Jumbe Kondo
Senior Member
- Oct 18, 2011
- 109
- 68
Mombasa ni mji mkongwe wa Afrika ya mashariki wenye sifa na tarekhe ndefu mno. Mji wenyewe ni kisiwa kilichozungukwa na maji pande zote ambacho kina mikondo miwili ya bahari. Mkondo wa kwanza ni wa kaskazini yaani maeneo ya bandari ya zamani ya Mombasa hadi Mwakirunge, maeneo haya yalikuwa makao ya Waswahili wa miji tisiya (Tisa twaifa) wakiwemo; Wamtwapa, wamvita, Wakatwa, Wabajuni ama Wagunya, Wakilifi,Wafaza,Wajomvu na Washaka. Kati ya makabila haya wengine walihamia Mombasa baada ya kuvundika( kuvunjika) kwa miji yao na wengine walikuja kwa khiari.
Kwenye mkondo wa bahari wa kusini wa kisiwa cha Mombasa waliishi waswahili wa miji mitatu (Thalatha twaifa) nao ni Wakilindini, Wachangamwe na Watangana ambao ndio wenyeji wa asili wa mji Mombasa. Maisha ya watu hao yalitegemeya sana uvuvi,ukulima na biashara. Kulingana na historia hapo kale palikuwa na uhusiano wa kibiashara baina ya miji ya pwani na Uarabuni,Uajemi, bara Hindi na Uchina. Siku hizo za kale biashara ilikuwa ni ya kubadilishana vitu. Kwa mfano Waarabu walileta tende,nguo, chumvi na vyenginevyo kutoka makwao hadi upwa huu wa Afrika mashariki. Baada ya kumaliza kukaa kwao nao walipeleka makwao vitu kama nazi, vyakula na mbao za kuundia majahazi.
Kuhusiana na jina la Mombasa historia yake ni ndefu, na kabla ya jina hilo la "Mombasa" kuna majina mengine sita yaliyolitangulia nayo ni; Faladi,Kongoweya,Gongwa, Mvita, Mji wa Kale, Nyali Kuu na hatimaye kuitwa Mombasa. Na yote haya ni mabadilifu kwa namna mbali mbali.
Kuna hoja tofauti zinazohusiana na usuli wa neno "Mombasa". Hoja ya kwanza ni kuwa jina hili limetokana na maneno mawili ambayo ni "Mambo na Sasa". Hoja ya pili ni kuwa limetokana na neno "Mwambadze?" (ambalo ni la Kimijikenda na maana yake ni kama wasemavyo waswahili wa kimvita- mwambaje?- yaani, kwa "Kiswahili sanifu" husemwa hamujambo?)
Kwenye mkondo wa bahari wa kusini wa kisiwa cha Mombasa waliishi waswahili wa miji mitatu (Thalatha twaifa) nao ni Wakilindini, Wachangamwe na Watangana ambao ndio wenyeji wa asili wa mji Mombasa. Maisha ya watu hao yalitegemeya sana uvuvi,ukulima na biashara. Kulingana na historia hapo kale palikuwa na uhusiano wa kibiashara baina ya miji ya pwani na Uarabuni,Uajemi, bara Hindi na Uchina. Siku hizo za kale biashara ilikuwa ni ya kubadilishana vitu. Kwa mfano Waarabu walileta tende,nguo, chumvi na vyenginevyo kutoka makwao hadi upwa huu wa Afrika mashariki. Baada ya kumaliza kukaa kwao nao walipeleka makwao vitu kama nazi, vyakula na mbao za kuundia majahazi.
Kuhusiana na jina la Mombasa historia yake ni ndefu, na kabla ya jina hilo la "Mombasa" kuna majina mengine sita yaliyolitangulia nayo ni; Faladi,Kongoweya,Gongwa, Mvita, Mji wa Kale, Nyali Kuu na hatimaye kuitwa Mombasa. Na yote haya ni mabadilifu kwa namna mbali mbali.
Kuna hoja tofauti zinazohusiana na usuli wa neno "Mombasa". Hoja ya kwanza ni kuwa jina hili limetokana na maneno mawili ambayo ni "Mambo na Sasa". Hoja ya pili ni kuwa limetokana na neno "Mwambadze?" (ambalo ni la Kimijikenda na maana yake ni kama wasemavyo waswahili wa kimvita- mwambaje?- yaani, kwa "Kiswahili sanifu" husemwa hamujambo?)
Mwandishi: Hamisi Malengo
Mijikenda Ni Kina nani?
2014-04-24
![]()
Neno'' Mijikenda'' maana yake ni miji tisa au makabila tisa, pia huitwa ''Makaya Chenda''.Chimbuko la Wamijikenda latoka nchi ya Congo kama makabila mengine ya kibantu na walikaa Tanzania kisha wakahamia kusini mwa Somalia sehemu iitwayo ''Shungwaya'' ambayo inapatikana baina ya Mto Juba na Webbi Shebeli.Walipokuwa Shungwaya walikuwa wakiitwa ''Ashungwaya au ''Ashuru''.
Mababu wa Wamijikenda walichagua jina hili walipofika Pwani ya Kenya ili kuashiria makabila tisa yanayounda Mijikenda nayo ni: Giriama, Kauma, Chonyi, Kambe, Jibana, Ribe, Rabai, Duruma na Digo.Mtafiti Thomas Spear anasema kwamba Baba ya Wamijikenda ni ''Muyeye'' na alioa wanawake wawili alipokuwa Shungwaya, wakwanza ni ''Mbodze'' na wapili ni ''Matsezi'' ambao alizaa nao watoto tisa waliopelekea kupatikana kwa makabila ya Mijikenda.
Aliongeza kwamba Shungwaya hakukaa Mijikenda pekee bali kulikuwa na makabila mengine nao ni: Waboni, Wasegeju, Wataita, Wasanye, Wataveta, Wasagalla, Waata na Walangulo.
Makabila yote haya yanaishi Pwani ya Kenya lakini idadi yao ni ndogo sana isipokuwa Wataita na Wataveta kwani idadi yao ni kubwa na wanaishi katika Kaunti ya Taita Taveta.Wamijikenda wanaishi Pwani na Mombasa ndio mji Mkuu wa Pwani na uko mbali na Jiji la Nairobi kwa takriban kilomita 500.
Idadi yao ni inakaribia milioni tatu na sehemu wanazoishi ni:Taita Taveta, Kwale, Mombasa, Kilifi, Malindi, Tana River Tana Delta na Lamu.Katika upande wa dini Wamijikenda walikuwa wakizitukuza Turathi za Mababu zao ilhali wengine walikuwa wakiabudu Mizimu
. Kila kabila lilikuwa na sehemu ya kufanyia ibada ya kuabudu Mizimu zinazoitwa '‘Kaya'' ambayo ni misitu mikubwa iliofungamana. Kwaajili hiyo imani yao ya kumuabudu Mwenyezi Mungu ilikuwa dhaifu sana.
Hali iligeuka baada ya kuingia ulinganizi wa dini ya Kiislamu na Kikristo katika sehemu zao, watu walianza kuingia katika dini ya Kiislamu kwa wingi, baadhi yao waliingia katika dini ya Kikristo ilhali wengine walibakia katika dini zao za kuabudu Mizimu.
Katika upande wa Siasa Wamijikenda walikuwa wakiongozwa na Wazee ambao walikuwa wakihakikisha kwamba watu wanaishi pamoja na kusaidiana katika mambo mbalimbali na walikuwa wakichaguliwa kulingana na sifa zao njema kama vile Utu, Ushujaa, Ukarimu zikiwemo na sifa zengine.
Wamijikenda walikuwa wanatambulika hata kabla ya Kenya kupata uhuru, waliunda chama chao cha kisiasa mwaka 1945 kilichoitwa ''Muungano wa Wamijikenda'' (MIJIKENDA UNION) na kiliongozwa na marehemu Ronald Ngala ambaye asili yake ni Mgiriama. Chama hiki kiliundwa kwa lengo la kutetea haki za Wamijikenda.
![]()
Katika mwaka 1963, Ronald Ngala alianzisha chama cha kisiasa kilichoitwa ''KADU'' (KENYA AFRICAN DEMOCRATIC UNION) na yeye ndie aliekuwa kiongozi wa chama hicho na Rais mstaafu wa Kenya Daniel Toroitich Arap Moi alikuwa naibu wake.
Mwaka huo huo kulifanyika makubaliano baina ya chama cha KADU na chama cha ''KANU'' (KENYA AFRICAN NATIONAL UNION) ambacho kilikuwa kikiongozwa na aliyekuwa Rais wa kwanza wa Kenya marehemu Mzee Jomo Kenyatta, walikubaliana kukifutilia mbali chama cha KADU ili kuunda chama kimoja cha KANU.
Ronald Ngala alikubali wito huu na alichaguliwa kuwa waziri katika serikali ya Kenya mpaka alipofariki mwaka 1982.Katika upande wa uchumi Mijikenda wanategemea kilimo na kufuga wanyama.
Wanapanda mimea kama vile: Muhogo, Kunde, Mahindi na Viazi tamu ikiwemo na mimea mengine pia hufuga Ng'ombe, Kondoo na Mbuzi. Walifanya biashara na walikuwa Madalali katika biashara baina ya Waarabu na Wagalla kwani walikuwa wakizichukua ng'ombe kutoka kwa Wagalla na kuwauzia Waarabu ambao walikuwa na mafungamano ya kibiashara na Wabantu kupitia Pwani ya Kenya.
Wamijikenda walianzisha Soko Giriama sehemu iitwayo'' Birya''.Katika mwaka 1858 Wamaasai walivamia sehemu za Wamijikenda na waliiba idadi kubwa ya ng'ombe kwasababu walikuwa wanaamini kwamba ng'ombe zote Duniani ni zao.
![]()
Wamijikenda kwa sasa wanategemea kilimo cha Mahindi, Makaa ilhali wengine wanategemea biashara ya kuuza Pombe ya Mnazi.
Katika upande wa mavazi mwanamume huvaa nguo iliyotengenezwa kwa pamba inayoziba sehemu ya chini mpaka magotini iitwayo "Mfulo" na juu yake huvaa kipande cha nguo nyengine iitwayo ''Mkumbuu'' kisha huvaa nguo nyengine juu ya bega lake la kushoto iitwayo ''Yamba'' na juu ya bega lake la kushoto huweka fimbo yenye vichwa viwili inayomsaidia na shughuli zake zengine.
Mwanamke huvaa nguo ya kitamaduni iliyotengenezwa kwa pamba na huwa na miuzi mingi mizito iitwayo ''Hando'' na wanawake walioolewa hujifunga pambizoni mwa tumbo zao mkanda unaoitwa ''Magalia'' na juu ya shingo yake huvaa mkufu unaoitwa ''Ndale'' na kwenye miguu yake huvaa ''vikuku'' pamoja na kuvaa mapambo mengine yanayomfanya yeye kuwa tofauti na wenzake pia hujipaka wanja kenye macho yake na manukato kwenye mwili wake yaitwayo "Muranze".
Katika upande wa harusi jambo la kumchagua msichana huachiwa wazazi au Baba Mdogo ama Shangazi. Msichana huchaguliwa kutoka familia yenye kusifika na sifa ya kazi, uaminifu zikiwemo na sifa zengine njema.Wakati wa kuposa mzazi wa kijana huandamana na baadhi ya watu katika familia pamoja na marafiki zake mpaka kwa wazazi wa binti anayehitajika kuposwa huku wamebeba chupa zilizojaa pombe ya mnazi na huitwa ''Kadzama''.
Wakifika nyumbani kwao husema maneno haya:''Namala mudzungu wa utsungu'' maana yake ni nimekuja nyumbani kwenu ili kumposa binti yenu kwaajili ya kijana wangu. Kama msichana hajaposwa Babake husema:''Mudzungu wa utsungu uhaha'' maana yake ni karibuni sana mnachokihitajia kipo.
![]()
Baba wa kijana hupeana pombe kwa Baba ya msichana ambaye humuita na kumuonyesha kama ishara kwamba wageni wamekuja kumposa.
Binti akiridhia, Babake hupeana ile pombe kwa Baba zake wadogo na Wajomba ili nao wanywe na kuonyesha kwamba wamekubali. Kisha Baba ya kijana humueleza mwanawe yote yaliyojiri na humtuma ili amwangalie msichana na kufahamiana nae huku wakisuhubiana na marafiki zao kwani hawaruhusiwi kukaa faragha kabla ya ndoa.
Baada ya mda wa wiki moja au mbili Baba ya kijana hurudi kwa mara ya pili ili kutoa Mahari yaitwayo ''Mahunda'' ambayo zamani ilikuwa ni ng'ombe au mbuzi tofauti na sasa.