. wee huelewi maana ya mifumo ya nchi. hivi hapa unavoviongelea ni vitawi tu vya miti mikubwa ya mifumo ya nchi. huyo CAG anachaguliwa kupitia mifumo gani? ipo sahihi? nani anamteua CAG na anamteua kwa sheria ipi? hiyo sheria imeundwa chini ya sheria mama(Katiba) ya aina gani? katiba ya nchi ndo baba na mama wa matawi mengine yote ya mifumo ya nchi. Je Katiba ya sasa inayotetewa na ccm ipo kwa maslah mapana ya nchi au kikundi kidogo cha ccm?
hiyo NHC unaongelea ipo kwa sheria ipi na sheria hiyo inatokana na katiba ya aina gani?
Mfumo wa ccm unamfanya Rais, badala ya katiba ya nchi, kuwa Mungu mtu wa kuteua kila mtu, kuunda na kuvunja kila Taasisi ya Umma nk nk. Mfumo ni dhaifu kuanzia juu, ni mfumo wa kulindana na hata wizi, na ufisadi, wa ccm si wa mtu mmoja mmoja bali ni wa kimfumo na ndo maana wao wenyewe kwa wenywe hawakamatani. Mwizi hawezi kumkamata mwizi mwenziye. wanalindana na ikibidi mwizi anamua mwizi mwenziwe ili kupoteza ushahidi..rejea ya stakishari jamaa wa pikipiki ilivokataa kuwaka wezi wenziwe walimfanyaje?
wewe na mimi hatujui hata alikozikwa Balali ni wapi, au wewe unajua?
Nadhani unachanganya mambo Katiba sio mfumo bali ni mkataba wa mamlaka ya serikari na wananchi unaoelezea mipaka ya serikari na jinsi nchi itavyo endeshwa ikifafanua limitations za powers za serikari, uhusiano wa mamlaka za serikari katika kutekeleza azima ya uongozi na kusimamia, mgawanyo wa majukumu na haki za wananchi katika nchi husika.
Namna gani chama tawala inasimamia hizo administration za serikari katika kufikia malengo ya kisera, bunge linavyosimamia serikari na mahakama pamoja na taasisi zake zingine za kisheria zinavyolinda sheria za nchi na kuakikisha kila kitu kinafanyika ndani ya mipaka ya katiba na sheria za bunge ndio mfumo.
Kwa hivyo mfumo umegawanyika katika sehemu tatu kuu serikari kuu (taasisi ya raisi na baraza lake la mawaziri pamoja na vyombo vinavyosadia kusimamia uendeshawaji wa shuhuli za serikari kwa na namna ya watchdogs kama ewura, CAG, TBS, etc pamoja na idara za serikari zilizoko chini ya mamlaka ya wizara), pili bunge linalo isimamia serikari pamoja na kuleta hoja za wananchi bungeni kuhusu mahitaji yao, kutunga sheria za nchi na kusimamia maslahi ya wananchi na accountability ya serikari i.e mawaziri, watchdogs and idara za serikari azifanyi mambo kiholela, tatu judiciary ie mahakama na vyombo vya sheria kama polisi, takukuru etc, ambavyo vipo kuakikisha vitu vinafanywa kisheria na sheria zenyewe azipo kinyume na mkataba wa wananchi na serikari (katiba) to ensure checks. Hayo ni kwa ufupi lakini kuna mambo mengi sana katika kila mhimili unaovyanya kazi zake kuakikisha efficiency zinapatikana ikiwemo maadili ya watumishi, sheria za sehemu na upeo wa wasimamizi wenyewe.
Kwa hivyo mfumo mmbovu unatokana na mambo mengi sana na unaweza kosolewa na chombo chochote cha usimamizi CAG katika shughuli zake anaweza kosoa udhaifu wa usimamizi wa mapato na akatoa sababu zake, bunge linaweza kosoa mfumo wa wizara fulani kwenye mechanism za kutekeleza sera na kuonyesha upotefu wa mapato, hiyo sera isivyo wafikia kundi fulani au kupitia kamati zake inaweza kuona mfumo wa tender unaoleta ufisadi, conflict of interest, mahakama zinavyochelewa kutoa haki au adhabu kwa wakosaji etc.
Mahakama nayo inaweza ona sheria fulani za nchi sio sahihi kikatiba, sehemu zake zingine zinaweza kuwa poorly funded kama polisi walivyo katika kuhakikisha wezi wanapelekwa sehemu husika na usimamizi imara wa sheria za nchi, wezi serikarini awalindwi etc.
Mwenye jukumu la mengi ya yote hayo ni chama tawala kwa sababu wao ndio wasimamizi wakuu na wenye mamlaka ya kuakikisha kila kitu kipo katikaa ubora wake na kila taasisi ina deliver accordingly as stated by their function, sasa kama CAG kutokana na mamlaka yake akisema sehemu fulani nimekutana na hiki na bado hakuna maamuzi the bulk stop with the responsible authorities to change things inaweza kuwa kubadilisha sheria, waziri, mkurugenzi wa shirika, namna bora ya usimamizi or even more investment depending on the nature of the highlighted problem.