Tunahitaji utaifa wetu zaidi ya chochote, kwa maana nikutokana na mshikamano, umoja na amani heshima itapatikana.
Tukianza kugawana mabucha tutagawana mpaka mitaa ya kuishi, mwisho wa mgawanyo huu ni maudhi na kuangamia kwa taifa letu.
Hayati JK Nyerere hakupenda kabisa kuona watu wake wanagawanyika kwa maana yoyote ile, sio tu alipinga ubaguzi wa dini majukwaani alimaanisha ndiyo maana hapakuwa na mambo ya kipuuzi kama haya tuyaonayo sasahivi. wengi wetu tunambeza sana mwalim lakini hii mitafaruku itawakumbusha, kwanini hatukutofautina wakati ule tunatofautiana sasa hivi?
Kikwete amelala sana, ameacha watu kuhubiri matusi, kibaya zaidi Rais na serikali yake wameacha wachochezi wamemwaga sumu, chuki, kashifa na kujenga matabaka bila kukemewa kiasi kwamba sasa kila mmoja anajiona bora zaidi ya mwingine.
-Kwanini mkristo asihubiri imani yake kutoka kitabu chake kitakatifu (Biblia) na ishie humo, kunasababu gani kuchambua kitabu cha dini nyingine? kunafaida gani kuongelea imani zingine. (watawala wakaliacha hili haya ndiyo matokeo-kuvunja utanzania wetu)
-Kwanini mwislam asihubiri imani yake kutoka kitabu chake kitukufu (koraan) na ishie humo, kunasababu gani kuchambua kitabu cha dini nyingine? kunafaida gani kuongelea imani zingine. (watawala wakaliacha hili haya ndiyo matokeo-kuvunja utanzania wetu)
Sasa kila mtu ameamka anadai haki yake, tunaelekea wapi? kikwete na ccm yake wapo wapi? Nyumba yetu inateketea kwa urafi wa madaraka, hawawezi kuwakemea wazi wazi waumini wa hizi dini mbili kama alivofanya mwalimu, alikuwa hodali sana ndio maana tumefika hapa tulipo kwa amani, hakuacha wachochezi kuharibu vichwa vya watanzania. Walioachiwa kijiti wameshindwa kabisa cha ajabu bado kuna watu wanamlalamikia Nyerere jaman wakati wake tuliishi salama na wote tuliitana ndugu.
Jambo la msingi kwetu sote ilikuliepusha taifa na maafa
1. Wakristu walejelee walivoishi na waislam siku za nyuma, mwislam achinje ili sote tujumuike pamoja katika meza na kuishi kama wanadamu ( Sio najisi kimuingiacho mtu kinywani bali kitokacho kinywani, hicho kitamtia unajisi-wivu, kijicho, uzinzi, wizi, ubakaji, ......maana haya yanatoka katika mawazo yetu) Inapofikia suala kitimoto na vinginevyo wakristu wanaovitumia wawe na staha, pia hekima hunasababu ya kusababisha maudhi kwa mtu mwingine.
2. Waislam wajenge utulivu na staha, wapatane na jirani zao kwa maana amani hupatikana kutoka mioyo minyenyekevu. Watanzania wameishi kwa miaka mingi bila misuguano ya kidini nini kimetokea sasa hata tuchukiane?
Hakuna sababu ya kugombania fito wote tunaishi tanzania, tunajenga tanzania na tukiichoma tanzania tutaenda wapiii?!