Historia ya Mombasa na makabila yake

Historia ya Mombasa na makabila yake

mi ni mmoja kati ya watu wanaoamini PWANI si KENYA
Hivi mtaamini nikiwaeleza kuwa pwani ya kenya ilikuwa chini ya himaya ya ufalme wa zanzibar hadi baada ya kikao cha lancaster house kukubalika kenya kupewa uhuru ndipo kinamzee kenyatta walipoiomba serikali ya uingereza iwapatie eneo hilo na serikali ya uingereza ikanunua eneo hilo toka kwa mfalme wa zanzibar na tokea mwaka 1962 mwambao wa kenya ukawa chini ya serikali ya kenya
 
Ni maili kumi tu kutoka pwani ndo ilibaki himaya ya masultani ------- wa zanzibari. Japo utapata miji mingi hata kilometa 300 ndani bado yana majina ya hao watu kama Sultan Hamudu
 
Hivi mtaamini nikiwaeleza kuwa pwani ya kenya ilikuwa chini ya himaya ya ufalme wa zanzibar hadi baada ya kikao cha lancaster house kukubalika kenya kupewa uhuru ndipo kinamzee kenyatta walipoiomba serikali ya uingereza iwapatie eneo hilo na serikali ya uingereza ikanunua eneo hilo toka kwa mfalme wa zanzibar na tokea mwaka 1962 mwambao wa kenya ukawa chini ya serikali ya kenya
Kwamaana nyingine mombasa ni tz, kwaherin
 
Ambayo maana yake kwa Kiingereza ni:

Kongowea (Mombasa) is like a roaring surf; Mvita is a city of old
It is always seething (with trouble), with so much noise and endless cries
It is a place full of shields, lances, bows and arrows, and long
swords
The dead are dead and gone! There is no feigning death (i.e. one
dies only once).

Gongwa (Mombasa) is a city full of malice (towards its enemy), so
bear no spite against it!
It thrusts down powerful ones and renders them as helpless as the sick
It shatters them and fills their hearts with sorrow
The dead...

Gongwa is the land of Mwana Mkisi*; Mvita, what an awesome
place it is!
It has warlike men who spoil for a fight
Men who are intransigent and obdurate, possessed of everlasting
fury
The dead....

If you (Omanis) have come seeking a war with our mighty lions
Then bear their clamorous wrath, and do not flee!
These lions have terrible claws that are already stretched out
The dead....

It is still we Mombasans, indeed it is. Do not think we are dead
It is us you are waging war against. We are fighting you so that
you may not rule over us
It is we demons who destroy yonder lands
The dead....

When Kongowea roars, it groans like someone suffering from a
terrible malady
Even those who are far away hear its rumblings
The warriors quietly take their positions and make their strategic
manoeuvres
The dead....
Ahsante sana ingawa mimi ni mpenzi wa historia ya mwambao wa afrika mashariki lakini umenielimisha kitu ambacho nilikua sikifahamu -Ahsante
 
Usichanganje mada, hapa tunazungumzia historia ya mombasa.
Vijana wengi wa pwani hawafahamu historia ya maeneo yao na uzi huu ni fursa japo ndogo tu kuelewa makabila , mila, desturi, dini nk ya maeneo yao.
Kama wewe unaona haikufai achana nayo ila unahaki ya kuanzisha uzi mwingine unaohusiana mkoa wa kilimanjaro.
 
Mombasa ni mji umezaliwa kwa vita ndiposa eneo la kati bado laitwa Mvita.
tangu miaka za nyuma Waswahili pamoja na ndugu zao Wamijikenda wamekuwa wakitwangana na Waarabu Wamanga( Oman), Waajemi ( Persians), Wabulushi, Wahadhramuti (Yemen), Wareno, Waturuki na Wazanzibari.
Japo sasa hawa watu wote wamo na wanaishi nasi bado mji upo imara.
~
Ni waswahili tu waliyaacha majina yao wakaanza kujiita majina ya waarabu lakini bado mila na tamaduni zao zile zile.
Kiswahili kimezaliwa Kenya haswa Lamu baaada ya wabantu kugura Shungwaya kuepuka mashambulizi ya Wagalla na watu ambao siku hizi twawaita Wasomali.
Singwaya ilikuwa maeneo ya Kismayu kusini mwa Somalia ya sasa. Bado kuna makabila kongwe ya Waswahili kule - Wabajuni, Watikuu, Wabarawa, Wambalazi, Wamwini, Wandau n.k. japo wengi wamehamia Kenya na Tanzania kwa sasa.
 
Mwandishi: Hamisi Malengo

Mijikenda Ni Kina nani?

2014-04-24

111.jpg


Neno'' Mijikenda'' maana yake ni miji tisa au makabila tisa, pia huitwa ''Makaya Chenda''.
Chimbuko la Wamijikenda latoka nchi ya Congo kama makabila mengine ya kibantu na walikaa Tanzania kisha wakahamia kusini mwa Somalia sehemu iitwayo ''Shungwaya'' ambayo inapatikana baina ya Mto Juba na Webbi Shebeli.Walipokuwa Shungwaya walikuwa wakiitwa ''Ashungwaya au ''Ashuru''.

Mababu wa Wamijikenda walichagua jina hili walipofika Pwani ya Kenya ili kuashiria makabila tisa yanayounda Mijikenda nayo ni: Giriama, Kauma, Chonyi, Kambe, Jibana, Ribe, Rabai, Duruma na Digo.
Mtafiti Thomas Spear anasema kwamba Baba ya Wamijikenda ni ''Muyeye'' na alioa wanawake wawili alipokuwa Shungwaya, wakwanza ni ''Mbodze'' na wapili ni ''Matsezi'' ambao alizaa nao watoto tisa waliopelekea kupatikana kwa makabila ya Mijikenda.

Aliongeza kwamba Shungwaya hakukaa Mijikenda pekee bali kulikuwa na makabila mengine nao ni: Waboni, Wasegeju, Wataita, Wasanye, Wataveta, Wasagalla, Waata na Walangulo.

Makabila yote haya yanaishi Pwani ya Kenya lakini idadi yao ni ndogo sana isipokuwa Wataita na Wataveta kwani idadi yao ni kubwa na wanaishi katika Kaunti ya Taita Taveta.
Wamijikenda wanaishi Pwani na Mombasa ndio mji Mkuu wa Pwani na uko mbali na Jiji la Nairobi kwa takriban kilomita 500.

Idadi yao ni inakaribia milioni tatu na sehemu wanazoishi ni:Taita Taveta, Kwale, Mombasa, Kilifi, Malindi, Tana River Tana Delta na Lamu.
Katika upande wa dini Wamijikenda walikuwa wakizitukuza Turathi za Mababu zao ilhali wengine walikuwa wakiabudu Mizimu

. Kila kabila lilikuwa na sehemu ya kufanyia ibada ya kuabudu Mizimu zinazoitwa '‘Kaya'' ambayo ni misitu mikubwa iliofungamana. Kwaajili hiyo imani yao ya kumuabudu Mwenyezi Mungu ilikuwa dhaifu sana.

Hali iligeuka baada ya kuingia ulinganizi wa dini ya Kiislamu na Kikristo katika sehemu zao, watu walianza kuingia katika dini ya Kiislamu kwa wingi, baadhi yao waliingia katika dini ya Kikristo ilhali wengine walibakia katika dini zao za kuabudu Mizimu.

Katika upande wa Siasa Wamijikenda walikuwa wakiongozwa na Wazee ambao walikuwa wakihakikisha kwamba watu wanaishi pamoja na kusaidiana katika mambo mbalimbali na walikuwa wakichaguliwa kulingana na sifa zao njema kama vile Utu, Ushujaa, Ukarimu zikiwemo na sifa zengine.

Wamijikenda walikuwa wanatambulika hata kabla ya Kenya kupata uhuru, waliunda chama chao cha kisiasa mwaka 1945 kilichoitwa ''Muungano wa Wamijikenda'' (MIJIKENDA UNION) na kiliongozwa na marehemu Ronald Ngala ambaye asili yake ni Mgiriama. Chama hiki kiliundwa kwa lengo la kutetea haki za Wamijikenda.


ronald%20ngala.jpg


Katika mwaka 1963, Ronald Ngala alianzisha chama cha kisiasa kilichoitwa ''KADU'' (KENYA AFRICAN DEMOCRATIC UNION) na yeye ndie aliekuwa kiongozi wa chama hicho na Rais mstaafu wa Kenya Daniel Toroitich Arap Moi alikuwa naibu wake.

Mwaka huo huo kulifanyika makubaliano baina ya chama cha KADU na chama cha ''KANU'' (KENYA AFRICAN NATIONAL UNION) ambacho kilikuwa kikiongozwa na aliyekuwa Rais wa kwanza wa Kenya marehemu Mzee Jomo Kenyatta, walikubaliana kukifutilia mbali chama cha KADU ili kuunda chama kimoja cha KANU.

Ronald Ngala alikubali wito huu na alichaguliwa kuwa waziri katika serikali ya Kenya mpaka alipofariki mwaka 1982.
Katika upande wa uchumi Mijikenda wanategemea kilimo na kufuga wanyama.

Wanapanda mimea kama vile: Muhogo, Kunde, Mahindi na Viazi tamu ikiwemo na mimea mengine pia hufuga Ng'ombe, Kondoo na Mbuzi. Walifanya biashara na walikuwa Madalali katika biashara baina ya Waarabu na Wagalla kwani walikuwa wakizichukua ng'ombe kutoka kwa Wagalla na kuwauzia Waarabu ambao walikuwa na mafungamano ya kibiashara na Wabantu kupitia Pwani ya Kenya.

Wamijikenda walianzisha Soko Giriama sehemu iitwayo'' Birya''.
Katika mwaka 1858 Wamaasai walivamia sehemu za Wamijikenda na waliiba idadi kubwa ya ng'ombe kwasababu walikuwa wanaamini kwamba ng'ombe zote Duniani ni zao.

mijikenda2.jpg


Wamijikenda kwa sasa wanategemea kilimo cha Mahindi, Makaa ilhali wengine wanategemea biashara ya kuuza Pombe ya Mnazi.


Katika upande wa mavazi mwanamume huvaa nguo iliyotengenezwa kwa pamba inayoziba sehemu ya chini mpaka magotini iitwayo "Mfulo" na juu yake huvaa kipande cha nguo nyengine iitwayo ''Mkumbuu'' kisha huvaa nguo nyengine juu ya bega lake la kushoto iitwayo ''Yamba'' na juu ya bega lake la kushoto huweka fimbo yenye vichwa viwili inayomsaidia na shughuli zake zengine.

Mwanamke huvaa nguo ya kitamaduni iliyotengenezwa kwa pamba na huwa na miuzi mingi mizito iitwayo ''Hando'' na wanawake walioolewa hujifunga pambizoni mwa tumbo zao mkanda unaoitwa ''Magalia'' na juu ya shingo yake huvaa mkufu unaoitwa ''Ndale'' na kwenye miguu yake huvaa ''vikuku'' pamoja na kuvaa mapambo mengine yanayomfanya yeye kuwa tofauti na wenzake pia hujipaka wanja kenye macho yake na manukato kwenye mwili wake yaitwayo "Muranze".

Katika upande wa harusi jambo la kumchagua msichana huachiwa wazazi au Baba Mdogo ama Shangazi. Msichana huchaguliwa kutoka familia yenye kusifika na sifa ya kazi, uaminifu zikiwemo na sifa zengine njema.
Wakati wa kuposa mzazi wa kijana huandamana na baadhi ya watu katika familia pamoja na marafiki zake mpaka kwa wazazi wa binti anayehitajika kuposwa huku wamebeba chupa zilizojaa pombe ya mnazi na huitwa ''Kadzama''.

Wakifika nyumbani kwao husema maneno haya:''Namala mudzungu wa utsungu'' maana yake ni nimekuja nyumbani kwenu ili kumposa binti yenu kwaajili ya kijana wangu. Kama msichana hajaposwa Babake husema:''Mudzungu wa utsungu uhaha'' maana yake ni karibuni sana mnachokihitajia kipo.


Sacred-Mijikenda-Kaya-Forests-Kenya.jpg


Baba wa kijana hupeana pombe kwa Baba ya msichana ambaye humuita na kumuonyesha kama ishara kwamba wageni wamekuja kumposa.

Binti akiridhia, Babake hupeana ile pombe kwa Baba zake wadogo na Wajomba ili nao wanywe na kuonyesha kwamba wamekubali. Kisha Baba ya kijana humueleza mwanawe yote yaliyojiri na humtuma ili amwangalie msichana na kufahamiana nae huku wakisuhubiana na marafiki zao kwani hawaruhusiwi kukaa faragha kabla ya ndoa.

Baada ya mda wa wiki moja au mbili Baba ya kijana hurudi kwa mara ya pili ili kutoa Mahari yaitwayo ''Mahunda'' ambayo zamani ilikuwa ni ng'ombe au mbuzi tofauti na sasa.
 
Mombasa iliwahi tekwa mara mbili tu na wakaazi wakatorokea nyika hata na Malindi na Lamu.
1587 wala watu waitwao WaZimba walianza vita hatari katika miji ya Tete na Sena nchini Msumbiji wakapanda wakimla kila mtu katika jiji walizoteka. Kilwa waliwala watu alfu tatu...Mombasa watu wote wakatorokea Malindi. Ilikuwa ni Malindi tu ndo WaSegeju waliwashinda na kuwaua Wazimba na kumaliza kero.

Mara ya pili ilitokana na uvamizi wa wala watu toka Madagaska waitwao WaSakalava ambao walimla hata Sultani wa Kilwa enzi hizo.
Baadaye mwaka 1698, Wareno walifukuzwa mjini na Ngome Ya Yesu ikatekwa. Hapo ndipo WaOmani wakaanza kujazana kisiwani kwetu na kuleta athari mbaya ya mila zao na wengi kujifanya Waswahili. Hii ilikubalika kwa sababu urithi wa mbari kwa Waswahili unatokana na mama kwa hivyo wana wa waarabu, wajemi, wasindhu, wahadhramuti, wamalayi, wajava, wahindi wakaanza kujiita Waswahili na kuzagaa kote mwambao na hapo wamijikenda ambao lugha yao ilikuwa sawia na Kiswahili kwa kiasi kikubwa enzi zile wakaanza kujitenga.
Hapo ndo maneno mengi ya Kiarabu na lugha nyenginezo yakaingia Kiswahili.
Ni Wadigo tu walikubali kuwa Waislamu. WaDuruma nao wakawafata baadaye lakini wengine haswa WaGiriama na Warabai wakaendelea na mila zao za jadi.
 
Hapa nadhani hatuna tena ubishi kuwa Kiswahili kimeanzia wapi na ni nani anayo historia ndefu kati ya Mombasa na Zanzibari. Gede, Lamu, Pate, Faza, Shanga, Shela, na visiwa vya bajuni ndio miji ya kwanza ya Waswahili vikiwa vimeanzishwa kati ya karne ya 5 na ya 9 - 500AD hadi 800AD.
Mombasa imeanza mwaka wa 900AD ikiwa Malindi ni nzee kidogo.
~
Visiwa vya Pemba na Unguja vilikuwa vikimilikiwa na makabila ya kibantu ya Pwani tangu enzi za zama wakiwemo wa Digo, Bondei, Zigua, Wasini, Zaramo, Ndengereko, Doe, Kwere n.k. lakini walikuwa wameisha swahilishwa wakati Wareno wanaingia miaka ya 1500 na wakati wa Omani wanaanza kuwatawala. Mila na dasturi zao za jadi ni za kibantu cha bara na wala sio kiarabu na Kiajemi kama watu wanavyodanganywa sasa.
 
Haya sasa tizama mbari za Waswahili wa Mvita ( Mombasa).
Hawa ndo Waswahili wa jadi. Jina lao haswa ni Wa Ngozi.
Asili ya Mswahili sio Omani wala uarabuni kama fulani wanavyowahadaa watu.
Makabila ya waswahili yapo na asili yao ni Bantu na lugha zao sawasawa tu na zengine za Ki mijikenda.
Hamna Mwarabu aliyekuja hapa kutufunza ndimi yetu.
Tujivunie na majina yetu tuwache kuwapa watoto wetu majina ya ghuba na ulaya. Ngeu haipotei.
Turudi asili yetu.
Somo limetolewa na Shehe Stambuli
Wa-Kilindini:
Mbari ya Mwinyi Nguti wa Mwinyi Mwinzagu
" " " Hunzi
" " " Kombo wa Dani
" " " Kae wa Pembe
" " " Hudumzi
Wa-Tangana:
Mbari ya Mwinyi Muli
" " " Mjaka
" " " Umbwi
" " " Ngwisa
Wa-Changamwe:
Mbari ya Mwinyi Kitue
" " " Mgosi
" " " Mfaki
" " " Koba
" " " Ngovo
 
Hizi ndio mbari za Waswahili kwa wale wanaosema hakuna kabila la Wangozi (Waswahili).
Je wayaona yale majina ya ghuba hapa? Akina Al ndizi bin paipai ibn embe?
Sasa aje mjinga kutuambia eti Waswahili na Kiswahili kilianzia Masahariki ya Kati na Bara Asia wakati twajua ni WaMijikenda na makabila mengine ya KiBantu ya mwambao wa Pwani ya Afrika mashariki ndio waliowazaa ndu'zetu hawa.


1. MBARI ZA WAKILINDINI

Mbari ya Mwinyi Nguti wa Mwinyi Mwinzagu
" Mwinyi Humzi
" Mwinyi Kombo wa Dani
" Mwinyi Kae wa Pembe
" Mwinyi Hudumzi



2. MBARI ZA WATANGANA

Mbari ya Mwinyi Muli
" Mwinyi Mjaka
" Mwinyi Umbwi
" Mwinyi Ngwisa


3. MBARI ZA WACHANGAMWE

Mbari ya Mwinyi Kitue
" Mwinyi Mgosi
" Mwinyi Mfaki
" Mwinyi Koba
" Mwinyi Ngovo


4. MBARI ZA WAMVITA

Mbari ya Mwinyi Kutani
" Mwinyi Kae
" Mwinyi Hunziali


5. MBARI ZA WAMALINDI

Mbari ya Banu Shasha
" Banu Mbwana


6. MBARI ZA WAJOMVU (au WAJUNDA)

Mbari ya Mwinyi Faki
" Mwinyi Chande wa Shamaniya
" Mwinyi Usi Muhija
" Mwinyi Uledi wa Ndau
" Mwinyi Jaa wa Mwinyi Nguti


7. MBARI ZA WAMTWAPA

Mbari ya Mwinyi Nyali (au Mbari ya Ng'ombeni)
" Mwinyi Jimve
" Mwinyi Goziadi
" Mwinyi Rakwe
" Banu Muyaka
" Banu Shemapwe

8. MBARI ZA WAKILIFI

Mbari ya Mwinyi Shoka
" Mwinyi Kiwanda
" Mwinyi Mkomati
" Mwinyi Gome


9. MBARI ZA WAPATE

Mbari ya Wa-Pate
" Wa-Amu
" Wa-Kitau
" Wa-Twaka
" Wa-Tukut
" Wa-Kipungani
" Wa-Barawa
" Wa-Shela

10. MBARI ZA WAGUNYA (au WABAJUNI)

Mbari ya Washaka
" Wa-Uziwa
" Wa-Ungama
" Wa-Ozi
" Wa-Sada
 
Sasa kama ulitaka kujua majina kindakindaki ya Waswahili kabla hawajakuja wageni bas hapo umeyapata yote.
 
Back
Top Bottom