Hili la kuchinja lisitugawe, Linazungumzika

Hili la kuchinja lisitugawe, Linazungumzika

Ukiwa mtu wa kudaidai tu unajiweka kwenye kundi la watu wanaolaumu wenzao kila siku kwa matatizo yao. Kila siku udhaifu wako utakuwa unamtafuta aliyesababisha we uwe dhaifu katika jambo hilo...
 
Ambacho nimejifunza katika mijadala hii ni kuwa masuala ya udini ni extra sensitive issue katika jamii yetu. Tume ya katiba inatakiwa kuwa makini sana na masuala haya katika kuandika rasimu ya Katiba. Bado tunataka taifa ambalo ni secular bila kuwa na vipengere vinavyotaja dini yoyote. Mambo ya kidini yatamkwe wazi kuwa yatafanywa na kila dini kivyakevyake bila kuhusisha dola. Vinginevyo mambo kama mahakama ya ksdhi n.k. yatalipua taifa!!
 
Hakuna cha ibada wala nini.

La muhimu ni kwamba kwa mnyama asiyechinjwa kiislamu basi wenye mabucha watajipunguzia wateja.

Na waandike tu kwamba bucha hii nyama yake siyo halali basi nasi tutawacha kununua tutatafuta bucha nyengine.

Si unaona mfano Uingereza nyama zinazochinjwa kihalali basi huandikwa tu 'halaal meat', yamekwisha!
 
Vita vyetu si juu ya damu na nyama bali ni juu ya falme na mamlaka ukiona mkristo anapigia kelele ilo ni mkristo wa minofu tu huyo
 
Vita vyetu si juu ya damu na nyama bali ni juu ya falme na mamlaka ukiona mkristo anapigia kelele ilo ni mkristo wa minofu tu huyo
Halafu kote kulikotokea vulugu, shughuri ilikuwa ya wakristu, mnyama wa wakristu na mchinjaji mkristu..... Tena kwingine walitaarifiwa kuwa kuna samaki hivyo asiyekula nyama iliyochinjwa na mkristu basi ale samaki, lakini waligoma... SASA HAPO NDO UTAONA NANI NI WA MINOFU
 
Mkuu sisi hatubaguani wala wakristo hatuna nia mbaya...tatizo wenzetu kufika pointi wakaona wana haki ya kuchinja kisheria na ukijichinjia kamnyama kako hata kama ni msiba wako nyumbani wanakushitaki kwa barua tena BAKWATA huoni kuwa ni kuingiliana uhuru wa maisha....Kwani ni wapi Mkristo kakatazwa kuchinja ???
 
Waafrika upuuzi wa kushadadia dini za watu wataacha lini?

I mean its not even about the Songhai bantu vs the bantu migrants.

ImageUploadedByJamiiForums1359926085.750959.jpg
.........
 
Tatizo siyo waislam kuchinja ndugu yangu, bali kwao ni ibada sasa wanatulisha vitu vilivyofanyiwa ibada tofauti na misingi ya imani yetu. Hapo ndipo tumepata utata kwamba kumbe kulikuwa na ibada nyuma ya kuchinja huko.

una uhakika?
 
Nimekuwa nikifuatilia sakata la nani achinje nyama kule Mwanza, na nimebaki kushikwa na butwaa.

Jamani, nadhani tumesahau mauwaji ya kimbari kule Rwanda na sisi tunatamani kuchinjana wenyewe kwa wenyewe.

Ni jambo linanishangaza nakutokuelewa mim ni mkristo na sion ubaya wa muislam kuchinja kutokana na utamaduni tumeuzowea kuwa waislam ndio wanachinja na pasipo katiba kusema mahali popote na mimi sioni ubaya.

Jamani mbona haya ni mambo ya tangu miaka mingi na haijawahi kuonekana mtu akilalamika imekuwaje ghafla tunataka kuchinja liwe swala la katiba. Jamani hili ni taifa moja na tu wamoja tusianze kubaguwana kwa udini na ukabila maana hakika hakuna atakaye pona.

Yatupasa kumuomba Mungu na kuishi ktk hali ya umoja na upendo kama taifa moja chini ya Rais mmoja. Tusibaguwane wala viongozi wa dini tusiwe wachochezi na ikiwezekana hao wakristo wakaondoe kesi mahakamani.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake..

Mkuu nahofu sana na hawa watu kwanini wanataka kuleta migogoro ya dini?
 
Halafu kote kulikotokea vulugu, shughuri ilikuwa ya wakristu, mnyama wa wakristu na mchinjaji mkristu..... Tena kwingine walitaarifiwa kuwa kuna samaki hivyo asiyekula nyama iliyochinjwa na mkristu basi ale samaki, lakini waligoma... SASA HAPO NDO UTAONA NANI NI WA MINOFU


Hivo eeeeh??

Kwaiyo sasa,sisi Maustadhi hatukutaka kitu cha ubwabwa samaki badale yake tukademand kitu cha Ubwabwa na Nyama Sio??

lol,kaazi kweri kweri..!
lakin tutafika tuuh..
:madgrin:
 
Watanzania tuwe macho na tuepuke mitego ya kijinga. Swala la kuchinja si issue ya kutupotezea muda waanzilishi wa ujinga huu wana lao jambo. Na kwa kiasi kikubwa wamekwishafanikiwa ni janja ya watu fulani wenye malengo ya kuivuruga Mwanza ili watu waanze kufikiria mambo ya imani za kidini badala ya mambo ya maendeleo. Hivi wote munaong'ang'ania kuchinja ni haki yenu tueleze ni sheria gani ya Tanzania imewaruhusu? Kama ibada kaswalie/kasalie nyumbani kwako si machinjioni. Ningeshauri wanaMwanza wadharau wajinga wote wanaotaka kufanya jambo la kuchinja kuwa issue. Kumaliza ubishi watafutwe wasiokuwa wakristu wala waislamu ndo watuchinjie nyama asiyetaka asile. Acha kutuzengua na imani zenu za kudandia kwani nyie ni waarabu au wazungu? Hizo dini si zenu bali kinachowasumbua ulimbukeni tu. Tangu lini mukasikia watu wanagombania jambo hili huko zilikoanzishwa dini hizi?
 
Tatizo siyo waislam kuchinja
ndugu yangu, bali kwao ni ibada sasa wanatulisha vitu vilivyofanyiwa
ibada tofauti na misingi ya imani yetu. Hapo ndipo tumepata utata kwamba
kumbe kulikuwa na ibada nyuma ya kuchinja huko.

Mdau35, kwani umekula nyama hizo kwa muda gani toka uzaliwe? na hicho unchodai ibada, ulikuwa unakichukuliaje mpaka leo ujifanye ndio habari mpya kwako?
 
Last edited by a moderator:
Kwa taarifa yako mimi huwa sili red meat, ninazokula zote nina uhakika na uchinjaji wake.
Mdau35, kwani umekula nyama hizo kwa muda gani toka uzaliwe? na hicho unchodai ibada, ulikuwa unakichukuliaje mpaka leo ujifanye ndio habari mpya kwako?
 
Last edited by a moderator:
Usibishe kilicho wazi, watumie maneno yoyote yale, mwisho wa siku kwa waislamu kuchinja kwao ni ibada.....kama mkristu, kushiriki ibadaya kiislamu haitakiwi.

unalazimisha na ushapewa jawabu au unaelewa sana bila ya kuskiliza imekuwa tatizo sasa kama mkee anayetafuta talaka hana suluhu moyon mwake....
 
hivi wafanya biashara wa nyama wamelalamika? mi nadhani kelele za vyura hazizuii tembo kunywa maji

nashangaa hi inadhirisha uadui mkubwa unatafuta penye ufaa tu..naogopa hata mtuuuu mmoja akiljilipua hakuta kalika tena hapa
 
Hivyi kule Ulaya na Marekani dini gani wanachinja kule eti? labda mashine inachinja au? hivyi machinjio ya kisasa nasikia ndo nini kama bado yanategemea mtu achinje? waziri wa mifugo waulizie wenzio nchi zilizoendelea wanachinja vipi? halafu atapost hapa jf eti.
 
Back
Top Bottom