PreGE2025 Hili ndilo shtaka la Tundu Lissu

PreGE2025 Hili ndilo shtaka la Tundu Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Tuna DPP mjinga sn, uchaguzi upi hapo umetajwa wa TFF au CHADEMA? hovyo kabisa japo baadae atafuta hakuna la maana
Baada ya Lissu kuona mna hizi akili, kaamua kuchukua chake mapema awaachie huo uchaguzi was TFF mhangaike nao. Baada ya uchaguzi anatimua zake ubelgiji. Lissu genius kweli.
 
Baada ya Lissu kuona mna hizi akili, kaamua kuchukua chake mapema awaachie huo uchaguzi was TFF mhangaike nao. Baada ya uchaguzi anatimua zake ubelgiji. Lissu genius kweli.
Lakini mumeo si tutapiga naye kura au naye atatuacha?
 
Propaganda is real

Wanapalilia moto kwa juu
 
Inasikitisha sana

Anyway, JPM alisingiziwa mabaya mengi 😎
Kwani magu alikinukisha vibaya sana? Alileta uasi?

Domo needs to learn nchi Lazima iwe na mifumo ya kudhibiti mihemuko na mitopolo ya hisia… the country ingeshakua Kama Congo of everyone angenukisha na kuasi

Kuna mambo hata Kama Unataka kuyafanya kamwe usiropoke

Domokaya linampoza domo lake, likishapanda mzuka linakosa kwbisa filter za upeo na busara
 
Hapo kama wanataka kubalance mambo wampe na Mwenezi Kesi maana alitoa pia taarifa za uongo.Taarifa ya kutoa taharuki kwa kusema CDM wataleta MPOX &EBOLA.
Hawa jamaa Wana double standard.
 
Hili jeshi letu la Polisi sijui linaongozwa na watu wa aina gani? Sasa uhaini aliofanya Tundu Lissu uko wapi?

Kuhamasisha watu kuwa watazuia uchaguzi wa October 2025 ni uhaini? Kwani kuna uchaguzi ambao umezuiwa? Sasa huo uhaini wanautafsiri vipi? Ni kipi alichofanya? Amehamasisha mapinduzi kwenye mikitano aliyohutubia? Na huo uchaguzi usipofanyika kwa sababu nyingine itakuwa pia ni uhaini?

Hili jeshi la Polisi na ofisi ya DPP wana watendaji wa aina gani? Yani vijishtaka vya ajabu ajabu na posho za walipa kodi wanapewa kabisa.
Jwa hiyo mropokaji atishie uasi hadharani halafu jeshi la polisi likae kimya? Hapo tutakua na nchi kweli? Katika hili Mropokaji kateleza.
 
Hili jeshi letu la Polisi sijui linaongozwa na watu wa aina gani? Sasa uhaini aliofanya Tundu Lissu uko wapi?

Kuhamasisha watu kuwa watazuia uchaguzi wa October 2025 ni uhaini? Kwani kuna uchaguzi ambao umezuiwa? Sasa huo uhaini wanautafsiri vipi? Ni kipi alichofanya? Amehamasisha mapinduzi kwenye mikitano aliyohutubia? Na huo uchaguzi usipofanyika kwa sababu nyingine itakuwa pia ni uhaini?

Hili jeshi la Polisi na ofisi ya DPP wana watendaji wa aina gani? Yani vijishtaka vya ajabu ajabu na posho za walipa kodi wanapewa kabisa.
Walaaniwe Hawa watu na kabineti Yao...
 
Wanabodi,

Kama kawa, kila nipatapo fursa


Kufuatia tishio la matamshi yenye viashiria vya uhaini dhidi ya serikali ya JMT kwa baadhi ya watu, na watu hao kushikiliwa na vyombo vya dola, waneibuka watu, mashirika, wanaharakati kupigia kelele kuna kesi ya uhaini, na hadi baadhi ya taasisi za kimataifa kutaka kuingilia kati mambo yetu ya ndani!, hivyo kufuatia mwandishi wa makala hizi kuwa pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, naomba kuitumia makala ya leo, kuanza mfululizo wa makala elimishi kuelimisha umma kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu kwa jicho la mtunga katiba.

Naomba nianze na elimu fupi kuhusu makosa mawili makubwa kuliko makosa yote kwenye katiba yetu. Makosa haya ni kosa la kuua, (murder), na kosa la uhaini, (treason), ambayo yote adhabu yake ni kifo, au "capital punishment", na kwa Tanzania adhabu hii inatekelezwa kwa kunyongwa hadi kufa, kwa nchi yetu tuna gereza moja tuu la kunyongea ni gereza la Isanga, liko Dodoma.

Uhaini ni nini? Uhaini umetajwa kwenye sura ya Saba kifungu cha 39 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, yaani penal code kinasema Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais.

Kwa mujibu wa sheria tuliofundishwa darasani, uhaini ni vitendo na sio kauli ni uchochezi!. Kwa vile mpaka sasa hakuna mashitaka yoyote ya uhaini yaliyofunguliwa katika Mahakama yoyote, nawaombeni Watanzania wenzangu tusishabikie uzushi wa uhaini, hili sio jambo la kheri hata kidogo.

Vivyo hivyo kwenye jinai ya uhaini, sio kila matamshi ya uhaini ni uhaini, ili kuwepo kwa jinai ya uhaini, lazima kuwepo kwa zile sifa kuu mbili, actus reus na mens rea ya kupanga kufanya uhaini. Kitendo cha mtu ameghafilika tuu na hoja za Club House, akaanza kuhororoja kutoa matamshi ya kupindua serikali, haimaanishi ni uhaini wa kupindua kweli serikali, lakini matamshi hayo yanaweza kuwa ni matamshi ya uchochezi hivyo kusababisha watu wapange kweli kupindua serikali, lakini matamshi tuu kama matamshi bila ya kuwepo means rea ya kupindua serikali, watu hao watakuwa wamefanya kosa la sedition na sio treason.

Wasalaam
Paskali
NB. Jamhuri inaweza kubadili, kuongeza au kurekebisha shtaka hilo kwa mujibu wa Sheria.
Asante kwa kutuletea hii, hakuna uhaini wowote hapo kwa mujibu wa sheria tulifundishwa sisi!. Uhaini My God!. Kuna Uwezekano Anadanganywa na Kadanganyika? I Don't Believe This!. Sitatizwi na Uongo Wao, Natatizwa na The Motives Behind Such Lies! Pia soma Ijue Katiba ya JMT kwa Jicho la Mtunga Katiba: Watanzania Tusishabikie Uhaini. Hukuna Uhaini wa Kauli na Maneno, Uhaini ni Mipango na Matendo

P
 
Hawa jamaa Wana double standard.
Uzushi na uhaini ni sawa ?

Walipozusha chair kala sukari kuna mtu alihangaika nao?

Uasi ni treason na Haina msamaha

Mfundisheni kudhibiti kamudomo
 
Back
Top Bottom