mahindi hayaoti mjini
JF-Expert Member
- Nov 29, 2022
- 2,488
- 2,979
- Thread starter
- #61
Yaani nisiwe na akili ajili ya kuuliza tu kama chadema ni chama cha kidini?Ndugu, lazima utakuwa na tatizo la akili. Kama ungekuwa na akili timamu lazima ungekujua kuwa hapa Tanzania hakuna chama kinachoungwa mkono au kukataliwa na dini moja.
Kuna wachungaji, manabii, maaskofu na kuna mashekhe pia wanaoimba wimbo wa CCM, 'tulinde amani' (ie hata kama hakuna haki). Kwa uchache, umesikia tamko la Malasusa na shekhe mkuu wa BAKWATA, wakiimba huo wimbo.
Lakini wapo viongozi wa dini, maaskofu, wachungaji, manabii, mashekhe, wanaungana na watanzania walio wengi kuwa huwezi kuongelea Amani, bila kuongrlea HAKI. Hawa wanaungana na wananchi wengi wenye akili timamu, wasio wanafiki, wanaoipenda nchi yao, wanaoona wazi kuwa mifumo yetu ya udhulumaji haki iliyotamalaki kwenye nchi hii, ni tishio kwa amani yetu, tukitaka amani ya kweli ni lazima tufanyie maboresho ya sheria na mifumo inayotengeneza mazingira ya kuwadhumuru wananchi. SHURA YA MAIMAMU, TEC, Maaskofu, wachungaji, manabii na mashekhe, mmoja mmoja wamesimama kwenye msingi huu.
Na hakika, yeyote ambaye hataki kurekebisha na kubora mifumo yetu ambayo ni ya kuwadhulumu wananchi mamalaka yao, ni mashetani na maibilisi wakubwa.
Nchi inataka haki, haitaki kuendelea na ushetani unaofurahiwa na tale maibilisi ya CCM.
Mbona mnaweweseka hivyo? Jibuni swali ni chama cha kidini?