mwananchit
JF-Expert Member
- Oct 13, 2008
- 242
- 298
Ndugu zangu wakristo, hii vita ya nani achinje tusiichukulie kijuujuu kana kwamba ni vita ya kimwili bali ni ya kiroho na Biblia iko wazi kabisa juu ya jinsi ya kupigana vita za kiroho. Mtume Paulo katika 2Wakorintho 10:2-5 atatuasa hivi:-
2 Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu
3 Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo
4 Silaha za vita vyetu si za mwili, Bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome
5 Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu na tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo
Wakristo kwa kuanzisha mabucha yetu ni kwamba tunapigana vita sahihi ila kwa njia isiyo sahihi, hii vita ipo katika ulimwengu wa roho na si vinginevyo.
Hivi mtu yeyote akichinja vyovyote anavyoona inafaa na akaelekeza shingo ya mnyama uelekeo wowote na akatamka maneno yoyote inakudhuru nini ndugu yangu mkiristo? Hebu tumalizie kwa kusoma maneno aliyotuambiaBwana Yesu baada ya kuyashinda mauti katika Injili ya Marko 16:17-18
17 Nazo ishara hizi zitafuatana na wale waaminio: Kwa jina langu watatoa pepo wachafu, watasema kwa lugha mpya,
18 Watashika nyoka kwa mikono yao na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe, wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.
Kwa kumalizia, hii vita ya kimwili ya nani achinje ni mkakati maalum wa Shetani wa wa kutukosanisha na ndugu zetu Waislam kwa kutupiganisha vita kwa njia mbadala ambapo kushindwa ni lazima. Hakuna mahali popote katika agano jipya ambapo tunafundishwa jino kwa jino au kupigana vita ya kiroho kwa njia za kimwili. KAMA VILE AMBAVYO HAUNUNUI NGUO MPYA NA KUANZA KUIVAA BILA YA KUIWEKEA MIKONO KWANZA, VIVYO HIVYO WEWE NENDA BUCHA YOYOTE NA UNUNUE NYAMA YAKO, IWEKEE MIKONO IKIWA MBICHI AU MBIVU, MSHUKURU MUNGU HALAFU KULA! SASA HAPO KUNA HAJA YA KUGOMBANIA MACHINJIO KWELI? HEBU TUWAACHIE NDUGU ZETU WAISLAM JUKUMU LAO LA KIHISTORIA LA KUTUCHINJIA KITOWEO! Natanguliza shukrani kwa kunielewa.
2 Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu
3 Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo
4 Silaha za vita vyetu si za mwili, Bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome
5 Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu na tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo
Wakristo kwa kuanzisha mabucha yetu ni kwamba tunapigana vita sahihi ila kwa njia isiyo sahihi, hii vita ipo katika ulimwengu wa roho na si vinginevyo.
Hivi mtu yeyote akichinja vyovyote anavyoona inafaa na akaelekeza shingo ya mnyama uelekeo wowote na akatamka maneno yoyote inakudhuru nini ndugu yangu mkiristo? Hebu tumalizie kwa kusoma maneno aliyotuambiaBwana Yesu baada ya kuyashinda mauti katika Injili ya Marko 16:17-18
17 Nazo ishara hizi zitafuatana na wale waaminio: Kwa jina langu watatoa pepo wachafu, watasema kwa lugha mpya,
18 Watashika nyoka kwa mikono yao na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe, wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.
Kwa kumalizia, hii vita ya kimwili ya nani achinje ni mkakati maalum wa Shetani wa wa kutukosanisha na ndugu zetu Waislam kwa kutupiganisha vita kwa njia mbadala ambapo kushindwa ni lazima. Hakuna mahali popote katika agano jipya ambapo tunafundishwa jino kwa jino au kupigana vita ya kiroho kwa njia za kimwili. KAMA VILE AMBAVYO HAUNUNUI NGUO MPYA NA KUANZA KUIVAA BILA YA KUIWEKEA MIKONO KWANZA, VIVYO HIVYO WEWE NENDA BUCHA YOYOTE NA UNUNUE NYAMA YAKO, IWEKEE MIKONO IKIWA MBICHI AU MBIVU, MSHUKURU MUNGU HALAFU KULA! SASA HAPO KUNA HAJA YA KUGOMBANIA MACHINJIO KWELI? HEBU TUWAACHIE NDUGU ZETU WAISLAM JUKUMU LAO LA KIHISTORIA LA KUTUCHINJIA KITOWEO! Natanguliza shukrani kwa kunielewa.