Hii Tabia ya Kupenda ligi barabarani

Hii Tabia ya Kupenda ligi barabarani

Ha ha ha ha ha....
Mbona zamani ilikuwa kawaida, mwaka 98 kabla ya ratiba na tochi Mbeya Dar tumefika saa 8.30 mchana. Na kuna mabasi yalikuwa na uwezo wa kurudi, tatizo lilikuwa askari. Mwaka 2005, Mbeya Dar na Hekima tumeingia Ubungo saa 10 jioni, by saa 4 asubuhi tulikuwa tunakula Ilula, saa 8 mchana tupo Morogoro. Sio story, zamani watu walikuwa wanatembea. Ndio zikaja speed governor, tochi na wakamaliza na ratiba.

Kwa gari binafsi, tushatoka Mbeya 11 jioni tukaingia Dar saa 6 usiku; na kuna siku niko na IT tumetoka Mlandizi saa 5 usiku by 11.30 tuko Mbeya.
Hebu tuandikie wino mate tuweke pembeni, Mbeya -Makambako mlitumia mda gani na hiyo private? Yaani hapo umekimbia hadi mate yamekauka mdomoni nakupa masaa mawili kwa upendeleo! Je Makambako -Dar ulitumia masaa matano?[emoji23][emoji23]
 
Kama unataka ligi unapotoka DAR jaribu kufanya ligi na gari za magazeti ndio utajipima uwezo hao wote uliofuatana nao waoga.
Hahahahaaa... hao jamaa sijui roho yao wanaweka wapi..

Niliwahi kupanda gari la gazeti from dar saa saba usiku, saa kumi na mbili kasoro wako dodoma wana distribute gazeti
 
Wakuu, nimezoea sana kutembea safari ndefu haswa Dar-Kahama-Geita na Dar-Mwanza, mara chache Dar-Bukoba.
Mara nyingi napenda kusafiri jioni au asubuhi sana.

Hizo route nilizozitaja hapo juu hazina Magari madogo mengi usiku, zaidi ya malori na mafuso. So huwa hatujui mambo ya ligi kabisa.

Kuna hii route ya Arusha-Dar na ligi huwa inaanzia pale Njia panda ya Himo, wakuu kuna watu wanapenda kushindana sana, kwenye barabara.

Juzi kati hapa tumetoka Arusha kwenda Dar tulivyofika Pale Njia Panda ya Himo, kulikuwa kuna gari kama tatu ndogo, Mark x nyeupe, Murano moja nyeusi na Alphad ya Silver, plan niliyokuwa nayo nikupoteza muda pale Njia Panda, at least usumbufu upungue barabarani kumbe zile gari zilikuwa zinatafuta abiria wa Dar, mimi kwenye gari ninayoendesha tulikuwa watatu. Sikuwa na wazo la kuchukua abiria.

Ilivyofika saa kumi na mbili kama na nusu hivi yule jamaa wa Alphad akang'oa, baada ya kama dakika kumi, Mark X akang'oa.
Hapo nimepaki upande wa pili wa barabara.

Ukapita tena muda kidogo Murano akang'oa...Tukamaliza mambo yetu tukaanza kuondoka, nilijua nikipiga mashine vizuri nitaenda kuwatoa kabla hata hawajafika Same!!
Tumeanza kutembea sio kwa speed kali hiyo jioni jioni ya saa moja bado watu ni wengi barabarani na mibasi + magari makubwa mengi yakitoka Dar kuja Moshi, Arusha.

Haikuchukua dakika nyingi saana kufika Mwanga, nikaiona ile Murano ndio inaondoka, nikajua labda alikuwa anaongezea abiria, nikawa nimempita mbele kabla ya Kisaranga nikaipita na ile Mark x, Alphad sikuiona. Giza linazidi kuongezeka naona na barabara inapungua jam.

Tumepita Lembeni kwenye Kivuko cha treni jamaa wa Mark X akaovertake kwa speed kali kuianza Tambarare flan hivi kuelekea Same, hapo ndio ikawa shughuli hakuniacha mbali sana, kabla ya sehemu inaitwa mgagao Murano akaniovertake akaenda akaovertake na mark x..

Baada ya Murano kunipita nikagundua Mark X kaongeza speed zaidi kwasababu alianza kuniacha kwa mbali kidogo.

Nikagundua hawa watu kama vile wanafanya ligi hapo road, nikaamua na mimi kujihusisha nao, ule mtiti haukuwa wa kawaida Tukaanza kutembea sasa pita nikupite ikaanza, jamaa wa Mark X tulikuwa tunamuacha sana...

Mpinzani wangu mkubwa alikuwa jamaa wa Murano, hadi tunafika Korogwe, kwenye kona yakuelekea Old Korogwe, kuna beria, tukamkuta jamaa wa Alphad pale na gari nyingine ndogo mbili, zote zinaenda Dar, ebwana eeh kama ni ligi ndio ilikuwa kama vile inaanza piga nikupige,

Jamaa walikuwa wanatoa changamoto sana, hata kusinzia huwezi muda wote unawaza kumtangulia aliyeko mbele yako na kutokukubali aliyeko nyuma yako akupite! Huu mfumo ulifanya tukafika Dar mapema sana! Huu utaratibu wa Ligi kwenye hii barabara sijui kama ni wa kila siku, Kuna mashindano sana.

Ni barabara yenye ligi tena matata sana.
Kuna MwanaJf anayependa ligi barabarani, share na sisi.
Nikusahihishe kidogo nikuwa "nyinyi mnapenda kifo siyo ligi"
 
Wakuu, nimezoea sana kutembea safari ndefu haswa Dar-Kahama-Geita na Dar-Mwanza, mara chache Dar-Bukoba.
Mara nyingi napenda kusafiri jioni au asubuhi sana.

Hizo route nilizozitaja hapo juu hazina Magari madogo mengi usiku, zaidi ya malori na mafuso. So huwa hatujui mambo ya ligi kabisa.

Kuna hii route ya Arusha-Dar na ligi huwa inaanzia pale Njia panda ya Himo, wakuu kuna watu wanapenda kushindana sana, kwenye barabara.

Juzi kati hapa tumetoka Arusha kwenda Dar tulivyofika Pale Njia Panda ya Himo, kulikuwa kuna gari kama tatu ndogo, Mark x nyeupe, Murano moja nyeusi na Alphad ya Silver, plan niliyokuwa nayo nikupoteza muda pale Njia Panda, at least usumbufu upungue barabarani kumbe zile gari zilikuwa zinatafuta abiria wa Dar, mimi kwenye gari ninayoendesha tulikuwa watatu. Sikuwa na wazo la kuchukua abiria.

Ilivyofika saa kumi na mbili kama na nusu hivi yule jamaa wa Alphad akang'oa, baada ya kama dakika kumi, Mark X akang'oa.
Hapo nimepaki upande wa pili wa barabara.

Ukapita tena muda kidogo Murano akang'oa...Tukamaliza mambo yetu tukaanza kuondoka, nilijua nikipiga mashine vizuri nitaenda kuwatoa kabla hata hawajafika Same!!
Tumeanza kutembea sio kwa speed kali hiyo jioni jioni ya saa moja bado watu ni wengi barabarani na mibasi + magari makubwa mengi yakitoka Dar kuja Moshi, Arusha.

Haikuchukua dakika nyingi saana kufika Mwanga, nikaiona ile Murano ndio inaondoka, nikajua labda alikuwa anaongezea abiria, nikawa nimempita mbele kabla ya Kisaranga nikaipita na ile Mark x, Alphad sikuiona. Giza linazidi kuongezeka naona na barabara inapungua jam.

Tumepita Lembeni kwenye Kivuko cha treni jamaa wa Mark X akaovertake kwa speed kali kuianza Tambarare flan hivi kuelekea Same, hapo ndio ikawa shughuli hakuniacha mbali sana, kabla ya sehemu inaitwa mgagao Murano akaniovertake akaenda akaovertake na mark x..

Baada ya Murano kunipita nikagundua Mark X kaongeza speed zaidi kwasababu alianza kuniacha kwa mbali kidogo.

Nikagundua hawa watu kama vile wanafanya ligi hapo road, nikaamua na mimi kujihusisha nao, ule mtiti haukuwa wa kawaida Tukaanza kutembea sasa pita nikupite ikaanza, jamaa wa Mark X tulikuwa tunamuacha sana...

Mpinzani wangu mkubwa alikuwa jamaa wa Murano, hadi tunafika Korogwe, kwenye kona yakuelekea Old Korogwe, kuna beria, tukamkuta jamaa wa Alphad pale na gari nyingine ndogo mbili, zote zinaenda Dar, ebwana eeh kama ni ligi ndio ilikuwa kama vile inaanza piga nikupige,

Jamaa walikuwa wanatoa changamoto sana, hata kusinzia huwezi muda wote unawaza kumtangulia aliyeko mbele yako na kutokukubali aliyeko nyuma yako akupite! Huu mfumo ulifanya tukafika Dar mapema sana! Huu utaratibu wa Ligi kwenye hii barabara sijui kama ni wa kila siku, Kuna mashindano sana.

Ni barabara yenye ligi tena matata sana.
Kuna MwanaJf anayependa ligi barabarani, share na sisi.
Tuhakikishie kama umeandika haya ukiwa umefika Dar .. maana haya mambo hayaendi bila mtu
 
Hebu tuandikie wino mate tuweke pembeni, Mbeya -Makambako mlitumia mda gani na hiyo private? Yaani hapo umekimbia hadi mate yamekauka mdomoni nakupa masaa mawili kwa upendeleo! Je Makambako -Dar ulitumia masaa matano?[emoji23][emoji23]
Mbeya - Makambako ni km 170 tu.... ukitembea kwa 160kph haizidi dk 80, plus matuta na vitu vingine. By the way Dar Mbeya ni km 820 tu. Ukipiga hata average ya 100kph ni masaa 8. Ukiachana na Kitonga + Iyovi, maeneo mengine yote kama usiku unapiga 140-160 bila shida.
 
Mbeya - Makambako ni km 170 tu.... ukitembea kwa 160kph haizidi dk 80, plus matuta na vitu vingine. By the way Dar Mbeya ni km 820 tu. Ukipiga hata average ya 100kph ni masaa 8. Ukiachana na Kitonga + Iyovi, maeneo mengine yote kama usiku unapiga 140-160 bila shida.
Sijakuelewa mkuu..una km 170 alaf ukitembea kwa speed ya 160kph itatumika muda gani?
 
Mbeya - Makambako ni km 170 tu.... ukitembea kwa 160kph haizidi dk 80, plus matuta na vitu vingine. By the way Dar Mbeya ni km 820 tu. Ukipiga hata average ya 100kph ni masaa 8. Ukiachana na Kitonga + Iyovi, maeneo mengine yote kama usiku unapiga 140-160 bila shida.
Iyovi ni kona kona flani hivi zinazokera
 
Ligi nyingine iko Dodoma - Dar kila ijumaa kuanzia saa kumi na mbili jioni.. au siku bunge linavunjwa... ni hatariiii
From Singida to Dar, nilikuwa siendeshi mimi.
nilivyofika Dodoma, nikapokea usukan ndani ya Aud A6 3.2...this sedan car was fantastic tuliziacha V8 na Nissan patrol kadhaa. Ligi ya Dodoma to Dar ni za kuotea otea...
 
Back
Top Bottom