Hii sentensi ipo sahihi au huwa tunakosea??

Katavi

Platinum Member
Aug 31, 2009
41,983
12,702
Hivi tunaposema kwa mfano:

Nimekula WALI KWA KUKU au WALI NA KUKU, huwa tupo sahihi???

Wataalamu wa lugha tafadhali...
 
Hivi tunaposema kwa mfano:

Nimekula WALI KWA KUKU au WALI NA KUKU, huwa tupo sahihi???

Wataalamu wa lugha tafadhali...
Mkuu.
Zote hizo mbili ni sahihi.

ya pili ni orodha.
ya kwanza ni masimulizi.

...halafu si unaelewa kuwa huwa ni sinia au sahani bonge na kipaja kimoja cha kuku?
Yaani wali pomoni, tele lakini mchuzi au mboga ni kijinofu kadogo!!! Mitaani kwetu...pengine wengi wangesema " uswahilini".
 
Mkuu.
Zote hizo mbili ni sahihi.

ya pili ni orodha.
ya kwanza ni masimulizi.

...halafu si unaelewa kuwa huwa ni sinia au sahani bonge na kipaja kimoja cha kuku?
Yaani wali pomoni, tele lakini mchuzi au mboga ni kijinofu kadogo!!! Mitaani kwetu...pengine wengi wangesema " uswahilini".

Nimependa maelezo yako. Good!
 
Na tukisema: Wali kuku!
Pia ni sawa.
Inategea wapi tu utatumia hiyo.
Mazingira ya matumizi ya lugha, register kwa kimombo.
Ukiitumia mkahawani na kusema nipatie wali kuku au chips kuku basi ndio lugha ya mkahawani hiyo, lugha ya mtaani

Lakini ukija katika uandishi wa hadithi au makala ya gazeti ukitumia hiyo bila ya kuwa direct quote utakuwa kimatumizi ya lugha ina walakini kidogo ,ingawaje msomaji ataelewa unakusudia nini.
 
Hivi tunaposema kwa mfano:

Nimekula WALI KWA KUKU au WALI NA KUKU, huwa tupo sahihi???

Wataalamu wa lugha tafadhali...

Kwa mtazamo wangu, zote zinaweza kuwa sahihi au sio sahihi kwa kutegemea unataka kusema nini hasa (kufikisha ujumbe gani) lakini kilicho dhahiri ni kuwa hizo sentesi mbili hazina maana iliyo sawa!

Nimekula 'WALI NA KUKU': (ni kama unasisitiza zaidi aina ya vyakula ulivyokula) ingawa kwa usahihi zaidi ungepaswa kusema umekula 'wali na nyama ya kuku' (labda kama unakula kuku kama afanyavyo nyegere!). Kama kuna mtu jina lake ni Kuku (au hata kama unataka kumpa kuku ndege ubinaadamu kwa sababu maalumu), sentensi hiyo inaweza kuashiria pia wewe pamoja na huyo kuku mmekula wali mkiwa pamoja.

Nimekula WALI KWA KUKU: Kama kuna mtu jina lake ni Kuku, sentensi hiyo inaweza kuashiria pengine ulienda nyumbani kwa huyo Kuku na ukala wali. Lakini kwa matumizi ya kawaida, sote tunajua nyama ya kuku (kuku) hutumika kama kitoweo na kwa ajili ya kuliwa kwa pamoja na chakula kingine (wali, ugali etc). Katika muktadha huu neno kuku naona linabeba dhana ya kitendeo kwa maana kuwa ungewea kula wali wako kwa kutumia (pamoja na..) maharage, nyama, mlenda nk.
 
Kwa mtazamo wangu, zote zinaweza kuwa sahihi au sio sahihi kwa kutegemea unataka kusema nini hasa (kufikisha ujumbe gani) lakini kilicho dhahili ni kuwa hizo sentesi mbili hazina maana iliyo sawa!

Nimekula 'WALI NA KUKU': (ni kama unasisitiza zaidi aina ya vyakula ulivyokula) ingawa kwa usahihi zaidi ungepaswa kusema umekula 'wali na nyama ya kuku' (labda kama unakula kuku kama afanyavyo nyegere!). Kama kuna mtu jina lake ni Kuku (au hata kama unataka kumpa kuku ndege ubinaadamu kwa sababu maalumu), sentensi hiyo inaweza kuashiria pia wewe pamoja na huyo kuku mmekula wali mkiwa pamoja.

Nimekula WALI KWA KUKU: Kama kuna mtu jina lake ni Kuku, sentensi hiyo inaweza kuashiria pengine ulienda nyumbani kwa huyo Kuku na ukala wali. Lakini kwa matumizi ya kawaida, sote tunajua nyama ya kuku (kuku) hutumika kama kitoweo na kwa ajili ya kuliwa kwa pamoja na chakula kingine (wali, ugali etc). Katika muktadha huu neno kuku naona linabeba dhana ya kitendeo kwa maana kuwa ungewea kula wali wako kwa kutumia (pamoja na..) maharage, nyama, mlenda nk.

Mkuu
Uchambuzi wako umenichekesha sana...wacha utani bwana....inafaa sana hii katika utani.
Na hiyo red Search Results for 'dhahiri' | Matokeo ya Utafutaji kwa 'dhahiri' | The Kamusi Project
 
Kwa mtazamo wangu, zote zinaweza kuwa sahihi au sio sahihi kwa kutegemea unataka kusema nini hasa (kufikisha ujumbe gani) lakini kilicho dhahiri ni kuwa hizo sentesi mbili hazina maana iliyo sawa!

Nimekula 'WALI NA KUKU': (ni kama unasisitiza zaidi aina ya vyakula ulivyokula) ingawa kwa usahihi zaidi ungepaswa kusema umekula 'wali na nyama ya kuku' (labda kama unakula kuku kama afanyavyo nyegere!). Kama kuna mtu jina lake ni Kuku (au hata kama unataka kumpa kuku ndege ubinaadamu kwa sababu maalumu), sentensi hiyo inaweza kuashiria pia wewe pamoja na huyo kuku mmekula wali mkiwa pamoja.

Nimekula WALI KWA KUKU: Kama kuna mtu jina lake ni Kuku, sentensi hiyo inaweza kuashiria pengine ulienda nyumbani kwa huyo Kuku na ukala wali. Lakini kwa matumizi ya kawaida, sote tunajua nyama ya kuku (kuku) hutumika kama kitoweo na kwa ajili ya kuliwa kwa pamoja na chakula kingine (wali, ugali etc). Katika muktadha huu neno kuku naona linabeba dhana ya kitendeo kwa maana kuwa ungewea kula wali wako kwa kutumia (pamoja na..) maharage, nyama, mlenda nk.
Ni kweli kabisa zote mbili zinaweza kuwa sahih, lakini katika mantiki ya kitendo cha kula, wakati tunaelewa kuwa kilichokusudiwa ni chakula gani na mboga/kitoweo gani vilivyoliwa na mlaji, inapendeza zaidi kutumia "na" ambayo ina maana moja tu "and" kuliko "kwa" ambayo ina maana nyingi "with, by, to...." hali ambayo inaweza kuleta utata.
Angalia:
1. Juma amepigwa na Maria = Maria amempiga Juma au hata Juma na Maria wamepigwa.
2. Juma amepigwa kwa Maria= Kwao Maria au kwa ajili ya Maria.
 
zote zina mapungufu hasa tukizingatia kwamba KUKU ni kiumbe, sasa huwezi sema
WALI NA KUKU, kwa kuwa wali ni chakula kilichopikwa tayari ambacho kimetokana na Mchele
kwa nini? kwa sababu Mchele ukishapikwa hauitwi tena mchele bali huitwa WALI,

usahihi wa sentensi ni WALI NA NYAMA YA KUKU
kwa sababu mnyama, ndege, n.k akishachinjwa jina hubadirika hawi KUKU, MBUZI, NG'OMBE n.k
bali nyama ya KUKU, MBUZI, n.k
 
Kwa mtazamo wangu, wali na kuku ni sahihi, ila wali kwa kuku au wali wa kuku hua inachanganya kidogo.
 
Mkuu zinaweza kuwa sahii nakubaliana na wewe, mfano mtu akisema Wali kuku hii inakubalika?

Mkuu.
Zote hizo mbili ni sahihi.

ya pili ni orodha.
ya kwanza ni masimulizi.

...halafu si unaelewa kuwa huwa ni sinia au sahani bonge na kipaja kimoja cha kuku?
Yaani wali pomoni, tele lakini mchuzi au mboga ni kijinofu kadogo!!! Mitaani kwetu...pengine wengi wangesema " uswahilini".
 
Back
Top Bottom