demokrasia
Member
- Apr 6, 2011
- 52
- 5
Nimeingia kwenye ugomvi na girlfriend wangu baada ya kumtamkia maneno mabaya nikiwa na hasira. Sababu ya kufikia hatua ya kumtamkia maneno hayo ni baada ya yeye kunigombeza kwa sababu ya kumtafuta kwenye simu ya rafiki yake baada ya kumkosa yeye kwenye simu yake.
Jambo hilo lilinikera sana kwa sababu sikuona mantiki ya yeye kunikoromea kwa sababu ya issue ndogo kama hiyo. Hilo lilipelekea nikapata hasira na kumtamkia maneno mabaya. Lakini baada ya hasira kuisha, niligundua kuwa sikufanya jambo jema kumtamkia maneno hayo, hivyo nikaamua kumwomba radhi kwa hilo.
Kitendo cha kujishusha na kuomba msamaha imekuwa kama ndio nimewasha moto kwa sababu hataki kunisikiliza hata kidogo na hata simu hapokei, na hii ni wiki ya 3 hataki kupokea simu yangu?
Halafu tatizo ni kwamba ninaishi mbali sana na yeye. Mimi nipo Shinyanga na yeye yupo DSM. Nimejaribu kuhusisha baadhi ya marafiki zake wamweleweshe ili anisamehe, lakini ndio kwanza anazidi kuwa mkali.
Cha kusikitisha ni kwamba nilipoanza tu kuomba msamaha alinitumia sms kwamba "ameamua tu-break up". Sasa najiuliza, hivi kuomba msamaha ni makosa?
Wana JF naombeni maoni yenu.
Jambo hilo lilinikera sana kwa sababu sikuona mantiki ya yeye kunikoromea kwa sababu ya issue ndogo kama hiyo. Hilo lilipelekea nikapata hasira na kumtamkia maneno mabaya. Lakini baada ya hasira kuisha, niligundua kuwa sikufanya jambo jema kumtamkia maneno hayo, hivyo nikaamua kumwomba radhi kwa hilo.
Kitendo cha kujishusha na kuomba msamaha imekuwa kama ndio nimewasha moto kwa sababu hataki kunisikiliza hata kidogo na hata simu hapokei, na hii ni wiki ya 3 hataki kupokea simu yangu?
Halafu tatizo ni kwamba ninaishi mbali sana na yeye. Mimi nipo Shinyanga na yeye yupo DSM. Nimejaribu kuhusisha baadhi ya marafiki zake wamweleweshe ili anisamehe, lakini ndio kwanza anazidi kuwa mkali.
Cha kusikitisha ni kwamba nilipoanza tu kuomba msamaha alinitumia sms kwamba "ameamua tu-break up". Sasa najiuliza, hivi kuomba msamaha ni makosa?
Wana JF naombeni maoni yenu.