Hii Ndiyo Ilikuwa Msaada na VPN Haikuwa Msaada?

Hii Ndiyo Ilikuwa Msaada na VPN Haikuwa Msaada?

Kuna mandezi wengi sana mtandaoni, nahisi wengi humu ni vijana zetu wadogo sana.

Hawa ni wale ambao akipata kitu kipya na kigeni lazima awaonyeshe wenzake.

Karibu kila mtu alikuwa akipost aina ya VPN anayotumia, hapo nikaanza kujiandaa ikiwa wajomba wa switch wakizima itakuwaje, maana watazuia engo zote.

Sasa bana, siku moja kabla ya uchaguzi nilisearch web gani naweza kutumia ikiwa mtandao umefungwa nikapata moja hivi ambayo kwa uzembe usiku nikasahau kuidownload.

Na mimi nikapigwa lokoo ndiyo hadi leo.

Nilichojifunza ni kuwa watanzania pamoja na uoga tulio nao hatuwezi kukaa kimya kwa jambo ambalo linaweza kuwa faida kwa wakati ujao.
Unajua kitu kinaitwa mkongo wa taifa?

Sasa mkongo wa taifa ukizimwa na TTCL wewe mwenye internet ya Voda au Airtel unapataje internet hata kama una VPN?

Ili uweze kuwa na internet hapo ni ama utumie ya satellite kama StarLink ambayo Nape aliikataa akiwa Waziri, au uwe mpakani sana utumie mitandao jirani, au utumie network ya taasisi za serikali ambayo mara nyingi ethernet huwa haiunganishwi na apps unatumia kwenye servers za serikali tu na kwenye kifaa kilichounganishwa na waya tu.

VPN kazi yake sio kuzuia internet iliyofungwa. Ni kupeleka data traffic zako kwenye uzio na kuficha IP address yako, ila bado unatumia tu internet.
 
Back
Top Bottom