QUALIFIED BIOLOGY TEACHER
Member
- Oct 27, 2024
- 33
- 277
Leo asubuhi nilipeleka maombi ya kazi katika moja ya shule hapa mjini. Lakini uzoefu niliokutana nao leo ulikuwa mbaya sana.
Picha inaanza nilipofika getini, nikamsalimia mlinzi, mwanaume mwenye umri unaokadiriwa kuwa zaidi ya miaka 44. Nikamwambia naomba anielekeze ofisi ya mkuu wa shule. Mlinzi yule akaniambia kuwa bosi anaongea kwa simu, hivyo anipe CV zangu ili atampatie akimaliza. Nikamuomba kuwa nipo tayari kumsubiri mkuu hadi atakapomaliza kuongea kwa simu, lakini mlinzi akakataa.
Nilimsihi sana mlinzi yule angalau anipe dakika tano, lakini bado alikataa. Nikamuomba basi aniruhusu nipeleke bahasha hiyo kwa sekretari wa mkuu wa shule, naye akakataa. Nikaona sina jinsi, hivyo nikampa mlinzi bahasha yangu.
Cha kushangaza, mlinzi yule akaifungua bahasha na kuanza kusoma barua ya maombi na CV zangu. Nilihisi huzuni sana kiasi cha machozi kunilengalenga. Nikaona labda haikuwa bahati yangu kufanya kazi katika taasisi hiyo.
Picha inaanza nilipofika getini, nikamsalimia mlinzi, mwanaume mwenye umri unaokadiriwa kuwa zaidi ya miaka 44. Nikamwambia naomba anielekeze ofisi ya mkuu wa shule. Mlinzi yule akaniambia kuwa bosi anaongea kwa simu, hivyo anipe CV zangu ili atampatie akimaliza. Nikamuomba kuwa nipo tayari kumsubiri mkuu hadi atakapomaliza kuongea kwa simu, lakini mlinzi akakataa.
Nilimsihi sana mlinzi yule angalau anipe dakika tano, lakini bado alikataa. Nikamuomba basi aniruhusu nipeleke bahasha hiyo kwa sekretari wa mkuu wa shule, naye akakataa. Nikaona sina jinsi, hivyo nikampa mlinzi bahasha yangu.
Cha kushangaza, mlinzi yule akaifungua bahasha na kuanza kusoma barua ya maombi na CV zangu. Nilihisi huzuni sana kiasi cha machozi kunilengalenga. Nikaona labda haikuwa bahati yangu kufanya kazi katika taasisi hiyo.