Leo Waziri wa TAMISEMI ametangaza matokeo ya vijana waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza, ambapo zaidi ya wanafunzi 74,000 wamekosa nafasi kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa.
Jambo hili linasikitisha na kuhuzunisha sana maana sasa limekuwa wimbo wa taifa, kila wamalizapo wanafunzi ni lazima wengine wabaki kutokana na uhaba wa Vyumba vya Madarasa, hii inadhihirisha namna serikali ilivyojaa ubabaishaji na uzembe.
Hivi serikali inashindwa kuandaa vyumba vya kutosha mapema ili wanafunzi hawa wajiunge kwa pamoja pasipo kuwasubirisha, hivi kama tatizo dogo kama hili limewashinda wataweza yale makubwa kweli?
Hili linatia aibu na kuonesha namna tusivyokuwa makini na elimu ya watoto wetu.
Jambo hili linasikitisha na kuhuzunisha sana maana sasa limekuwa wimbo wa taifa, kila wamalizapo wanafunzi ni lazima wengine wabaki kutokana na uhaba wa Vyumba vya Madarasa, hii inadhihirisha namna serikali ilivyojaa ubabaishaji na uzembe.
Hivi serikali inashindwa kuandaa vyumba vya kutosha mapema ili wanafunzi hawa wajiunge kwa pamoja pasipo kuwasubirisha, hivi kama tatizo dogo kama hili limewashinda wataweza yale makubwa kweli?
Hili linatia aibu na kuonesha namna tusivyokuwa makini na elimu ya watoto wetu.