Hip Hop tumewakosea nini mabinti?

Hip Hop tumewakosea nini mabinti?

Kwakweli one the incredible ni hatari kwa wachana mistari
 
mm nadhani lugha chafu na style za maisha ya baadhi ya ma mc ndio ovyo,mfano kalapina,nyimbo ina matusi kibao,na mambo mengine kama kelele nyingi hua zinawaboa wadada,hata mm mtoto wa kiume sipendi mc anakua na mziki una matusi kibao,napenda sana hip hop hawa hapa,imam abbas,balozi dulasoul,mansour,hashim dogo,jay moe,prof jizy,fid q,adili,fanani,marehemu ngwea,king zila,ay na kala jeremiah,jcb,joe makini na nick wa pili,darasa,one,nick mbishi,lakini hao akina sijui roma mkatoliki,mheshimiwa temba,kalapina,nasikiaga kelele tu,ila cha ajabu 2pac alikua anapendwa sana na wadada,nadhani tungo zake pia zilikua saa nyingine zinawafanya wanawake wampende,nyimbo kama dear mama,baby dont cry,do for love,tatizo ma mc wa bongo akili ndogo ukiacha hao niliowataja na matamasha yenu sio,yamejaa ujinga,cheki matamasha ya jay z then utaona wadada wanavyopagawa,utasikia "we love you jay z" mjifunze kua na mvuto.
 
One.jpg

ant virus
 
Hio hop ni harakati na bahati mby wadada wako mbl sn na harakati! Wanataka kuimbiwa about love, starehe na raha! Hawataki kuskia shida na dhiki zinazoimbwa ktk sehemu kby ya hip hoo!
Uhuni ni binadam km mtu na sio tasnia husika!
Mbona rihana kachezea vichapo vya c.brown na brown hafanyi hio hop! W. Houston kafa mteja na hkw mtu HH!
TID mteja, kampiga mtu na jeka kaenda, TID hfny HH.
HH inatumia ubongo mgumu, na wadada hawapendi!
Siku ndomo akiwaimbia dhiki na shida za kitaa watamtema!
 
kuna ngoma nying za hiphop ni nzur...mi napenda mziki mzuri..i lyk councious!! mziki frm tamaduni musiq na weusi ndo aina ya hiphop ambayo wanawake wanapenda. umeona style ya gnako aluvyoswitch..unaona rap style ya kina joh makin n stereo!! waschana classic na hata wasiopenda kabisa hiphop wakienda kwny shoo wanaeza kucheza
 
Warembo niwaulize,men mnisaidie,kwa nini mabinti hawana feelings na wana wenye Hiphop lifestyle.Acha uhusiano wa mapenzi,hata ngoma zetu za movement "harakati" hamtaki kuskiza!Hata zile ngoma tunazowaimbia mnaziweka kapuni."Renee-Lost Boyz","Sonia,Radhia-Juma Nature", Mbona inakuwa kama nini warembo

Alafu wana Hip Hop ndo wanajua kuwaimbia mabinti na kuwasifia cha ajabu wadada hawapendi sana. Kama mdada tafuta ngoma ya Chochote Popote ya Joh makini, Right Here Ya G Nako, Una ya Profesor Jay au she gotta gwan ya Ngwair
 
wadada wanapenda v2 lainilainii!2cwalaum ndo walivoumbwa...achana na wanawake kwny harakat iz..kweny mgegedo ndo idara yao
 
Kinachosumbua hip hop ni nguvu nyingi, akili ndogo na kujidai ubabe hata pasipotakiwa.

Ila cha ajabu, mie na John Makini ni kitanda na shuka, nampenda sana huyu mwanamziki. Nitafutie kibao chake cha 'nikumbatie' akiwa na fundi Samwel.

toa mfano wa ubabe huo, majibu ya hii post yapo kwenye nyimbo ya nash mc Naandika
 
Hip Hop ni utamaduni kamili usio na shaka hata kidogo na ni harakati toka kuanza kwake na dhumuni lake ni ukombozi sasa hawa wanawake na harakati ni tofauti kabisa na kila kilichomo kwenye hip hop ni tofauti kabisa na maisha halisi ya binti hasa wa hapa kwetu wao wanataka wanaume walamba lips,skin jeans,poda usoni vitu ambavyo hauwezi vikuta kwenye huu utamaduni alafu hata mashairi ya nyimbo za mapenzi za hip hop lazima ufikiri na hawa wadada wanataka kusikia tu "mama Nassibu mama,mama Kidoti mama....." muda wa kufikiri kwenye muziki wenye ujumbe ni kipaji mfn Sonia au Radhia,wewe angalia hekaheka zao kwenye habari za GPL utanielewa au nenda kule siasani au jukwaa lolote ambalo lazima ufunguke utawakuta wachache kama jiongeze ila lazima tuwaelewe kua hip hop sio utamaduni wao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom