Hili la January Makamba ni hatari zaidi

Mkuu nimekusoma nashukuru sana. Nikuombe niongeze kuwa ni aibu mtu au watu kuwa chanzo cha kutokuelewana kwa kisingizio cha dini kwani kama ulivyosema Yesu na Mohamed hawakuja kuanzisha dini.
 
Niseme kuwa katika wagombea wa CCM angalau January katoa 'picha' atakuwa Rais wa namna gani akiweza kufika.....wengine wengi hatujui misimamo yao ya mambo mengi.

Sasa leo katika hotuba yake ya kutangaza nia January kazungumzia 'ufa wa kidini'na kwa mawazo yake akipewa Urais basi ataunda 'baraza maalum la viongozi wa dini'eti kazi yao iwe kukutana kila baada ya miezi miwili na kujadili namna 'ya kutunza amani'na kuondoa huo mgawanyiko wa kidini.

Binafsi naona likifanyika hilo ndio nchi itaingia kwenye mgawanyiko mkubwa zaidi wa kidini umoja wa watanzania, amani upendo na mshikamano haupo sababu ya viongozi wa kidini.

Watanzania wengi wamechanganya dini kwenye familia zao na wanashirikiana vizuri tu kuanzisha Taasisi zitakazo wapa sauti viongozi wa kidini ndio itakuwa 'platform' ya wao ku manipulate 'their influences' na ku gain more voice za kuwagawa wananchi.

Kinachohitajika ni kuwaacha na kuwa na serikali ambayo haiwapi sauti yoyote ile kwenye masuala ya kitaiifa.....'Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi' na viongozi wa dini waondolewe kwenye 'National Affairs' completely.

Tuache kabisa kushirikisha shughuli za kidini na za viongozi wa kitaifa...Sherehe zote za kidini zibaki kuwa za kidini na viongozi wa kitaifa hasa wa serikali.

Wasihusike na wala wasiende kwenda kuhutubbia masuala ya kitaifa ndani ya misikiti na makanisa.

Kama tuko serious na kutenganisha dini na siasa....basi tusiruhusu hizi idea za January kupewa nafasi.

Mawazo ya January kwa juu yanaonekana mazuri sana lakini kiukweli ni mawazo hatari sana sababu yatazidi kuwapa nguvu isiyo ya lazima viongozi wa kidini.

Watu kama Gwajima watajikuta wanapewa 'umuhimu wa kitaifa' usio na lazima kwa kupitia vyombo kama hivyo ambavyo January anataka kushawishi viwepo.

Dini ibaki kuwa ni jambo la mtu binafsi na viongozi wa dini waachwe huko huko kwenye mimbari za dini zao.

Mimi nakumbuka vizuri katika hotuba yake alimalizia kwa kusema atakuwa tayari kupokea mawazo mapya ya kuboresha serikali yake. Nadhani kwa hili pekee linatoa room ya kufanya maboresho ya mambo yote yenye mapungufu. Otherwise the guy is the best candidate!
 
Imenishangaza hiyo kauli....

Huwa nashangaa sana mfano eti kumsimika askofu rais au wazir mkuu anakuwa mgeni rasmi. Baraza la Idd eti rais au wazir mkuu anakuwa mgeni rasmi. Ajabu sana. Wakati mwingine unakuta huyo kiongozo wa serikali wala sio wa hiyo dini!
Naungana na Biss dini ziachwe zifanymbo yao. Kuna watz wengi sana hawajihusishi seriusly na mambo ya dini. Sasa kuleta mambo ya kuanza kufanya watu walazinike kuniidentify na dini si vizuri.
Mimi nadhan hawa wagombea wangeahidi kuhakikisha wanaidanya Tz iwe ya kisekula kwelikweli. Wabuni vitu vya kuwafanya watz kujisikia wamoja zaidi kuliko kuchokujaribu kuwapaisha viongozi wa dini.
Mfano mzuri ni kufufua mila za asili nakidogokidogo ili kudecolonize mind za watz.
 
Nadhani ccm wanatakiwa kucopy na kupaste mawaze yake na muhongo kuandaa ilani yao...january kaonyesha uozo wamserikali ya sasa
 
Umenifurahisha kupapasa jipu. Ni kweli we need to decolonise our minds. Nani asiyejua dini zetu hizi ni sehemu ya utamaduni wa jamii husika. Hivi wewe na mimi ngozi zetu nyeusi tulikuwa tunatambika na kupendana bila kuichukia miungu ambayo babu zetu walikuwa wanaiamini. Sasa inashindikana nini kuhuisha mambo mazuri ya mitume wa nje na wetu ili dunia iwe mahali pazuri zaidi pa kuishi? Waafrka tujiamini tupendane. Matatizo yetu ni mengi mno. Njaa .umaskini. Ukimwi, ujinga,uigaji, uchepukaji nk. Hili la dini tumwachie mtu na Mungu wake. Jehanam na pepo bado hazijajaa
 
Mkuu you have a point lakini tusijilinganishe sisi na wajerumani. Wewe fikiria tu zile propaganda za kuwa CUF au CDM ni vyama vya kidini zilivyokuwa na negative impact kwenye jamii yetu sasa ndio imagine tungekuwa na chama kabisa chenye mrengo wa kidini sasa hivi Tanzania si ingelishakuwa vipandevipande?

Hapana, sijasema tuwe na vyama vya kidini ila nimeongelea umuhimu wa dini katika jamii. Dini ni sehemu ya maisha yetu na haiwezi epukika. Mfano wa Markel nilitaka nikuonyeshe ktk picha kubwa.


Naungana na The Boss somehow viongozi wa kidini wasiwe wa matamko bali wawe washauri wa serikali maana serikali nayo ina ubabe sana hivyo kunapokuwa na organization zenye influence katika jamii kama hizi serikali inakuwa inafanya maamuzi yake kwa tahadhali

Nakubaliana nawe. Nchi nyingi zilizoendelea mfano Marekani wananchi wakigombana na serikali serikali huwatumia viongozi wa dini kusaidia kuleta amani. Mfano, Ferguson riots, Missouri na Baltimore, Maryland.
 
Last edited by a moderator:
Hii ni mada bora kwa uhai na ustawi wa Taifa la Tanzania na watu wake.

Kuwaweka viongozi wadin kwenye attention nikulipeleka Taifa kuzimu. Madai kadhaa yatazua migogoro hatimae machafuko na mwisho vita kamili.

1. Madai ya migawanyo ya madaraka kwa kuzingatia uwiano wa kidin badala ya taaluma za wahusika yatazuka huko.

2. Madai ya haki za kuchinja yataibukia hukohuko

3. Madai ya usawa wakumiliki resources kwa mitazamo ya din yataibuliwa mf. Mahospital, mashule, miradi nk

4. Madai ya migawanyo ya ruzuku bila kufuata utaratibu wala vigezo yataibuliwa ilmradi kila din ipate.

5. Madai ya kutofuga au kufuga baadhi ya wanyama yataibuliwa hatakama katiba inaruhusu.

6. Madai ya zamu yetu kupata urais siyo din yenu yatazuka nk

Kunamigogoro mingi itaibuka nakulitetemesha Taifa na kufarakanisha mtu na mtu, jiran na jiran, mkowa na mkowa nk.

Hili jambo nilakuliogopa kama ukimwi maana unapoingilia nipatamu sana kwa maambukizi mengi ukiachiambali ajali nk lakin UKIMWI UKIINGIA BALAA, KUTOKA NI MATANGA yaan vilio nakusaga meno.

Tusishabikie na kushangilia kifo tujiweke mbali na madhila balaa na hila za ibilisi. Viongozi wadin waache mbali kabisa na serikali isijingize kubeba gunia lililojaa na lijivuja tindikali aina ya cynide (udin) itatuangamizia Taifa letu.

Hongera The Boss hii ni mada bora na muhim sana kwetu na uhai Taifa kwa ujumla.


Exactly my point..
Viongozi wa dini 'wataanza kudeka' na kudai favor hii na ile
bora kuwaacha huko huko
 
Mkuu kuna mengine tunayachukua kama yalivyo maana ukiingia kwa undani zaidi ya imani za dini utagundua kwamba Yesu hakuwa Mkatoliki wala Mrutheri na hata Muhammad hakuwa Sunni wala Shia bali mcha Mungu, haya madhehebu ya dini tumeanzisha wenyewe na hatari yake ni kubwa toka kuanzishwa kwake hivyo bora kuwepo mawasiliano mazuri baina ya vyombo hivi na serikali kama mshauri. Tunachopinga ni serikali kushirikiana na imani hizi ila huwezi kataza mtu na imani yake utakuwa unaondoa uhuru na haki yake.

Uingereza wameweza tu kukomesha Ugaidi wa IRA kwa kuanzisha mawasiliano bora baina ya vyombo vya dini na serikali. leo wameshindwa kuleta salama huko Mahsariki ya kati kwa sababu serikali zinajaribu kuwasiliana zenyewe dhidi ya dini pasipo kufahamu kwamba chimbuko la misukosuko yote hiyo yote ni mawasiliano mabaya yaliyopo baina ya madhehebu na nasaba zao.

Mahala popote pakisha anza ubaguzi wa aina yoyote iwe dini, Ukabila ama rangi basi ni vizuri sana serikali kuwa karibu na vyombo hivyo, kuwasilikiza na hata kuwashauri juu ya sheria na misngi ilojenga Utaifa wao sio dini zao.


Kuanzisha mawasiliano na viongozi wa dini au kujadili lolote na viongozi wa dini
linaweza kufanyika bila kuunda chombo maalum na kuwapa 'platform'
ya wao kuongeza 'influence' ...katika jamii ambayo hiyo influence inaweza kuwafanya waligawe Taifa
au wengine waanze kudeka.......
 
Kuanzisha mawasiliano na viongozi wa dini au kujadili lolote na viongozi wa dini
linaweza kufanyika bila kuunda chombo maalum na kuwapa 'platform'
ya wao kuongeza 'influence' ...katika jamii ambayo hiyo influence inaweza kuwafanya waligawe Taifa
au wengine waanze kudeka.......
Viongozi wa dini ni wa dini wakideka kwa sababu wanakutana na viongozi wa serikali basi hao sii viongozi wa dini maana wanachaguliwa na waumini wenyewe kuwasilisha hoja zao inapobidi.

Kumbuka hawa viongozi wetu wa dini ndio wachochezi wakubwa wa mambo ya kisiasa katika dunia ya leo hapa tulipofika na kama tusipolitazama swala hilo kwa makini kuweza ku control mafuriko haya kwa kiasi fulani basi inaweza kuleta madhara makubwa zaidi mbeleni. Hoja ya kuwasiliana na viongozi wa dini inahusu uwezo wa serikali ku deal na mafuriko yake. Ukiweza kujua mapema kilichopo kichwani mwa mtu yeyote utaweza kukidhibiti kirahisi. Hii ni mbinu ya Kijasusi..
 
Hivi January aliposema atagawa milioni 50 kwa ila kijiji kwa shughuli za maendeleo aliwaelezea watu hizo hela atazitoa wapi? Na jee atatumia mbnu ani kuhakisha kuwa izo hela znatumika kwa matuizi yaliokusudiwa? Pili amesema atatoa bima ya afya kwa kila Mtanzania na hili liwezekana kwa kuunganisha hii bima na mifuko mbali mbali ya jamii anaweza kulielezea hili?
 
Dah....well said. Big up The Boss.
Huyo jamaa watu wanamuona kama vile ana kichwa juu ya kiwiliwili chake. Hawaoni wala hawajui kabisa kuwa nile ni kikapu tu.
 
Last edited by a moderator:
Hakuna mtu mwingine ndani ya ccm zaidi ya makongoro na p.m wake magufuri.
 
Back
Top Bottom