Hivi kinachoitwa MFUMO ni kitu gani?

Hivi kinachoitwa MFUMO ni kitu gani?

Hapa ndo najua hii nchi kwa nn ipo hivi hadi leo. Mkuu Lowassa akishinda anakuwa Rais wa nchi,akina mbowe watakuwa chini yake,yaani unachosema hapa lowassa akishinda waanze kumuomba abadili mfumo uliopo si ndicho unachomaanisha!!?? Akikataa mawazo yao itakuwaje na anauwezo hata kuwaacha kwenye baraza lake la mawaziri. Watafanya nini akina mbowe na wenzie wa ukawa?? Watarudi kwetu tena kutuambia huyu jamaa hafai?? Mimi ningewaelewa km lowassa angekuja chadema kuongeza nguvu tu lkn asigombee urais. Huo unaouita mfumo haujisimamii wenyewe,unasimamiwa na watu. Hao watu ndo hao hao wanatumia kila aina ya ujanja waendelee kuukumbatia. Amini usiamini lowassa akija kuwageuka chadema,chadema ndo itakuwa imezikwa haitaaminika tena!

Tatizo lako ni lile lile la Watanzania wengi tumeaminishwa kumwabudu mtu(RAIS) badala ya kuabudu sheria. Rais ni mtu tu kama wewe na huyupo juu ya sheria.

cdm/ukawa tutatengeneza sheria/katiba (na ndo mfumo wenyewe huo) ambao hata Rais atapaswa kuufuata na kuwa chini yake. Rais kupitia CDM hatokuwa mwenyekiti wa Chama nk nk. Tunataka mifumo iwekwe imuongoze rais jinsi ya kuenenda na si Rais arundikiwe madaraka ya kuamua tu kutenda kadri anavopenda. Unless utuambie ni wapi na lini Lowassa kasema akiwa Rais kupitia CDM hatobadilisha mifumo ya sasa ikiwemo Katiba ya Nchi?

na zaid sana ujue Rais si mtu, Rais ni taasisi, rais hatawali peke yake bali anatawala na wenzake.

acha uzuzu uliaminishwa kuwa Rais ni Mungu. Rais ni mtu muhimu katika nchi lakini Rais si kila kitu. Katiba ya nchi ndiyo (ndiyo inayopaswa kuwa) kila kitu, sheria za nchi ndo kila kitu. Tunatakiwa tuabudu KATIBA YA NCHI si Rais, Rais anakuja na kupita na anaweza kutoka udp, tlp, cuf, cdm, nccr nk nk lakini katiba ya nchi inasimama, na ukitaka kuibadilisha ni mbinde.
 
usiishi kwa hofu ya kukaririshwa mkuu. Lowasa ndio mpango kwa na ndiyo dawa ya kuiondoa CCM na mfumo mzima wa kifisadi.
 
magode

utajua tu tukishachukua nchi na kuusambaratisha tu oct 25 kwani hakuna namna nyingine ya kuujua
 
Last edited by a moderator:
Mada nzuri Sana. Naamini Dr Slaa ni mzuri zaidi ya Lowassa. Ni kweli Lowassa ana mtaji wa watu lakini kutuaminisha kwamba Lowassa ni presidential material bado.
 
magode

utajua tu tukishachukua nchi na kuusambaratisha tu oct 25 kwani hakuna namna nyingine ya kuujua
Me sina neno mkuu wangu mgt software lkn jitahidini kuweka akiba ya maneno. Nna hofu huenda huu ni mpango uliosukwa kuibomoa chadema!!
 
Last edited by a moderator:
Hivi Tanzania hapa hapa kuna watu wanajua kutumia computer ama smart phone lakini hawajui mfumo ni nini? duh hakyanani nchi ina mapimbi hii ..halafu wanajidai wanajua kila kitu dah
Thread km hii kwa watu wa kiwango chako cha kufikiri,ni vigumu sana kutoa maoni hapa. Ungesoma tu kisha ukaendelea na post zenye kiwango chako. Siyo lazima uchangie kila uzi..! Wenzako wote wamepita kimya kimya tu.
 
Mimi nijuavyo mfumo ni muunganiko wa wavitu watu kundi au makundi madogo madogo kwa kingereza mfumo ni systeme that combines several organ to perform the same work kwahiyo mfumo unao ongelewa kwa fikra zangu ni muunganiko wa watawala kutoka chama cha mapinduzi kikijumuisha Sera na taratibu za chama zinazofuatwa katika ngazi zote kuanzia chini hadi juu
 
Mimi nijuavyo mfumo ni muunganiko wa wavitu watu kundi au makundi madogo madogo kwa kingereza mfumo ni systeme that combines several organ to perform the same work kwahiyo mfumo unao ongelewa kwa fikra zangu ni muunganiko wa watawala kutoka chama cha mapinduzi kikijumuisha Sera na taratibu za chama zinazofuatwa katika ngazi zote kuanzia chini hadi juu
Hilo kundi likihama kwa pamoja kwenda chama kingine,na likapewa mamlaka huko litakakoelekea huo mfumo utakuwa umekufa!!?
 
Actions speak louder than words. Mkapa alibatizwa Mr. Clean alipotumbuKia CCM akawa fisadi wa mgodi wa Kiwira.
Tibaijuka alitoka UN akiwa msafi mweupe mpaka akasifiwa na kila mtu alipotumbukia ccm akatoka ibilisi. Tafakari
 
Unakosea sana pale unapomlaumu CAG,katiba tuliyonayo ambayo ndio inamuweka CAG in power via the president,haimpi mandate ya kuwajibisha culprits, that's why utaskia wanasem CAG anafanya kazi nzuri but hana meno. Chamsingi kubadili mfumo tulionao ambao hautaki kumpatia meno CAG via katiba mpya, then tuone effect us CAG moja kwa moja.. Kwakua katiba iliyopo sec 45.inamtaka CAG akishafanya uchunguzi wake aripoti kwa aliyemteua (Rais),hapo unategemea nini?
Tuutoe mfumo ndo tuurekebishe then tuurudishe kazini
Hakuna mahala nilipomlaumu CAG nilichosema katika post zilizofuatia baada ya hiyo uliyo hii quote kuna vitu vingi sana CAG wanakuja navyo baada ya ukaguzi wao na mapendekezo mengi sana katika kazi zao na hakuna kinachofanywa zaidi ya kupiga makelele ya siku moja mbili bungeni na pengine kubadili viongozi wa sehemu lakini hakuna hatua za kubadilisha the sectorial procedures kama walivyotaka wao.

Achilia mbali ufisadi bali pia jinsi mamlaka kama TPDC ilivyojiamulia kujipandishia mishahara yao, au bandari? walichofanya ni kubadili wakurugunezi wa sehemu lakini je kuna restriction zilizowekwa kuhakikisha makosa ayajirudii tena kuna oversight ya kuwadhibiti hawa watu kwenye public sector to ensure a universal approach on public procurement or expenditure, tayari kuna sheria nani msimamizi wa sheria ya 'Public Procurement act 2011' on full time basis mimi sijasikia this is why watu wanaenda nunua mabehewa ya second hand halafu tutegemee whistle blower kisa mamlaka kaachiwa katibu mkuu wa wizara ya fedha fisadi mwingine tu if you ask me. Huyo Mwakyembe aliekuwa wizara husika katolewa huko kapewa wizara nyingine sio awekwe benchi ata kama ausiki na ufisadi simply a matter of kutokuwa na uwezo kabisa unaona matatizo yenyewe yalipo hakuna accountability kabisa ukiaribu huku unapelekwa kule.

Isitoshe CAG anakuja na vitu vingi sana it is common sense pale kwenye ubadhirifu akapewa mamlaka ya kushitaki hilo wala sina ubishi nalo nakubaliana na wewe na wengi wamesema pia. Swala lenyewe wala alihitaji kubadili katiba au hata kupata baraka za bunge this is just a matter of delegated/secondary legislation kutoka mamlaka husika kwa sababu CAG ipo kisheria tayari hakuna sababu ya kurudi bungeni kama lengo ni kuongeza ufanisi wa kitengo kuwapa hayo mamlaka ya kushitaki, tatizo lenyewe hela za kuweza kufanya hivyo na procedure za mahakama zinazochukua muda mrefu inaweza kuwa tatizo yale yale mfumo mbovu.

Kwa sasa ndio kwanza CAG kapunguziwa budget yake, je umesikia maelezo ya Saada Mkuya how is their new budget suppose to allow them to do the same work efficiently na jinsi CAG anavyotakiwa ku-organize their same mission under the new reduced funds, what reasons were behind the cuts.

Ndio tunarudi pale pale viongozi wenyewe nao ovyo pia nani anawateuwa raisi sifa gani anaangalia wanajua yeye na huyo Rajabu Luhavi wake. Mfumo unakasoro katika sehemu nyingi by the way tunapozungumzia mfumo wa serikari una levels nyingi.
 
ufisadi ni zao la mfumo.

tunapozungumzia mfumo tuna maanisha sheria za nchi zinazo endesha masuala ya nchi husika na kwa msingi huu, kinacho itwa mfumo katika taifa ni katiba na sheria zake,
sasa katiba ya nchi hii ambayo ndio bustani na ardhi yenye rutuba kwa ajili ya mafisadi, na iliyo kuza mfumo wa chama dola, ndio tatizo la nchi hii. kwa mfano rais wa nchi hii akifanya kosa la jinai au vinginevyo akiwa ndani ya madaraka au nje ya madaraka, hatoshtakiwa kwa kosa lolote kwasababu katiba inampa kinga, maana yake ni kwamba hata rais akila rushwa hakuna atake muwajibisha kikatiba, lkn pia mtumishi yeyote yule haswa hawa wakubwa wa serikali ni waajiliwa wa rais na kisheria zetu hapa bongo, rais pekee ndio mwenye mamlaka ya kumuadhibu huyo mtumishi wa umma, na kibaya zaidi atafanya kwa utashi wake tu, kwahiyo akiona haifai kumuadhibu kama alivyofanya kwa muongo, jairo, mkapa na kiwira na epa na mengine mengi, jinsi alivyo sita kuwawajibisha japo ilidhiilika wazi kuwa wahusika walikuwa na makosa, hiki ndicho kinachoitwa mfumo mbovu wa utawala yaani katiba ya nchi hii na sheria zake zinalinda na kutengeneza mazingira mazuri ya ufisadi, na ndio maana ccm walipinga katiba ya warioba iliyo taka mikataba iwekwe wazi, wabunge wawajibishwe, na maadili ya viongozi, kwasababu uhai wa ccm unategemea uhai wa mfumo huu wa utawala ambao nao hutegea rushwa
ndio maana ili kuupinga mfumo huu ni lazima uwaondoe wote wanao ulinda mfumo huu nao ni ccm na si mtu mmoja
:teeth:
 
japo umejichangachanganya lakini kimsingi umeeleza vizuri sana maana ya mfumo.

kifupi hapo kwenye red huo ndo mfumo lakini ni mfumo daraja la pili kwa maana ya kuwa zao la mfumo daraja la kwanza, mfumo mama, ambao ni KATIBA ya nchi.

mfumo huo kwenye red unawekwe/ unaundwa/ unatengenezwa na mfumo mkuu ambao ni katiba. Katiba ndo inayotakiwa iseme serikali(executive) iweje, ifanye kazi zipi kwa namna gani, kwa mamlaka yepi, iwajibishwe vipi nk nk, vivyo hivyo kwa Bunge(legislature) na Mahakama (Judiciary). Ukiwa na Katiba mbovu, Mfano katiba ambayo inaipa serikali(executive/Rais) nguvu za kupitiliza mfano Rais kuwa na uwezo wa kuteua na ku fire the executive almost yote, tena wakati mwingine at will tu bila kufuata sheria, Rais kuteua Judiciary, Rais kuteua sehemu ya Legislature na yeye mwenyewe kuwa sehemu ya legilsature ndo haya unayoyaona ya watu kuiba (kosa la jinai) badala ya kushtakiwa wanaambiwa tu warudishe walichoiba na mambo yanaisha.

Katiba YA nchi ndo ama itasema, au itaweka msingi wa kutengeneza subdelegation itakoyoelekeza huyo CAG ateuliwe vip, afanye kazi zake kivip aripot kwa nan nk. Kama CAG kazi yake ni kufuatilia utendaji wa serikal utategemea vip atende vema ikiwa serikali hiyo anayoikagua ndo hiyo hiyo inayomteua, inamlipa na ndo ina mamlaka ya kumfukuza kwa kadri itakavoona inafaa?! Tungetegemea mfumo mama (Katiba) mathalan uielekeze kwamba CAG ateuliwe na executive(Rais) lakini uteuzi wake uwe approved na legislature na ikibidi kumfukuza au kumbadilisha au kubadilisha maslahi yake kwa namna yoyote ile basi isifanyike bila idhini ya bunge, na aripoti kwa bunge na si kwa rais ambaye naye anaweza kuwa mtuhumiwa

tunataka mfumo ambao wananchi ndo wenye mamlaka ya mwisho na si mtu mmoja tu kama Rais(executive) ndo analundikiwa mammlaka yote ya nchi. Katika hali kama hii ya sasa siku tukipata Rais mwendawazimu tutapona kweli??!!
Nimeshakwambia katiba ni mkataba (mwongozo wa jinsi nchi itakavyo endeshwa na imegawanywa katika sehemu zake) wewe unachoongelea preambles za katika huo sio mfumo ni maelezo tu ya institution of the government; lakini hata hiyo katiba aiko static ina maana inaweza fanyiwa amendments kuongezea vitu au kubadilisha vitu iwapo unaona mamlaka fulani yana nguvu sana na yanachangia kuleta uzembe kwa teuzi zake serikari na chanzo chake katiba.

Mfumo ni kitu kingine kabisa it is a mechanism which encompasses ways of managing activities kufikia malengo, human resource managment, planning and operations za serikari, expectations za serikari katika maazimio yake, project management, supervisions, ethics, etc.

Kwa hivyo katiba inakuwa kama mwongozo wa kuhakikisha haya yote yanafanyika chini ya maelezo yake mfano kunaweza kuwa na sheria za kuhakikisha sector fulani isimamiwe hivi kama ya gesi na mafuta hayo ndio mambo ya serikari katika kufikia malengo yake na taratibu sahihi za kufanya mambo ambapo bunge linatakiwa kuridhia au labda sheria za manunuzi, sijui wafanyakazi wa umma etc. Yote hayo ni kwenye kufanikisha au kuboresha mfumo wa kufanya shughuli zao na haya yanaweza weka na serikari ya chama chochote muhimu yasiwe nje ya mipaka ya katiba.

Wakisema mipaka ya katiba ina maana kama katiba katika haki za binadamu inasema watu wote sawa, wewe kwenye sheria yako ukasema wanawake au vijana wasiovuka umri fulani awataruhusiwa kushika nyadhifa au sijui kufanya kitu fulani hilo swala na hiyo sheria inaweza kuwa challenged mahakamani kuwa kinyume na katiba.

Lakini kuweka kanuni za mfumo sehemu na jinsi ya kuboresha mfumo wa ufanyaji mambo sio issue ya katiba sijui kama unanielewa. Kwa hivyo kuunda chombo kama cha CAG uitaji katiba ni sheria tu ya kawaida serikari inaweza tunga au ikafanyia amendments sheria iliyopo kuhusu sector katika kuongeza ufanisi.
 
Mfumo = ni mkusanyiko wa vipengele mbali mbali vinavyotengeneza kitu kimoja.

Kama hvyo ndivyo then ni wazi kwamba mfumo ambao umeunganishwa na vipengele vingi sana ni vigumu kuuvunja.

Therefore, CCM kama chama tawala ndo zao la vipengele vingi vingi vingiiii vilivyojiunga na kusimama kwa zaidi ya miaka HAMSINI. U can imagine a system has deepened its roots to NATION'S soil for 50 yrs.!

Sasa , mfumo huu haung'ooki au tingishwa kirahisi ila tu kwa zile elements zilizouunganisha kuanza legea.

Sasa LOWASA hapa ni bolti ya kwanza tu kulegea.. Hahaha! Polen UKAWA.

Bado mna safari ndefu.
 
Yes..! Na CCM hawastahili kupaniki.
CHADEMA HAS A WEAKENED SYSTEM.
 
Mimi sirudii majibu watu wameshayatoa hapo juu,ila mimi nauliza tu kwani Lowassa ni fisadi ???????? kama ni fisadi kwanini hajashitakiwa hadi katoka ccm???????

Hili swali kamuulize Dr Slaa, Mbowe, Msigwa, Mnyika, Lissu na Lema
 
Tatizo lako ni lile lile la Watanzania wengi tumeaminishwa kumwabudu mtu(RAIS) badala ya kuabudu sheria. Rais ni mtu tu kama wewe na huyupo juu ya sheria.

cdm/ukawa tutatengeneza sheria/katiba (na ndo mfumo wenyewe huo) ambao hata Rais atapaswa kuufuata na kuwa chini yake. Rais kupitia CDM hatokuwa mwenyekiti wa Chama nk nk. Tunataka mifumo iwekwe imuongoze rais jinsi ya kuenenda na si Rais arundikiwe madaraka ya kuamua tu kutenda kadri anavopenda. Unless utuambie ni wapi na lini Lowassa kasema akiwa Rais kupitia CDM hatobadilisha mifumo ya sasa ikiwemo Katiba ya Nchi?

na zaid sana ujue Rais si mtu, Rais ni taasisi, rais hatawali peke yake bali anatawala na wenzake.

acha uzuzu uliaminishwa kuwa Rais ni Mungu. Rais ni mtu muhimu katika nchi lakini Rais si kila kitu. Katiba ya nchi ndiyo (ndiyo inayopaswa kuwa) kila kitu, sheria za nchi ndo kila kitu. Tunatakiwa tuabudu KATIBA YA NCHI si Rais, Rais anakuja na kupita na anaweza kutoka udp, tlp, cuf, cdm, nccr nk nk lakini katiba ya nchi inasimama, na ukitaka kuibadilisha ni mbinde.

Acha ndoto wewe katiba haiandikwi ovyovyo na kirahisi kama cdm ilivyonunuliwa, kakojoe ulale maana mshauzwa.
 
Nimeshakwambia katiba ni mkataba (mwongozo wa jinsi nchi itakavyo endeshwa na imegawanywa katika sehemu zake) wewe unachoongelea preambles za katika huo sio mfumo ni maelezo tu ya institution of the government; lakini hata hiyo katiba aiko static ina maana inaweza fanyiwa amendments kuongezea vitu au kubadilisha vitu iwapo unaona mamlaka fulani yana nguvu sana na yanachangia kuleta uzembe kwa teuzi zake serikari na chanzo chake katiba.

Mfumo ni kitu kingine kabisa it is a mechanism which encompasses ways of managing activities kufikia malengo, human resource managment, planning and operations za serikari, expectations za serikari katika maazimio yake, project management, supervisions, ethics, etc.

Kwa hivyo katiba inakuwa kama mwongozo wa kuhakikisha haya yote yanafanyika chini ya maelezo yake mfano kunaweza kuwa na sheria za kuhakikisha sector fulani isimamiwe hivi kama ya gesi na mafuta hayo ndio mambo ya serikari katika kufikia malengo yake na taratibu sahihi za kufanya mambo ambapo bunge linatakiwa kuridhia au labda sheria za manunuzi, sijui wafanyakazi wa umma etc. Yote hayo ni kwenye kufanikisha au kuboresha mfumo wa kufanya shughuli zao na haya yanaweza weka na serikari ya chama chochote muhimu yasiwe nje ya mipaka ya katiba.

Wakisema mipaka ya katiba ina maana kama katiba katika haki za binadamu inasema watu wote sawa, wewe kwenye sheria yako ukasema wanawake au vijana wasiovuka umri fulani awataruhusiwa kushika nyadhifa au sijui kufanya kitu fulani hilo swala na hiyo sheria inaweza kuwa challenged mahakamani kuwa kinyume na katiba.

Lakini kuweka kanuni za mfumo sehemu na jinsi ya kuboresha mfumo wa ufanyaji mambo sio issue ya katiba sijui kama unanielewa. Kwa hivyo kuunda chombo kama cha CAG uitaji katiba ni sheria tu ya kawaida serikari inaweza tunga au ikafanyia amendments sheria iliyopo kuhusu sector katika kuongeza ufanisi.
Kimsingi tunaongelea jambo moja, na tunakubaliana, ila tofauti yetu ni kitu kidogo sana. Kuna jambo ndogo tu hutaki kulielewa.

well. nikuulize kitu, hapo kwenye red, je unaweza kuweka kanuni ya kuongoza chochote kile katika nchi bila kuwa na katiba kwanza? Jibu hapa ni hapana, kwa sababu, kabla hujatengeneza kanuni au mwongozo mwingine wowote ule (iwe sera, sheria, kanuni, utaratibu, waraka nk nk) lazima kwanza ujue/ufanye reference ya Kanuni/sheria/mwongozo mama (yaani katiba) ili ujue kwanza katiba inasemaje juu ya hiyo sub kanuni unayotaka kutunga. Sababu ya kufanya hiyo reference ni kwamba, na kama ulivyosema wewe mwenyewe, haitakiwi itungwe kanuni, sera, sheria, mwongozo, au utoe waraka wowote ambao unapingana na katiba la sivyo kanuni hiyo itakuwa ni illigal. vivyo hivyo na mifumo inatengenezwa na sheria sera kanuni (ambazo zinatokana na/au sharti zilandane na katiba ya nchi) na ambazo zinaboreshwa siku hadi siku ili kuifanya mifumo ufanye kazi vema zaid na zaid. Ndo maana ulikuwa unaona watu wenye akili kama cdm na ukawa walikuwa wanahoji uwepo kwanza wa mifumo ( sera, sheria, kanuni nk) ya uendashaji wa biashara ya gesi kabla gesi haijaanza kuchimbwa na kabla mikataba haijaanza kuingiwa. Lakini ninyi ccm, kama kawaida yenu, mlikuwa mnakimbilia tu kuchimba gesi kabla hata ya kutengeza hiyo mifumo ya kusimamia hiyo kazi. Anyway, ni uzuzu fulani ambao tunataka sasa kushirikiana na Lowassa kuundoa.

Kwa hiyo, kimsingi, Sipingani na maelezo yako ila nachokuelewesha ni kuwa katiba ndo kanuni ya kwanza kabla ya kanuni nyingine zote, ndo sheria, sera, mwongozo wa kwanza unaozaaa miongozo mingine yote hence mifumo yote ya uendeshaji nchi
 
Acha ndoto wewe katiba haiandikwi ovyovyo na kirahisi kama cdm ilivyonunuliwa, kakojoe ulale maana mshauzwa.
ahahahaahaah, mmeliwa mwaka huu, mmeshaingizwa mjini na watoto wa mjini kina mbowe.
 
ufisadi ni zao la mfumo.

tunapozungumzia mfumo tuna maanisha sheria za nchi zinazo endesha masuala ya nchi husika na kwa msingi huu, kinacho itwa mfumo katika taifa ni katiba na sheria zake,
sasa katiba ya nchi hii ambayo ndio bustani na ardhi yenye rutuba kwa ajili ya mafisadi, na iliyo kuza mfumo wa chama dola, ndio tatizo la nchi hii. kwa mfano rais wa nchi hii akifanya kosa la jinai au vinginevyo akiwa ndani ya madaraka au nje ya madaraka, hatoshtakiwa kwa kosa lolote kwasababu katiba inampa kinga, maana yake ni kwamba hata rais akila rushwa hakuna atake muwajibisha kikatiba, lkn pia mtumishi yeyote yule haswa hawa wakubwa wa serikali ni waajiliwa wa rais na kisheria zetu hapa bongo, rais pekee ndio mwenye mamlaka ya kumuadhibu huyo mtumishi wa umma, na kibaya zaidi atafanya kwa utashi wake tu, kwahiyo akiona haifai kumuadhibu kama alivyofanya kwa muongo, jairo, mkapa na kiwira na epa na mengine mengi, jinsi alivyo sita kuwawajibisha japo ilidhiilika wazi kuwa wahusika walikuwa na makosa, hiki ndicho kinachoitwa mfumo mbovu wa utawala yaani katiba ya nchi hii na sheria zake zinalinda na kutengeneza mazingira mazuri ya ufisadi, na ndio maana ccm walipinga katiba ya warioba iliyo taka mikataba iwekwe wazi, wabunge wawajibishwe, na maadili ya viongozi, kwasababu uhai wa ccm unategemea uhai wa mfumo huu wa utawala ambao nao hutegea rushwa
ndio maana ili kuupinga mfumo huu ni lazima uwaondoe wote wanao ulinda mfumo huu nao ni ccm na si mtu mmoja
:teeth:
hii katiba au mfumo huu haukuweko huko nyuma kipindi cha mwalimu?au katiba imebadilika?ufisadi ni wizi tu?wanasiasa waache kuhadaa watu,ccm haina sera ya ufisadi ila viongozi ndiyo mafisadi na wezi,nyerere mwenyewe alikuwa mwizi.
 
Back
Top Bottom