kula ugali.yani unaweza ukawa na msichana wote mnasikia njaa mkaenda nae kwenye mgahawa wewe ukaagiza nguna lakini yeye ataagiza vijitu vya kjiinga jinga kama vile sausage, chips etc sasa najiuliza kwanini warembo wengi hawapendi kugonga nguna?

Nadhani ungebadirisha matokeo ya utafiti wako nadhani usahihi ungekuwa "hawapendi kula Ugali adharani/ kwa kuonekana"
 
Mie napenda ugali balaa... Tena uwe na nyama choma na kichuri uuuuwiii.... My favourite food.. Ina maana mie sio mrembo???
 
Habari watanganyika wenzangu?

Kuna utafiti nimeufanya na sample size yangu nimeichukulia maeneo ya mijini hasa Dar ktk utafiti wangu nimegundua kuwa wasichana wengi warembo hawapendi kula ugali.yani unaweza ukawa na msichana wote mnasikia njaa mkaenda nae kwenye mgahawa wewe ukaagiza nguna lakini yeye ataagiza vijitu vya kjiinga jinga kama vile sausage, chips etc sasa najiuliza kwanini warembo wengi hawapendi kugonga nguna?

wanaogopa kukata magogo magumu.
 
Tunakula ugali ila hatupendi kula ugali wa migahawani au mahotelini,

Raha ya ugali uusonge mwenyewe nyumbani tena kwa mboga uzipendazo.

Ila ujue pia inategemea na asili ya mtu.
 
kiukweli mi sijui ila ugali na dagaa ni balaaa..... hivyo vibaga tunakuala kuwatia hasara tu wengine mpaka tushibe baga zaelfu ishirini na wine na maji na hapo na nachukua ya kula home ..... sasa ukija kupiga hesabu lazima niwe nimekupiga gape kwenye ulaji..
 
Yani hilo liko wazi.
Wadau ea jamvin eeeeee...
Yan hayo mashauz wanayo hasa watuonapo gent, wakiw peke yao ususan majumban wako vizuriiiii!!!
Bada vs Bamiya fresh inashuka bila tomato.
 
Hahahahahahahahaha.....na bado wanaacha kidogo eti wameshiba mimi kuna kipind nilitoka na ex gf amekula chipsi eti kabakisha nikamwambia usinitanie hebu songeza hiyo plate hapa unafikiria tunatumia pesa za msoga kidogo nimwambie na hiyo juice uliyoacha lete hapa....hahahahahahahaaha

ha ha ha,mkuu we nae balaa,yaelekea mshipa wa aibu ulishakatika miaka mingi sana.
 
Kupunguza mitumbo mikubwa == vitambi

Kama ungekuwa mjanja ungejua kwamba chips ndio mbaya kwenye swala la kunenepeana na vitambi kwasababu ya mafuta.

Hao wenye swagga za kujidai hawalagi ugali ni watu ambao katika mazingira yao ya kawaida chip na hizo sosegi wanazipata kwa nadra. Kwahiyo siku wakipata mtu wakuwanunulia lazima watumie hiyo nafasi vizuri. Na asikudanganye mtu, huko makwao wanaula sana ugali.

Sema sasa utamuonaje wa maana asipokuletea mapozz ya "Bae mi sipendi kabisa ugali, alafu nipo kwenye diet. Ntakula tu chips kuku!" as if chips kuku ndio chakula healthier kuliko vingine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom