Hivi kituko gani unakikumbuka ulikifanya wakati mdogo

Nakumbuka nyumba ya jirani kulikua na watoto watatu baba yao alikua na uwezo kifedha wilayani kwetu lakini pia alikua mkoloni sana. Kwao hawa watoto kukutwa na pesa lilikua ni kosa la jinai linaloadhibiwa kwa bakora lukuki.

Siku moja hawa jamaa zangu wakawa wameiba pesa ndani kwao hivo wakawa wamejaa pesa mfukoni. Jioni ilipofika wakaenda kununua samaki waliokaangwa kwa mama mmoja aliyeitwa mama khalidi. Huyu mama alikua ni jirani yao. Bahati mbaya huyu mama hawakumkuta kwani alikuwa amekwisha ondoka kuwapeleka samaki eneo la biashara ambapo ni mbali kidogo na nyumbani kwake.

Basi jamaa zangu kwa kuhofia kuchelewa nyumbani na kufika kabla ya baba yao hajawasili kutoka kazini wakarejea nyumbani mikono mitupu bila samaki. Mida ya saa mbili usiku baba yao akawa amekwisharejea nyumbani. Huku nyuma mama muuza samaki nae akawa amerejea kwake na akawa amebakiza samaki nadhani biashara haikuwa nzuri. Wanae wakamwambia kina flani walikuja nunua samaki hawakukukuta. Mama wa watu akajua dili hili siliachii. Si akabeba sinia la samaki hadi kwao na jamaa zangu. Kufika akabisha hodi, mmoja wa jamaa zangu akaenda kufungua mlango. Kugundua aliyepo mlangoni ni mama wa samaki akafunga mlango haraka haraka akijua mama kawaletea noma. Baba yake akauliza kwa nini kafunga mlango ilihali aliyebisha hodi hajaonana na wakubwa (yaani baba ama mama yao jamaa zangu). Akamuliwa afungue mlango mgeni aingie. Mlango ukafunguliwa mama wa samaki na sinia lake kaingia ndani.

Mama wa samaki akaeleza shida yake kuwa kapata taarifa samaki walihitajika wakati yeye akiwa biasharani. baba wa jamaa zangu akaitikia kinafiki ati ni kweli na akawahimiza wanae wanunue wale samaki kwa bashasha na unafiki mkubwa.

Baada ya biashara mama wa samaki huyooo akaondoka zake. Huku nyuma baba wa jamaa zangu akaenda kukata bakora akawahimiza wanae wawatafune wale samaki huku akitaka maelezo pesa ya kununua samaki ilitoka wapi. Jamaa zangu wakawa wazito kula wale samaki. Basi mzee akaanza kuwatembezea bakora kwanza za kuwahimiza kula wale samaki. Jamaa zangu wakawa wanakula wale samaki huku wakilia na wakati huo huo yule baba yao akiwa nje anaanda mzigo wa bakora huku akifoka "leo mtanitambua si nilishawakataza kuwa na pesa leo mtanitambua".

Jamaa zangu huku wakilia wakatafuna wale samaki lakini wakati huo huo mvua za bakora zikiwanyeshea kuwahimiza waongeze kasi ya kula wale samaki.

Aisee baada ya zoezi la kula wale samaki lilipokwisha baba yao aliwashushia bakora za kutosha sana kama adhabu ya kukiuka amri yake ya kutokukutwa na pesa mfukoni.

Ni kituko kilichofanywa na jamaa zangu lakini hunichekesha sana kila nikikikumbuka ama tukumbushanapo pindi nionanapo na mmoja wa hawa jamaa zangu.


Hahahaaaaaaa kwa kweli mkuu hapa nimecheka mpaka kunyanzi zimejaa usoni.. Madingi wakoloni ni noma. Hahahaaaaaaaaaaaaaaaaa kwikwikwiiiiiiiii uuuuhhhhhhiiiiiiii....
 
...nikiwa darasa la pili (mwaka Ninteen Kweusi!), tulikuwa tunatakiwa kwenda shule SAA TANO mchana. Siku hiyo wanafamilia wote walikua wametoka (nilikuwa naishi kwa bibi yangu). Baada ya maandalizi mengine yote sikuweza kuona mafuta ya kupakaa (kupaka?). Ikabidi nipekue ndani ya begi la mama yangu mdogo nikakuta kichupa kidogo cha rangi ya blue/kijani hivi. Nilipofungua nikaona kun amafuta nikapakaa toka kichwani hadi miguuni.

Punde si punde nikaanza kujisikia joto lilichnaganyika na msisimko wa mwili pamoja na harufu nzito. Kwa kuwa nilikuwa nimeshachelewa shule nikatoka vivyo hivyo mbio kwenda shule (kama kilomita moja hivi toka nyumbani). Nilipofika nilikuwa nimesweat kupita kiasi na bado nikisikia joto/msisimko na harufu nisiyoijua. Nilipoingia darasani mwalimu wa somo alikuwa ameshaanza kufundisha. Alipona hali niliyokuwa nayo akanisimamisha akauliza kulikoni? Mimi nikaishia kuomba msamaha kwa kuchelewa kuingia darasani. Akanichukua kunipeleka kwenye bomba la maji la shule kuninawisha-nikaja kuelewa baada ya kumsikia akiongea na walimu wengine kumbe nilikua nimepakaa VICKS KINGO nikidhani ni mafuta ya kupaka!!!


Nadhani ilikuwa "VICKS VAPORUB". But that was really funny. You made my day...!
 
nakumbuka nilipokuwa mdogo nilikuwa napenda sana kuendesha magari. Sasa ma Uncles zangu walikuwa wananifundisha kubalance steering na clutch na mafuta. Sasa basi kila nikiwa na mdingi namuomba kushika stering ananipakata nafurahi.

Siku moja dingi kapaki gari nje na kuna wageni ndani, basi nimekaa sebuleni na wageni nikauona funguo wa gari la dingi. Basi nikasema kiutani mbele ya wageni, baba naenda kuendesha gari. si unajua tena wageni dingi hakurespond chochote, nikajua ni tiki hiyo.
Ilikuwa mishale ya saa moja usiku basi fasta mpaka nje nikaweka funguo hapo najua free ikoje na clutch nikawasha.
Kidogo nikaweka namba moja(gari lilikuwa na gia 4 za mbele na reverse), basi kumbe nadhani nimeweka gia kumbe bado free, nikaachia clutch naona gari haliendi, nikakanyaga mafuta mpaka mwisho.

Nilishtukia nashushwa na nilipigwa kofi hilo ambalo sitalisahau maishani,,, nilisikia zzzzzzzzzzzzzz nikakimbilia chooni wala sikulia

Aloo...! That was really frightening. Nadhani hiyo resi iliyotoka ingemtoa roho dingi.
 
nyumbani palikua na mpera, sikumoja tukapanda juu ya mpera tukiongozwa na kaka yetu, alipofika juu akachagua tawi moja akakaa basi wote tukajitahidi kupanda na kumpandisha mdogo wetu wa mwisho aliekua mdogo sana, alipomalizia kupanda dada yetu akakaa kwenye tawi tu likakatika tukaanguka chini tukaanza kulia, kaka yetu akawa anajitahidi kutunyamazisha ili mama asisikie ila ikashindikana kwa yule mdogo wetu aliyekua analia kwa sauti kubwa, mama yetu alipotoka nje shughuli ilitukuta, hakuna rangi tualiacha ona.
 
Mimi nakumbuka primary nilisoma boarding ila kila jpili tunaruhusiwa kwenda kanisani na kuhakikisha ifikapo saa tisa tuwe eneo la shule, kwangu ilikuwa kawaida siendi kanisani ila naenda kwa shangazi yangu napiga mamisosi mazuri then wakati wa kuaga kuondoka ananisindikiza tukifika kahatua flani namwona ananyoosha mkono nikipokea kanifinyia sh 50 ya noti, sasa hali ikawa imezoeleka hivyo, siku 1 wakati wa kusindikizwa nikaagwa na kupewa mkono wa kwaheri masomo mema, unaambiwa kila ikiupapasa ule mkono sikutani na kitu kigumu nikajua labda kitu hicho kimedondoka unaambiwa nikaangaza sana down hola, kumbe muda wote huo mm nimedata shangazi yangu hana mbavu ikabidi anihurumie pale pole mwanangu leo hamna siku nyingine basi mpaka leo nikikutana nae ndio utani wangu mpaka wanangu wote kawahadithia
 
tulikuwa darasa la 4. wakati huo kingereza hakipandi hata kidogo. kukawa na mwl fulani mwanaume wa kingereza. yeye kila akiingia darasani anauliza what 'do you do?" sisi hatujui jinsi ya kujibu. yeye kwa kutuona hivyo anakasirika na kuchukua 'dasta' na kutupiga nayo vichwani. inauma! ikawa sasa tunamjadili huyu mwl nae kila siku duyudu duyudu. likawa jina lake.

siku moja mwenzetu mmoja akawa nje ya darasa wakati mwl duyudu yuko darasani anafundisha. yule jamaa akaanza kuita kwa dirishani "duyudu eee duyudu ee!" mwl duyudu akasikia. akaanza kunyata taratibu kwenda nje. jamaa kule nje hajui yeye anaita tu duyudu duyudu! kutahamaki kakwidwa chini mbali juu mbali (kiunoni kwa nyuma huku akiinuliwa juu) Jamaa alipata kibano mpaka tulimwonea huruma. haikutosha!

Siku moja kitoto cha darasa la kwanza kikatumwa na mwl mwingine kwenda stafu kumwomba mwl duyudu kitabu cha kingereza cha mwalimu. yule dogo akafika staff ambako kulikuwa na walimu wengine. katoto ka watu innocently kakaanza:

"mwl duyudu, mwl ...kanituma kitabu...!!!"

Hakumaliza! alibamizwa kibao mpaka katoto ka watu kakadondoka sakafuni staff room!!! sijui yuko wapi sasa hivi teacher Duyudu!
 
Mwanangu siku moja akiwa 4 yrs alitoa kali,wakati huo alikuwa anasoma chekechea, yeye alikuwa anapenda sana kuchora.
Siku moja mamake alikuta amechora picha ya mwanamke amebeba ndoo ya maji.wife alipoona ile picha akamsifia kisha akamuuliza ,mwanangu umechora vizuri sana lakini hujachora wowowo la huyu mwanake liko wapi ?
Mwanangu akakubali kweli mama subiri sasa hivi.
Aliporudi akamwonyesha mama yake nyuma ya karatasi alilochora ile picha .mama hakugundua akamuuliza nini umechora huku tena ?
Mtoto ,ni wowowo mama si huwa linakuwa nyuma.
Wife aliponisimulia nilicheka sana.
 
Dah..nilipokuwa mdogo kuna cku housegal we2 2kiwa sebulen na wageni,akajisahau akajamba kwa sauti na kwa kuwa nilikuwa karibu yake akanifokea kwa nguvu "we mtoto mbona unajamba mbele za wa2" mimi nikamjibu "mimi cjajamba,nimekuckia ni wewe" ebwana aliona noma na bdae ucku alinifinya..tehe tehe.
 
Duh noma......nilikuwa na jamaa angu mmoja anaitwa ton,jamaa lilikua jizi sana la vitabu pale shuleni,basi siku moja nikaenda kumwazima kitabu cha history,katika kusomasoma nikakutana maswali ambayo yalinigonga..kwa kutaka umaarufu kwamba nasoma sana ikabidi niende kwa mwalimu wa history kumuuliza yale maswali. Kumbe kile kitabu ni cha yule ticha,jamaa alikiiba toka kwa mwalimu. Ticha kucheki ni kitabu chake, akaniuliza umekipata wapi hiki kitabu nikamwambia kanipa ton,ton kaitwa.........nadhani kilichoendelea mnakifahamu coz jamaa mpaka leo kila akiniona lazima anablame ile ishu........teheteheeeee
 
my favourite brother (RIP)alikuwa mtundu sana,nilikuwa nampenda sana hadi akichapwa nalia. akiwa std 4 nadhani,kama kawa akatoroka kuenda mpirani.kurudi akachapwa na mama (kiboko cha mpera yaani!),afu akaambiwa akaoge.akaingia bafuni hakuoga,akaamua kunya kwenye bathtub,japo choo kipo hapo hapo!manake bifu lilikuwa na dada ambaye ndo anamsemelezea.dada kustukia issue akamsemea.mama akachapa kipigo cha paka mwizi,mi nalia tu!kaka kuachiwa akajifungia chumbani muda mrefu.dingi anaingia kupata ripoti akamuita.kuna mablanket yale sijui yalikuwa kilimanjaro blankets?likichakaa linafumuka nyuzi,yalikuwa yametelekezwa juu ya makabati.kumbe jamaa kajifungia anachana blanket anajifunga kama sanda ya lazaro kwenye sinema za Yesu.ile kutoka chumbani tu baba na mama hawana mbavu,wote wanacheka mi nikabaki puzzled!yaani hadi leo tukikumbushana hiyo incident we wish he was alive tucheke nae.
 
Story za utoto noma, mi nakumbuka nilikuwa mdokozi sana wa vitu kama ndizi mbivu, kulamba sukari na kadhalika.

Ikaja siku moja ikaletwa asali ya dawa kwenye chupa ya double cola (size ya chupa ya fanta) ikaningizwa kwa juu ili kuzuia udokozi, nikafanya mikakati yote ya kuifikia nikashindwa. Nikagundua mbinu ya kupanganisha viti, nikawa nalifungua lile chupa afu nachuovya mti kisha nalamba. Siku ya siku nikakutwa na maza niko juu nalamba kijiti, kucheki chupa inakaribia kuisha, nilipewa kichapo cha haja kisha akanifungia chumbani ili akitoka sokoni anidunde tena. Nilikoma udokozi.
 
nakumbuka darasa la pili nilienda na maparachichi shuleni nikiwa nimeyaweka ndani ya begi la madaftari. Sasa si nikajisahau nikalikalia begi? Kilichofata madaftari yote yakatapakaa maparachichi halaf badala ya wenzang kunisaidia ndio wakawa wanayalamba madaftari
 
my favourite brother (RIP)alikuwa mtundu sana,nilikuwa nampenda sana hadi akichapwa nalia. akiwa std 4 nadhani,kama kawa akatoroka kuenda mpirani.kurudi akachapwa na mama (kiboko cha mpera yaani!),afu akaambiwa akaoge.akaingia bafuni hakuoga,akaamua kunya kwenye bathtub,japo choo kipo hapo hapo!manake bifu lilikuwa na dada ambaye ndo anamsemelezea.dada kustukia issue akamsemea.mama akachapa kipigo cha paka mwizi,mi nalia tu!kaka kuachiwa akajifungia chumbani muda mrefu.dingi anaingia kupata ripoti akamuita.kuna mablanket yale sijui yalikuwa kilimanjaro blankets?likichakaa linafumuka nyuzi,yalikuwa yametelekezwa juu ya makabati.kumbe jamaa kajifungia anachana blanket anajifunga kama sanda ya lazaro kwenye sinema za Yesu.ile kutoka chumbani tu baba na mama hawana mbavu,wote wanacheka mi nikabaki puzzled!yaani hadi leo tukikumbushana hiyo incident we wish he was alive tucheke nae.

Hahahaha wewe mbavu zangu. Inachekesha sana ila pia inasikitisha sana hasa kwa kua kaka yako kesha tangulia mbele za haki (RIP)
 
Hahahaaaaaaa kwa kweli mkuu hapa nimecheka mpaka kunyanzi zimejaa usoni.. Madingi wakoloni ni noma. Hahahaaaaaaaaaaaaaaaaa kwikwikwiiiiiiiii uuuuhhhhhhiiiiiiii....

Mkuu sio mchezo madingi enzi hizo bwana hahahaha. Sio hawa wa siku hizi wanawajaza watoto minoti tu
 
Big up mwanzisha thread! Ila nadhani katabia hako umekaacha...vinginevyo tukuweke kwenye list ya Mwembeyanga.

Kituko changu:

Nikiwa darasa la tatu, nilipewa jukumu la kwenda kuchunga ngome wa kitongoji na ili kuwa inakaribia kuwa Pasaka, siku ambayo ilikuwa ni ya furaha kwetu watoto kwani tulikuwa na uhakika wa kula wali na nyama, kwani baada ya hapo ni mpaka Krismas ndio utapata menu kama hiyo. jukumu hili lilikuwa lina fanyika kwa zamu kwa kila kaya yenyekumiliki mifugo na lilikuwa la siku tatu. Utaratibu ilikuwa unachukua mifugo hiyo asubuhi na kuirudisha saa kumi na mbili jioni. Ukichelewa kurudisha mifugo hiyo kwa muda uliopangwa unarudia jukumu hilo kwa siku nyingie 3. Nilikuwa mpezi wa kusiliza redio, hivyo kila zamu yetu ilipofika mzazi wangu alinuruhusu kwenda na redio machungani. Siku ya kituko ilikuwa hivi, nilichukua mifugo asubuhi kama kawaida huku nikiwa nimebeba pamba (chakula cha kulia machungani) pamoja na redio. Mbuga yenyewe ilikuwa kubwa sana ikiwa na milima na mabonde hivyo baadhi ya vitongoji/vijiji vya jirani vilitumia mbuga hiyo bila kuchanganya mifugo. Basi nikiwa kwenye kilima kimoja wapo ambapo nilikuwa naweza kuona mifugo yote niliamua kukaa kitako na kuanza kushambulia "pamba" yangu huku nikisikiliza redio.Nilikuwa nasikiliza idhaa ya Taifa ya Kenya(KBC). Basi baada ya Kumaliza kulishambulia lipamba langu huku KBC ikiporomosha midundo ya KATITU niliangaza bondeni nikaona mifugo nayo imepumzika maana ilikuwa yapata saa nane za mchana kijua cha mawingu kikiipasha mbuga. Nami niliamua kupumzika kwa kujilaza kwenye mwamba uliokuwa karibu, redio ikiwa karibu nasikio langu. Si mnajua mambo ya shibe na redio inavyobembeleza ni kanzaa kuuchapa usingizi (msiniulize niliota nini)....,Niliposhtuka nilimsikia Leornad Mambo Mbotella wa KBC akisema"... hivi sasa ni saa 11 na robo za jioni..." kuangaza bonde sikuona mifugo wala ndama, bali kwa mbali saana niliona watu kama wanakimbiza ng'ombe. Kilichonijia kichwani ni kuwa ng'ombe wameibwa (kumbuka hapajawahi kutokea wizi wa ng'ombe kijijini kwetu bali katika tarafa nyingine). Basi nilikimbia kurudi nyumbani, mwendo kama wa saa nzima...nilipofika nyumbani na mueleleza mzazi wangu....ninachokumbuka alisema" wameamukuja na huku kisa nyama ya Pasaka...". Wanakitongoji walijikusanya kwa ajili ya kwenda kukomboa mifugo...mimi sikuambatana nao kwani nilikuwa mdogo...Tuliambiwa walipofika huko mbugani walikuta baadhi ya ng'ombe wanarudi nyumbani wengine wako bondeni wengine waliwakuta kwenye msitu uliokuwa mbali kweli kweli...Mifugo yote ilirudishwa kijijini yapata saa saba usiku. Wanakitongoji hao walishidwa kuafikiana kama kweli kulikuwa na wezi wa mifugo au mchugaji alishindwa kuchunga mifugo kwa uangalifu....mwisho wa yote kaya yetu haikupewa adhabu ya kurudia jukumu la kuchunga.
 
mimi nakumbuka nilchukuliwa na aunt yangu kwa lengo la kunisomesha maana familia yangu ilkua duni walkua matajiri sana lakini baada ya kuhamia kwake cha moto nilikiona maana nilkua house girl wa familia......... nilkua nawapikia watoto wake japo walkua wakubwa kwangu, nawafulia, nafanya usafi nyumba kubwa ya kifahari ikifika saa ya kuosha vyombo napanda juu ya kiti ili nifkie sink maana nlkua mdogo sana ikifika saa ya kula niko hoi hata kula siwezi nasinzia tuuu.....................................

jamani sitamani kuwa mtoto hata kidogo


pole mama D, hiki sio joke, ni stori half ni ya kweli na inahudhunisha.
mshukuru mungui hata hivyo, ulipata challange zilizokujenga na leo naamini ni mama mwema kwa D.
 
Me sikumbki nilikua na umri gani, ila nakumbuka ilikua mida ya chakula cha usiku.
watu tupo mezani, kwa kawaida tulikua tunasali kwa ajili ya kila kitu na hata msosi wenyewe,.
sikua nimewahi kusali kabla, siku hyo mama akaniteua nisali "tasia leo utaomba, haya fungeni macho".alisema.
wote wakafunga macho, nikawaza jinsi nitakavyo anza kumwomba au kumshukuru mungu kabla ya kumsalim,
nikaona haiwezekani, ikabidi nimsalim kwanza mungu. "shkamoo Mungu" basi wooote wakaangua kicheko na sala nikakatisha.
maza aliponiuliza nikajib "sasa mama m nitaanzaje kuongea na mungu bila kumsalim"??
 
my favourite brother (RIP)alikuwa mtundu sana,nilikuwa nampenda sana hadi akichapwa nalia. akiwa std 4 nadhani,kama kawa akatoroka kuenda mpirani.kurudi akachapwa na mama (kiboko cha mpera yaani!),afu akaambiwa akaoge.akaingia bafuni hakuoga,akaamua kunya kwenye bathtub,japo choo kipo hapo hapo!manake bifu lilikuwa na dada ambaye ndo anamsemelezea.dada kustukia issue akamsemea.mama akachapa kipigo cha paka mwizi,mi nalia tu!kaka kuachiwa akajifungia chumbani muda mrefu.dingi anaingia kupata ripoti akamuita.kuna mablanket yale sijui yalikuwa kilimanjaro blankets?likichakaa linafumuka nyuzi,yalikuwa yametelekezwa juu ya makabati.kumbe jamaa kajifungia anachana blanket anajifunga kama sanda ya lazaro kwenye sinema za Yesu.ile kutoka chumbani tu baba na mama hawana mbavu,wote wanacheka mi nikabaki puzzled!yaani hadi leo tukikumbushana hiyo incident we wish he was alive tucheke nae.

Ahahahaha..pole sana mkuu
 
Me sikumbki nilikua na umri gani, ila nakumbuka ilikua mida ya chakula cha usiku.
watu tupo mezani, kwa kawaida tulikua tunasali kwa ajili ya kila kitu na hata msosi wenyewe,.
sikua nimewahi kusali kabla, siku hyo mama akaniteua nisali "tasia leo utaomba, haya fungeni macho".alisema.
wote wakafunga macho, nikawaza jinsi nitakavyo anza kumwomba au kumshukuru mungu kabla ya kumsalim,
nikaona haiwezekani, ikabidi nimsalim kwanza mungu. "shkamoo Mungu" basi wooote wakaangua kicheko na sala nikakatisha.
maza aliponiuliza nikajib "sasa mama m nitaanzaje kuongea na mungu bila kumsalim"??
he he he heeeeh!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom