Hii tabia ya kudharau simu za Tecno itakwisha lini?

Hii tabia ya kudharau simu za Tecno itakwisha lini?

Wewe ndie mshamba sijawahi kuona.

Wewe ndio unaambia watu watafte exposure wakati wewe huna? Vivo nex uilinganishe na s10+? Una akili timamu kweli? Hizo ranking umezitoa wapi?.

Simu hazilinganishwi umekaa kwenu mbagala maji matitu huko na vivo nex yako ukasema hii simu ni nzuri kuliko simu zote Duniani...

Jamaa kaongea kwa mihemko na jazba nikaona hata tukisema tueleweshane hatakua tayari...

Halafu hawa ndugu zetu sijui kwa nini, Wengi wao wanakua na hasira na panic kweli,
Sasa unafura watu kusifia tuu samsung na iphone? ndio maana simu zao wengi zimepasuka vioo kimbe ni kugombana na keyboard...

Nokia Sirroco Simu ya 2018 unaleta kwenye battle na flagship za 2020 seriously?

Hizo simu nyingine alizotaja ni kweli ni simu nzuri, Lakini bado zina mambo mengi zimepigwa na Samsung, kwingine wametoka flat.

Hatubishi, Kampuni mpya za simu kwa sasa zinawakimbiza sana iphone na samsung(huawei tumuweke pembeni kesi yake ni tofauti)
Ila bado wanahitaji mda kuwashusha hawa ma Giants(akiwemo huawei) Pale juu,

Yeye anadai bei na soko ndio maana hazifiki huku. Hii kwa kweli hapana, simu zote alizotaja zimesambaa, ila wamiliki ni wachache kwa sababu tofauti ikiwemo zenyewe kutojitangaza vizuri na kushindwa local market competition na kampuni nyingine,

Sijui kwa nini watu hua wanadanganyana, Unasikia mtu anakuambia kuna simu bora sana duniani ambazo haziji huku kwetu eti sababu ya uchumi n.k n.k?

Sijui hii dhana wanatoa wapi? Ndio zipo kampuni ambazo simu zao hazifiki huku, ila ni kwa sababu nyingine ila sio Ubora na Bei.

Kampuni bora za simu dunianni zinajulikana, Simu bora kutoka kampuni hizo zinajulikana,
Vyote hivi sio kwa ramli ni kwa takwimu/data na historia.

Sasa hio ambayo haiji huku na ni bora ni ipi? Hili funga kamba wengine ila sio wote..
BIG phone BIG Market...

Tetea upande wako, ila tumia tuu fact haina haja ya kugombana na masufuria huko uliko...

Yeye angetumia tuu dhana yake ya kua hawezi kutumia brand ya simu ambayo watu wengi wanatumia kwa anavyodai(samsung na iphone).....

Hayo ni maamuzi na mawazo yake hakuna atakaye mlazimisha, japo ukihoji unaona kabisa kuna ukakasi, Samsung na Iphones zimezagaa kiasi hicho? oky kama zimezagaa je ni Matoleo yote? wangapi wanatumia flagship za samsung na iphones bongo hii?
Jibu analo.

Mwisho unakuja kuona Point yake ni kutumia brand ya simu adimu na sio bora zaidi ya iphone na samsung.

Hatupaswi kumponda mtumiaji wa simu flani, Sababu ya mtazamo wako, hata kama pia una fact kama kampuni hio si bora kulinganisha na hio nyingine, Mpe fact mwache na Maisha/Maamuzi yake.
 
Tecno ubora wake n kwenye Battery capacity na Camera kwakwel najivunia Xm yngu camera yke n kam 2 ya samsung galaxy s8 na hapo bado inaizid kwa battery capacity.
 
I phone ukinunulia tanzania nyingi ni feki labda uwe umenunua nje ya nchi dubai na ulaya. Au asia sio china
 
Biashara matangazo

Kuna watu wanajua kuna ligi moja tu ya mpira yaani La liga kisa kuna lionel Mesi

Ukiwaambia pia uingereza kuna ligi ya EPL hawaelewi na wanakucheka kwani la liga kwao ndio bora

Hivyo wewe samsung na i phone ni mazingira uliyonayo yanakutesa sana ndio simu unazopata

Hata maduka makubwa Dar nasikia ni Tecno,iphone na samsung
 
I phone ukinunulia tanzania nyingi ni feki labda uwe umenunua nje ya nchi dubai na ulaya. Au asia sio china
Ni kweli kabisa mkuu,hata haya magar(Toyota,nissan,benz etc) tunayonunulia hapa hapa hapa bongo yanakuaga ni 'feki' sana labda kwa watu wanaoununulia magari Japan,US,Dubai,Germany ndio yanakuaga Original.
 
Jamaa kaongea kwa mihemko na jazba nikaona hata tukisema tueleweshane hatakua tayari...

Halafu hawa ndugu zetu sijui kwa nini, Wengi wao wanakua na hasira na panic kweli,
Sasa unafura watu kusifia tuu samsung na iphone? ndio maana simu zao wengi zimepasuka vioo kimbe ni kugombana na keyboard...

Unanunua simu kubwa ambayo kioo kikiharibika unaanza kuhangaika. Bora ununue simu inayoendana na budget na matumizi yako
 
Unanunua simu kubwa ambayo kioo kikiharibika unaanza kuhangaika. Bora ununue simu inayoendana na budget na matumizi yako
Hapa sasa mkuu Umetoka nje ya mada..
Maana hata tecno leo hii anasimu zinakalibia 600k..
Na samusung ana simu kuanzia 150k..
Mada inahusu brand.
 
Acheni dharau wakubwa mwenye tecno huo ndio uwezo wake wote tumeona hapa kipindi cha corona imedhiirika wazi kuwa 80% ya wabongo choka mbaya hata barakoa kununua ishu sasa unamfosi vipi mtu anaepiga kibarua cha kuunga unga mshahara laki mbilj anunue Galaxy S8 mnataka watu wawe wezi au watoe tako ama point yenu nini?

Unawaponda wenzio kisa wana tecno hauna tofauti na Chris Mauki aliyesema wanaume wanaorudi bila kitu wasanii..

Maisha kupata na kukosa kama wewe unaweza kununua I phone, Samsung, sema asante Mungu acha kudharau wenzio...
 
Smart phone 3 bora Dunia
1)iPhone
2) sumsung
3)Sony experia
NA hapo Sony na sumsung wanashinda
wangombania namba mbili

Smart phone za hovyo 3 Dunia
1)Tecno
2)Huawei
3)iflix
Mimi sijawai kutumia simu ya smart ya kichina toka simu za kawaida kipindi hiko nilikuwa natumia Nokia sumsung blackberry hizo ndio simu zangu na Sasa natumia Sony kwa matumizi ya kawaida kwa sababu inabebeka na iPad tablet ni ya nyumbani
mkuu sio kwel Huawei yuko vizuri sana na ana simu nzuri zaid ya izo iPhones na samsung.
kuna
IMG_20200527_083057.jpg
 
Back
Top Bottom