Hivi hii ya Mgawo wa Umeme kuendelea hadi June 2024 nimeisikia mahala jana peke yangu tu au?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,638
109,002
Rais Samia alituambia kwa uhakika kuwa hadi Mwezi ujao Machi Mgawo hautokuwepo tena na TANESCO nao wakasema hadi Mwezi huu wa Februari kutakuwa hakuna tena Mgawo wa Umeme na hatimaye jana nimesikia ( labda niwe nimesikia vibaya ) kuwa sasa Mgawo wa Umeme tutaenda nao na utaisha Mwezi June,. 2024.

Taifa lenye Watu Werevu na Wanaojitambua na Baba wa Mapinduzi duniani la Ufaransa ( France ) mwaka 1789 Raia ( Wananchi wa nchi hiyo ) walifanya Mapinduzi makubwa yaliyoibadili Ufaransa na kuleta Adabu kwa Watawala wa Taifa baada ya Bei ya Mikate iliyokuwa ikiliwa na Watu wengi wa Kawaida ( Masikini ) kama GENTAMYCINE huku kwa Dharau Kubwa Mke wa aliyekuwa Mfalme ( Kiongozi ) wa Ufaransa King Louis XV1 aitwae Marie Antoinette akiwaambia Wafaransa kwa Kejeli kuwa kama wanaona Bei ya Mkate ni Kubwa basi wanunue / wale Keki ambayo ni ya Gharama Kubwa na wanaomudu kula Keki ni Matajiri pekee.

Taifa lenye Watu ( Raia ) wa hovyo hovyo ( Going Goi ) popote pale duniani ( Tanzania haimo kwani ina Watu Werevu na Rais Mchapakazi kuliko wote duniani ) hata wakiwa wanakatiwa Umeme, bei ya Sukari kuwa juu, Maji yakiwa ni ya Mgawo,. Mfumuko wa bei kuwa juu, Elimu yao kuwa Duni na wanatumia Siku Tatu, Tano hadi hata Saba za Kumsifu na Kumuombea Fisadi Mfalme na Mafia kamwe usitegemee likawa na Maendeleo sana sana Taifa hilo kila Siku tu litakuwa linaongeza Wajinga na Wapumbavu.

Natamani sana kumjua ni Rais gani wa Afrika ( sasa Mstaafu aliyekuwa na Sifa ya kutokuwa na Akili ila aliyekuwa na Sifa ya Usanii ) kwa Dharau kabisa aliambiwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame 'Genius, Military and Intelligence Expert' kuwa ANAONGOZA MAITI ndiyo maana WANAWAFANYA watakavyo.
 
South Africa Kuna mgao,Nigeria Kuna Mgao sembuse Tanzania?

Waziri amesema mwisho wa mgao ni machi ila Bunge likatoa mda zaidi kwamba Hadi June kusiwe na mgao tena.
 
Tanzania yenye Majuha ( Morons ) kama Wewe kupata Maendeleo ni Ndoto za Alinacha
Maendeleo yapi unayozungumzia wewe popoma?
 
South Africa Kuna mgao,Nigeria Kuna Mgao sembuse Tanzania?

Waziri amesema mwisho wa mgao ni machi ila Bunge likatoa mda zaidi kwamba Hadi June kusiwe na mgao tena.
Wanatoa muda wa ziada kwa maslahi ya nani?
 
South Africa Kuna mgao,Nigeria Kuna Mgao sembuse Tanzania?

Waziri amesema mwisho wa mgao ni machi ila Bunge likatoa mda zaidi kwamba Hadi June kusiwe na mgao tena.
We jamaa nahisi ntakua nakufahamu. Katika maisha yangu nimekutana na mtu mmoja tu mwenye arguments za aina hii.

Yaani utetezi wako ni sawa na mwanafunzi anaepata 30% kwenye mtihani, halafu akiulizwa kwanini amefeli anajibu "mbona Juma kapata 20%, Ali kapata 15% na James kapata 10%, sembuse mimi?" Badala ya kujilinganisha na Hamza aliepata 85%, Hassan aliepata 90%, Esta 78% nk.
 
We jamaa nahisi ntakua nakufahamu. Katika maisha yangu nimekutana na mtu mmoja tu mwenye arguments za aina hii.

Yaani utetezi wako ni sawa na mwanafunzi anaepata 30% kwenye mtihani, halafu akiulizwa kwanini amefeli anajibu "mbona Juma kapata 20%, Ali kapata 15% na James kapata 10%, sembuse mimi?" Badala ya kujilinganisha na Hamza aliepata 85%, Hassan aliepata 90%, Esta 78% nk.
Ok hayo ndio majibu ya serikali wewe unatakaje sasa
 
Hii nchi hata wananchi wake ni kama wamerogwa, hawako serious, tuliambiwa sababu ya mgawo wa umeme ni upungufu wa maji kwenye mabwawa, bahati nzuri mvua zimenyesha nchi nzima tena za kutosha, sasa wameanza sarakasi zingine. Nchi zingine upumbavu kama huu usingevumilika. Hii serikali ya awamu ya 6 kuna maeneo imefeli pakubwa sana.
 
Spika ni mjanja sana! Kaona muda ni mfupi hadi mwezi machi ikabidi awalinde kwa kuongeza muda hadi mwezi juni pengine hapo katikati watarekebisha mambo wasije wakadai walipewa muda mfupi kurekebisha mitambo yao
 
South Africa Kuna mgao,Nigeria Kuna Mgao sembuse Tanzania?

Waziri amesema mwisho wa mgao ni machi ila Bunge likatoa mda zaidi kwamba Hadi June kusiwe na mgao tena.
We jamaa ni mpuuzi kweli.
 
Back
Top Bottom