HIV inanitesa

Pole sana dada yangu, unyanyapaa ktk jamii kweli upo, lkn kama umeamua kuwakinga wengine kwa maambukizi honera sana kwa hilo, nakushauri ukiwa ktk mahusiano umjengee mwenza wako mazingira ya no condom no sex, aking'ang'ania kavu basi mueleze ukweli. Mungu akubariki dada yangu.
 
Huwezi kujua kama upo wala kuugopa mpaka ukute umeathirika, jamani this disease is very real, ipo, ipo kabisaaaaaaaa! Ahsante mdada kwa kutukumbusha, usiwaambukize wengine, utapata neema na thawabu zako kutoka kwa MUNGU! MUNGU akuongoze na kukufariji katika kipindi chote cha ugonjwa wako, na sisi wengine jamani tuache kucheat, ambao hawajao/olewa wafanye hivyo na wastick to one man/woman marriage, sio mzaha hali ni mbayaaaaaa!

you said it right cacico. But inapotokea mtu kaathirika kumyanyapaa hakufai kamwe kwani hatujui ya kwetu ya kesho.

ngoja nikupe mfano nilipogundua am diabetic Dr ambaye ni dada yangu mzazi aliniambia hivi mdogo wangu siku hizi heri uugue Ukimwi utapata dawa kuliko sukari. na kibaya zaid sukari inanyong'onyeza mwili kuliko hata huo ukimwi. so to her ugonjwa ni ugonjwa tu, manake wa aina yyte ile waweza kuleta kifo hapendezi kuwanyanyapaa wagonjwa fulan na kuwakumbatia wengine.
 
Last edited by a moderator:
you said it right cacico. But inapotokea mtu kaathirika kumyanyapaa hakufai kamwe kwani hatujui ya kwetu ya kesho.

Ngoja nikupe mfano nilipogundua am diabetic dr ambaye ni dada yangu mzazi aliniambia hivi mdogo wangu siku hizi heri uugue ukimwi utapata dawa kuliko sukari. Na kibaya zaid sukari inanyong'onyeza mwili kuliko hata huo ukimwi. So to her ugonjwa ni ugonjwa tu, manake wa aina yyte ile waweza kuleta kifo hapendezi kuwanyanyapaa wagonjwa fulan na kuwakumbatia wengine.
msiri wangu upoooooo?? Mi miss u bana, lol! Cant wait for november tukae tena brajec kama ilivyo ada! Lol
 
hujui unachokizungumza na hakika hujui umesimama wapi kiasi cha kujua utaangukia wapi?usihukumu maana hujui lipi hasa limemkuta huyu dada,and tht not our case here,hebu jaribu kukua kidogo katika hili unless una tatizo personal!

Poleni kwa kuwakwaza kama nimewakwaza lakini hii kaukli yake ndio iliniudhi sana:

Na wakati mwingine mie kama binadamu uwa najikuta kwenye mahusiano kama mjuavyo mara ya kwanza mtatumia kinga ya pili njemba inataka kavu hapo ndo uwa napatwa na ngazi mwili mzima.
 
Poleni kwa kuwakwaza kama nimewakwaza lakini hii kaukli yake ndio iliniudhi sana:

Na wakati mwingine mie kama binadamu uwa najikuta kwenye mahusiano kama mjuavyo mara ya kwanza mtatumia kinga ya pili njemba inataka kavu hapo ndo uwa napatwa na ngazi mwili mzima.

yaah nimekuelewa my dear,najua pia tunatofautiana reaction,kwa hili alilosema ni kweli linastua lakini still tuatakiwa kumwonysha makosa yake huku tukiepusha hili lisiendelee kutokea!pole pia dear!
 
Katika habari niliyosoma yote bila kupepesa macho ni hii!

Jipe nguvu na jipe moyo utashinda. Soon or very soon...dawa itapatikana! Na huo ugonjwa utakuwa kama malaria tu! Mbona mwanga umeshaanza kuonekana?

Nakushauri pia, badilisha user name yako kama alivyoshauri snowhite. Ukitaka kushinda vita yeyote, lazima ujifikirie kwamba wewe ni mshindi!

Kuna wengi wanaishi miongoni mwetu, wameathirika, lakini wanaendelea kupanga maisha yao kwa kwenda mbele.

Pia tukumbuke kuwa VVU vinaweza kumpata mtu yeyote! Safari_ni_Safari weye...maneno hayo!
 
Last edited by a moderator:
Pole sana kwa kuumwa ugonjwa huu wa ukimwi. Nimekupa pole kwa sababu umejaribu kufunguka na kuiambia jamii kuwa wewe ni mwathirika. Lakini bado hujawa muwazi kabisa wa kujitambulisha ili jamii ikakufahamu na kukusaidia pale unapokuwa na shida au vishawishi kama ulivyosema.

Huo uzuri wako, kusoma kwako, nyumba na gari ni mali yako na visije kuwa vichocheo vya wewe kuwarubuni vijana na watu wengine wenye uroho wa fisi. Jitangaze kwa jina lako kamili na picha ili utambulike na hiyo itasaidia kutimiza ndoto yako ya kuondoa unyanyapaa hapa Tanzania na kumaliza hasira za kutaka kuambukiza watu kutokana na kunyanyapaliwa.

Lakini hujatueleza kinagaubaga unafikiri ni nini chanzo cha wewe kuwa mwathirika wa ukimwi kwasabu mlipokwenda kupima na mchumbaako wewe ndiye uliyeoneka mgonjwa? Je, ni uzuri wako uliokutumbukiza huko? Manake kutokana na maelezo yako inaonyesha bado unataka kuwatia watu majaribuni kwa kuwaambia ni jinsi gani wewe ulivyo mzuri! Hatari sana.
 
Mbona NGo's zipo nyingi ambazo unaweza Kujiunga nazo dada angu'..Kile aMBacho unaweza waambia hApa JF wale ambao wana status kama yako na HAta wasijitambua wakapime then Mujiunge kwa izo NGO's kama wasomi mtakuwa mmetumia Elimu yenu vizuri...

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
msiri wangu upoooooo?? Mi miss u bana, lol! Cant wait for november tukae tena brajec kama ilivyo ada! Lol
sasa hivi viwanja vimebadilika lol! kuna sehem nzuri acha kabisa wewe yaani ni full misosi na mamvinyo ya kufa mtu. ngoja nikamilishe kaz nitakualika mahali hutoamini. btw nakumbuka ulinikatili hamu yangu ya kwenda kunywa chai na wewe umesahahu enh?

this time kuna coffee bar moja matata mahali hakya Mungu lazima uende hata kwa fimbo lol?
 
oh!sikia mamii
hebu badilisha kwanza hyo user name yako,umeanza kujinyanyapaa mwenyewe!
kuwa ni mwathirika sio kifo,una nafasi ya kufanya mengi sana ambayo wengine(tunaoamini hatuna )hatufanyi
jipende na furahia maisha,kuathirika sio sababu ya kujikataa na kuwapa wengine sababu ya kukukataa au kujustfy kukataliwa na jamii,hiyo jamii inayokunyanyapaa yenyewe haijui hali zao kiafya ziko vipi
jichanganye na marafiki wengine watakaokupa tumaini la kuwa maisha yanaendelea,ukijifunga na kuamini kuwa kwa kuwa ur HIV+ basi marafiki unaowastahili ni wa aina hiyo tu hujitendei haki my dear!
wewe ni wa thamani sana na wa pekee!
thamani yako kama mwanadamu inabaki palepale haijalishi jamii inakuchukulia vipi!ulianguka hapo umefanikiwa kusimama ishi maisha yako unayodhani ni salama kwako na kwa wenzio!

I salute you, maneno kuntu maneno mujarabu kabisa Snowhite.
 
Una LEBO HIV+ utosini? wanakunyapaa vp?

Sio lazima kuwa na lebo, jamii nzima inavyowachukulia wenye virusi tu inaweza kuwa unyanyasaji. Habari za "ana ngoma" inakuwa kama tusi vile, na kwa sababu hawana lebo, mtu anaweza kusema vibaya wenye ukimwi huku hajui kwamba mtu wa pembeni yake ana virusi, or even worse, kwa sababu watu wengi hawajapima, mtu anaweza kusema vibaya wenye virusi wakati na yeye mwenyewe anavyo.
 
Poleni kwa kuwakwaza kama nimewakwaza lakini hii kaukli yake ndio iliniudhi sana:

Na wakati mwingine mie kama binadamu uwa najikuta kwenye mahusiano kama mjuavyo mara ya kwanza mtatumia kinga ya pili njemba inataka kavu hapo ndo uwa napatwa na ngazi mwili mzima.

kwani kosa ni lani hapo? yeye ama huyo njemba? tatizo ni wanaume ving'ang'anizi. dada yuko honest kabisa. msemo wa wanaume inzi kufia kidondani halali yake sasa hapo weye utasemaje?
 
Ndio umejiunga leo jamvini?
Kama unataka kweli muanzishe network ya JF+ unaonaje ukitumia ID yako ya zamani ili watu wakutrust?
Otherwise, hongera kwa positive thinking na kuwawajali na kuwalinda wengine.
 
Hivi jamani naomba kuuliza, hivi ni kweli condom huzuia maambukizi ya ukimwi?
Vipi kuhusu vitendo vingine vihusianavyo na ufanyaji ngono kama kunyonyana ndimi na midomo, kunyonya uke, kunyonya chuchu, kusugua uke wa mwanamke kwa kidole(sidhani kama huwa chavishwa condom)...
Maelezo ya bi dada HIV+ yamenifanya niamini kuwa kasi ya maambukizi ni kubwa na idadi ya waathirika si laki 9 kama serikali inavyobainisha kuna uwezekano hiyo namba ikawa hata mara mbili zaidi.
 
hii outing ya brajec november na mie msiniache jamani,napenda sana girls day out!pleeeeeease!
usjali lol! ila tu iyo huwa tunakaa kisha usiku tunaenda club japo kudance kidogo lol! japo wazee lakin tutoe stress atii.
 
sasa hivi viwanja vimebadilika lol! kuna sehem nzuri acha kabisa wewe yaani ni full misosi na mamvinyo ya kufa mtu. ngoja nikamilishe kaz nitakualika mahali hutoamini. btw nakumbuka ulinikatili hamu yangu ya kwenda kunywa chai na wewe umesahahu enh?

this time kuna coffee bar moja matata mahali hakya Mungu lazima uende hata kwa fimbo lol?
mi nishaboo kualikwa jamani!ahahhahah kama hamtajali jamani!
 
52 Reactions
Reply
Back
Top Bottom