Hili la kuchinja lisitugawe, Linazungumzika

Hili la kuchinja lisitugawe, Linazungumzika

hivi wafanya biashara wa nyama wamelalamika? mi nadhani kelele za vyura hazizuii tembo kunywa maji
 
Nani kakudanganya kuwa kuchinja ni ibada kwa waislamu? Toa ushahidi. Kwa taarifa yako hakuna uhusiano wa ibada na kuchinja kwa sababu hakuna sehemu yoyote katika qurani inayoamrisha ibada ya kuchinja. Pengine watu wanachanganya kitendo cha kuchinja wakati wa Idd el Hajj na kuchinja katika siku zingine. Kuchinja huwa ni ibada kwa siku hii tu na tena imeamrishwa kwa kila mtu mzima mwenye uwezo na siyo watu maalum. Kwa hiyo ni upotoshaji wenye nia ovu kudai kuwa kuchinja ni ibada kwa waislam.
Mnatuchanganya sasa, kwa hiyo siku ambazo si eid, nani anaruhusiwa kuchinja? Yeyote au?
 
Huu ni ukuwaji wa uchochezi wa kidini Tz.. sijui tunaenda wapi... ila kwa upande wangu sioni shida kuchinjiwa na mwisilamu..
 
Mnatuchanganya sasa, kwa hiyo siku ambazo si eid, nani anaruhusiwa kuchinja? Yeyote au?

Huna haja ya kuchanganyikiwa. Issue hapa ni ukweli kwamba kuchinja sio ibada ya kiislamu. Bali ni utaratibu wa kijamii kuthaminiana na kuheshimiana. Kwamba wakati mkristo hazuiwi kula mnyama aliyechinjwa na mtu yeyote, kwa waislam ni kinyume chake.
 
mkuu hizi ni inshu za kiimani na dini hizi ni tofauti kila mtu ana imani yake wakristo wana haki ya kulijadili hili
 
Me sina shida na habari za kuchinja, nachinja mwenyewe kuku nyumbani kwangu, na nikifikia hatua ya kuchinja mbuzi na ng'ombe nitafanya hivyo, muislamu akija kwangu akiuliza nani kachinja nitajibu kuwa ni mm, kama hatokula, faida kwangu. Sioni sababu ya kupigizana kelele kwa suala ya kuchinja nyama, tuna mambo mengi ya msingi ambayo tungeliweza kujadili na kuyatolea ufafanuzi kwa manufaaa ya taifa letu na kizazi kujacho. Shame on all of us!!
 
Tatizo siyo waislam kuchinja ndugu yangu, bali kwao ni ibada sasa wanatulisha vitu vilivyofanyiwa ibada tofauti na misingi ya imani yetu. Hapo ndipo tumepata utata kwamba kumbe kulikuwa na ibada nyuma ya kuchinja huko.

wewe ndugu yangu unataka kushirikishwa ibada usiyo ijua kwa sababu ya kuogopa mauaji ya kimbari ? mwanzoni hata mm sikuona tatizo kwani niliona ni utaratibu tu, lakini hii ya kwamba ni ibada! hiii ni hatari kwa Mungu, sikubali kushirikishwa ibada nisiyo ijua.
 
Me sina shida na habari za kuchinja, nachinja mwenyewe kuku nyumbani kwangu, na nikifikia hatua ya kuchinja mbuzi na ng'ombe nitafanya hivyo, muislamu akija kwangu akiuliza nani kachinja nitajibu kuwa ni mm, kama hatokula, faida kwangu. Sioni sababu ya kupigizana kelele kwa suala ya kuchinja nyama, tuna mambo mengi ya msingi ambayo tungeliweza kujadili na kuyatolea ufafanuzi kwa manufaaa ya taifa letu na kizazi kujacho. Shame on all of us!!

hongera kwa ujumbe mzuri.
 
Waafrika upuuzi wa kushadadia dini za watu wataacha lini?

I mean its not even about the Songhai bantu vs the bantu migrants.
 
Ibada gani kusema alahuu wakbaru maana yake mungu mkubwa kwani wakristo wanavyo chinja usemaje?tusiwe tuna tafuta sababu za kukosana.miaka nenda rudi waislamu ndio wachinjaji hii mambo ya ccm kutugawa kusema cdm ni chama cha wakristo matokeo yake ndio haya cdm hawataki kuchinjiwa na ccm ambao ndio wanajidai waislamu safi.

kweli we chizi hadi hii umepeleka katika itikadi ya vyama! Staili hii hatujengi kitu hapa
 
Tatizo siyo waislam kuchinja ndugu yangu, bali kwao ni ibada sasa wanatulisha vitu vilivyofanyiwa ibada tofauti na misingi ya imani yetu. Hapo ndipo tumepata utata kwamba kumbe kulikuwa na ibada nyuma ya kuchinja huko.

Hee kuchinja imekuwa ibada tena, hii mpya kwangu ijapokuwa ni mwislamu!
 
nawapenda sana wachina,hawana mambo haya na hawana dini na nchi inakwenda kiuchumi,sisi tuna dini,makabira na mambo mengi sana na bado tupo nyuma kwa kila kitu,vita sisi,ubaguzi wa dini sisi,ubaguzi wa makabira sisi,huku safi hakuna anayekuuliza dini yako wala kabila lako,unaulizwa kuhusu wapi unalala na nini unakula.
kwa hili hakuna cha muhimu tutakacho kipata zaidi ya kuja kupigana baadae ili apatikane mshindi.
hapa haluna cha ibada ya nani wala ya yule,maisha yanakwenda.
kwanini msiishi kama wahadhabe tu tujue moja,kuliko kutumia muda mwingi kulumbana pasi ya kufanya kazi zenye kuwaletea maendeleo?
 
mimi nasema ni upuuzi kwan wakichinja waislamu tukala sisi wakristo tatizo nini? Au tutapungukiwa na nini? Nacho weza sema hapa ni kwamba siku hizi hawa viongozi wetu wa dini wameweka ushabiki mbele sana bila kuangalia mambo ya msingi ambayo wanaweza yafanya au kuwafundisha waumini wao na wakauona ufalme wa mbingu
 
Huna haja ya kuchanganyikiwa. Issue hapa ni ukweli kwamba kuchinja sio ibada ya kiislamu. Bali ni utaratibu wa kijamii kuthaminiana na kuheshimiana. Kwamba wakati mkristo hazuiwi kula mnyama aliyechinjwa na mtu yeyote, kwa wai
slam ni kinyume chake.
Jibu swali, kuchinja kwa waislamu ni ibada au siyo ibada? Maana ugomvi upo hapo tu...
 
Kwanini tatizo hili lianze mwaka 2013?
Siku nyingine hakuna uchinjaji uliofanyika?
Ina maana masomo na kazi za uchinjaji zinatakiwa kufanywa na waislam tu?
Vyuo vinavyotoa kozi za wachinjaji waulize dini kabla ya kumruhusu mtu kujiunga kusoma?
Serikali inajenga machinjio ili kuajiri wachinjaji waislamu pekee?
Je bidhaa nyingi za nyama zisizo na nembo ya " kuhalalishwa kiislamu (halal), mbona zimeliwa kwa miongo na waislamu?

Je samaki wanatakiwa " kuvuliwa kiislamu"?
Senene, kumbikumbi n.k. navyo vinaandaliwa kiislamu?

Pamoja na haya kuna maswali mengi zaidi yasiyo na majibu NA KWA HAKIKA WALIOPANDA MBEGU HII HAWATATOKA BURE BILA KUDHURIKA NA MAZAO YAKE.
 
Back
Top Bottom