Hivi kwanini Mungu ana wivu?

Hivi kwanini Mungu ana wivu?

Nimekuuliza chanzo cha mtu ni nini?
Nilikwambia hivi, chanzo cha mtu ni mtu mwenyewe.

Wewe unataka chanzo gani?

Kama una chanzo kingine cha "mtu" kieleze na uthibitishe.
Hujanijibu.
Nimkuuliza muundo wa mtu ni upi, umesema ni muunganiko wa viungo vya mwili.
Sasa na wewe hebu eleza muundo wako wa mtu ulivyo.

Ni prove wrong kwamba, muundo wa mtu sio muunganiko wa viungo na mwili.
Ebu ya jibu kwanza hayo maswali ndipo tutapata majibu ya swali lako.
 
Ni nani?

Kwamba unataka awe mtu au kiumbe fulani?

Hili swali lako linafaa liwe Mungu ni nini?

Mungu ni neno la kufikirika tu ambalo kiuhalisia halipo.
Nani aliyeweka hizo limits kwamba mtu au kiumbe "nani" kitu "nini" ? Nani aliyekwambia hizo ndizo limits na kwamba hakuna options zingine? Ni dimensions za akili zako ndizo zinakudanganya kwamba kuna nyuma mbele juu na chini tu! Kama unafikiria kwa akili hizo basi unajidanganya mno!
 
Anajali na kujupenda kwa kuwa alikuumba ili umtumikie kwanini sasa asiwe na wivu nawe, mfano wewe umpendezeshe mkeo akichukuliwa hutakua na wivu mfano tu
 
Ndio maana nasema huyo Mungu yupo kwenye mawazo yenu ya kufikirika tu.

Hayupo katika uhalisia.
Uhalisia ni nini? Uhalisia ni matokeo ya ulimwengu wa kufikirika.

Ulipoota upo chooni ukajisaidia kitandani hukukiona choo?

Akija mfuasi wa mungu akakuchinja sababu wewe ni mpagani kwa kuwa kaagizwa na mungu kupitia ndoto aue wapagani hutokufa sababu hakumuona mungu?
 
Talanta ya ubishi na ujuaji huwa sina mkuu, ok turidi kwenye mada.

Science ni maarifa ambayo yamegundulika na yanaweza kuthibitika.

Je, unafikiri hadi sasa sayansi imegundua kila kitu kinachohusu ulimwengu?
still research zinaendelea na meaning of scince ni continues/cycle mtu anapoona gap ndipo anapo anzia.

watu walifanya reseach ya mungu hawakumuona,zimebakia imaginations and stories.
 
Anajali na kujupenda kwa kuwa alikuumba ili umtumikie kwanini sasa asiwe na wivu nawe, mfano wewe umpendezeshe mkeo akichukuliwa hutakua na wivu mfano tu
Achukuliwe na nan sasa, wakati kila kitu ni cha mungu mpaka shetani mwenyewe.
 
Anajali na kujupenda kwa kuwa alikuumba ili umtumikie kwanini sasa asiwe na wivu nawe, mfano wewe umpendezeshe mkeo akichukuliwa hutakua na wivu mfano tu
wivu ni tabia ya kibinadamu sio kwamba mnachosema ni maandiko ya wanadamu ili kuendeleza kutawala?
 
nashangaa sana bibilia inavyomuelezea mungu as if binadamu utakuta andiko linasema upon wapi wewe adamu,na adamu akaitika niko hapa mungu wangu.

mda mwengine wanasema mungu alikuwa anatembelea bustani...this is human behaviours
Ukiambiwa umeumbwa kwa mfano wake unaelewaje
 
Nani aliyeweka hizo limits kwamba mtu au kiumbe "nani" kitu "nini" ? Nani aliyekwambia hizo ndizo limits na kwamba hakuna options zingine? Ni dimensions za akili zako ndizo zinakudanganya kwamba kuna nyuma mbele juu na chini tu! Kama unafikiria kwa akili hizo basi unajidanganya mno!
Kwa hiyo kwa mfano, Ukitaka kuuliza jina la mtu fulani unaweza kutumia "Wewe unaitwa nini?

Kwa vile hakuna limits?

Na Ukitaka kuuliza kitu fulani unaweza kutumia, " wewe ni nani hicho?
 
Sorry kwa Hili swali..
Je Biden au TRUMP ni Baba Yako au Anko wako???
Sio Biden au Trump tu, hata ndege kuku pundamilia n.k wote ni wahusika katika maisha yangu! Wote ni viumbe hai! Na muumbaji ni mmoja.Who is Biden? Eti anko sijui mjomba! Nani aliyeset hizo limits? Ndiyo maana nasema huwezi kumuelewa au kuelewa akili za Mungu kwa dimensions za akili za kibinadamu ambazo ziko limited! HAIWEZEKANI!
 
Nyie mwanadai kuna Mungu sie twasema hayupo, kimatinki kabisa haiwezekani kuthibitisha kitu ambacho hakipo , wanaodai Mungu yupo wathibitishe ili kukanusha madai yetu ya kutokuwepo kwake.
Iko hivi mkuu mimi naipenda sayansi na ninaijua kiasi chake, mapungufu ya sayansi ni kwamba bado kuna vitu vingi haijavigundua.

Hivyo, sayansi haiwezi kuthibitisha kutokuwepo kwa Mungu ila haikubaliani na uwepo wake lakini weka kwenye akili kwamba science sio absolute ni bado ina safari ndefu ya kugundua vitu vingi.
 
Kiroho yenyewe ina sound kitapeli tu ,thibitisha kiroho.
Hapa ndo mnapofeli.

Ukishaambiwa kiroho au kiimani ujue hakuna kemikali za kuchanganya hapo ili patokee reaction.

Kuna mawazo, fikra, faith, dreams, thoughts na mambo yanayofanana na hayo na haya mambo yana impact ya moja kwa moja kama ambavyo unavyokojoa kitandani kwa kuona choo ndotoni.

Kwanza hilo lieleweke halafu ndo mambo ya uthibitisho yafuate.
 
Back
Top Bottom