Hii tabia ya viongozi kujifanya special kwenye matukio ya kijamii inanikwaza sana

DodomaTZ

Member
May 20, 2022
71
107
Kuna kitu nimekuwa nikikitafakari kwa muda mrefu, nikahisi yawezekana ni mimi tu fikra zangu ndiyo mbovu au za kizamani, lakini baada ya kumsikia Jaji Warioba akizungumzia suala hilo, nami nimepata nguvu kuamini kuwa ninachowaza kuwa ni tatizo basi inawezekana ni tatizo kweli

Zamani nakumbuka viongozi wengi walikuwa na kawaida ya kwenda sehemu za ibada na katika shughuli za kijamii zao yaani majirani wa mtaa mmoja au mitaa ya karibu.

Hiyo ilikuwa ikifanyika sana tu, na walipokuwa wakifika katika shughuli hizo wengi wao licha ya kuwa walikuwa na majina makubwa, walijishusha na kuwa sehemu ya jamii hiyo na kufanya kile walichotakiwa kukifanya.

Kama ni msibani basi walishiriki kama wananchi wa kawaida lakini bado walipewa heshima yao na wananchi wengine wa kawaida, kama ni kwenye ibada, hivyohivyo hawakuwa na makuu.

Sasa viongozi wengi wa sasa na watu maarufu wa fani tofautitofauti sijui ndio tandawazi au mimi ni mshamba, wengi wao wakishiri lazima watataka wawe watu special hilo eneo husika.

Wengine mbali na kuwa special watataka wapewe nafasi wazungumze, kibaya zaidi wakipewa nafasi hiyo badala ya kuzungumza kile ambacho kimewafanya wawepo hapo, wao wanaleta mada nyingine kabisa za kisiasa.

Hii ni mbaya, inamaana kama mtu kaenda Msikitini au kanisani au kwenye msiba au harusi, wewe kiongozi ukipewa nafasi usitumie nafasi hiyo kutaka kumkwaza mtingine kwa kuingiza sera za uchama au udini wako ambao hauna sababu za msingi.

Mimi hili suala linanikera sana ndio maana kuna wakati nikisikia kiongozi fulani wa kisiasa yupo katika msiba au nyumba fulani ya ibada na ninajua sera zake na mimi zinapishana bora nisiende kabisa hiyo sehemu.
 
Ushamba na kujikweza tu. Hata wasanii wana huu ujinga wakienda misibani. bahati mbaya sana ujinga huu alianzishaga Marehemu Joni na viongozi wa makanisa wakapatwa upofu kumruhusu kila siku.
 
Kuna kitu nimekuwa nikikitafakari kwa muda mrefu, nikahisi yawezekana ni mimi tu fikra zangu ndiyo mbovu au za kizamani, lakini baada ya kumsikia Jaji Warioba akizungumzia suala hilo, nami nimepata nguvu kuamini kuwa ninachowaza kuwa ni tatizo basi inawezekana ni tatizo kweli

Zamani nakumbuka viongozi wengi walikuwa na kawaida ya kwenda sehemu za ibada na katika shughuli za kijamii zao yaani majirani wa mtaa mmoja au mitaa ya karibu.

Hiyo ilikuwa ikifanyika sana tu, na walipokuwa wakifika katika shughuli hizo wengi wao licha ya kuwa walikuwa na majina makubwa, walijishusha na kuwa sehemu ya jamii hiyo na kufanya kile walichotakiwa kukifanya.

Kama ni msibani basi walishiriki kama wananchi wa kawaida lakini bado walipewa heshima yao na wananchi wengine wa kawaida, kama ni kwenye ibada, hivyohivyo hawakuwa na makuu.

Sasa viongozi wengi wa sasa na watu maarufu wa fani tofautitofauti sijui ndio tandawazi au mimi ni mshamba, wengi wao wakishiri lazima watataka wawe watu special hilo eneo husika.

Wengine mbali na kuwa special watataka wapewe nafasi wazungumze, kibaya zaidi wakipewa nafasi hiyo badala ya kuzungumza kile ambacho kimewafanya wawepo hapo, wao wanaleta mada nyingine kabisa za kisiasa.

Hii ni mbaya, inamaana kama mtu kaenda Msikitini au kanisani au kwenye msiba au harusi, wewe kiongozi ukipewa nafasi usitumie nafasi hiyo kutaka kumkwaza mtingine kwa kuingiza sera za uchama au udini wako ambao hauna sababu za msingi.

Mimi hili suala linanikera sana ndio maana kuna wakati nikisikia kiongozi fulani wa kisiasa yupo katika msiba au nyumba fulani ya ibada na ninajua sera zake na mimi zinapishana bora nisiende kabisa hiyo sehemu.

msikitini hakuna nafasi spesho ya mkubwa wote safu moja tu pili huwa hawapati kupewa kuongea ni imamu tu anaeongea
 
msikitini hakuna nafasi spesho ya mkubwa wote safu moja tu pili huwa hawapati kupewa kuongea ni imamu tu anaeongea
Unasemaje?Waziri mkuu Wkt anasema Magufuli Yuko ofisini anachapa kazi,si alisema maneno hayo msikitini?
 
Siku 1 nikakutana na Jerry Muro kijijini kabla hajapewa uDC. Mimi na mwenzangu tukawa hatuna time naye. Akaanza kujitambulisha akiuliza kama tunamjua. Nikamjibu sikujui. Akatuuliza kweni hatufuatilii mpira wa Simba na Yanga? Tukamwambia tunafuatilia ila hatukujui
 
msikitini hakuna nafasi spesho ya mkubwa wote safu moja tu pili huwa hawapati kupewa kuongea ni imamu tu anaeongea
Waziri mkuu Majaliwa alipotudanganya kwa kutuambia magufuli ni mzima na yupo anachapa kazi wakati jiwe keshavuta unakumbuka alizungumza hilo akiwa wapi?
 
Back
Top Bottom