Hii ndiyo CV ya Idd Azzan


Sio 1966 tu hata waliosoma miaka 1990s pia fursa ilikuwepo wabunge wa design hii wanasoma kwa sababu hata ukiangalia CV yake utaona amemaliza primary school 1979 lakini ajabu secondari amekumbuka kujiendeleza miaka ya 2000, hii inainyesha moja kwa moja kuna kitu alikuwa anatafuta nacho si kingine ni uongozi. Kama mtu alikosa fursa ya kwenda sekondari kulikuwa na fursa nyingine ya kusoma masomo ya jioni.
 
Mkuu tunaomba pia cv za wabunge wa chadema tulinganishe na hii.Ingekuwa ni vizuri mno
 
Hapo kwenye wakuu wa wilaya ndugu MchunguZI ndio inaniuma maana wanateuliwa watu ambao hata experience ya uongozi hawana, maana kazi ya mkuu wa wilaya ni kusimamia utekelezaji wa halmashauri alafu unamtoa mtu from nowhere tena msela with zero experience of local government kwenda kushika u-DC hapa unategemea nini hapa kama sio kufanya kampeni za chama tawala na vitu vingine vya kichama. Hizi poat zinatakiwa mtu ambae amekuwa katika utumishi wa umma kwa muda mrefu ili iwe rahisi kutekeleza shughuli na ndio maana unakuta DC anaingia vijijini na kuwafukuza kazi watendaji wa kata na vijiji/mitaa wakati hiyo si kazi yake (sema nchi hii ndio hivyo wananchi wake wengi ni kubali yaishe otherwise siku wananchi watakapojitambua nadhani watu wakigombea ubunge kipindi kimoja hawatachukua fomu kipindi kingine)
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tunaomba pia cv za wabunge wa chadema tulinganishe na hii.Ingekuwa ni vizuri mno

Inaelekea CDM mnaigopa maana alietoa hii thread hajajitambulisha kama CDM, kwanini zikija thread zinazoonyesha mambo tata ya CCM huwa mnakimbilia CDM kufanya comparison, why not other party?
 
hilo nalo neno ndo maana wanaishia kuomba rushwa.mie naomba kiingereza kipitishwe wawe wanaongea bungeni wengine kila siku watakuwa wagonjwa.

Hata kisipopitishwa kiingereza bado tatizo lipo pale pale hata kama ni kwa kiswahili kama mtu hana nondo za kutosha kuhusu mada flani hata umpe fursa ya kuuzungumza kisukuma bado hawezi kwa kuwa maarifa ya agenda husika na madogo. Ni kama tulivyokuwa primary school tunafundishwa kwa kiswahili lakini bado vilaza walikuwepo, elimu ni ufunguo wa maisha hata kama amesoma kijapani, kichina etc
 
DAR ES SALAAM ndo tulitegemea ingekuwa kitovu cha mabadiliko ktk hii nyanja ya democrasia lkn matokeo yake hovyo kabsa watu mna chuo kikuu cha kwanza TZ lkn ni wavivu wa kufikiri wanabaki kuwasufia wabunge wa upinzani kutoka vijijini jaman badilikeni wana daresalaama
 
Wapendwa huyo ndugu cv yake ni nzuri ukilinganisha na wabunge wengine wa ccm kama akina Lusinde wa mtera, au ngonyani wa korogwe na wengine kwa kweli ni shida kubwa. tatizo lingine linaloletelea haya yote ni kwamba mkwanja unatumika sana kwenye chaguzi zetu na kufanya wenye fedha kuingia kwa wingi kwenye chombo hiki nyeti cha maamuzi ya nchi yetu.
 
Leo hii nimehitimu mafunzo yangu ya shahada ya kwanza hakika nina nafasi ya kuwa mkurugenzi ikiwa hawa watu wasiokuwa na sifa wataondolewa wote. taifa linaloamini katika giza linafanya vitu kigizagiza pia.
 

Mkuu nilikuwa na mpango wa kuanzisha kombe la Mbuzi naona sasa nianzishe tu kombe la Kimbunga kutangaza jina ili 2015 nami nijikumbushe siasa.

Mkuu juzi juzi Kenya walijaribu kubadili sifa hasa za kielimu ili wabunge wawe wenye degree lakini kulikuwa na upinzani sijui uliishaje. Unapokuwa na watunga sheria wengi ambao wana sifa za chini usitegemee mabadiliko ya kuwaengua yapate njia nyepesi.
 

Ni kweli Kimbunga maana kuna mijadala kiukweli hata ukiwa umeenda shule bado inahitaji uwe mahiri katika maeneo flani sembuse mtu ambae shuleless. Kuna siku mbunge wa Mbozi (Godfrey Zambi) alikuwa anachangia akasema tatizo mambo mengi yanaandikwa kwa kiingereza lakini tunayajadili kwa kiswahili sijui lini yataandikwa kwa kiswahili, akatoa hoja yake kulikuwa kuna maneno hayaeleweki vizuri, waziri katika kujibu si akawa na kigugumizi kujibu na kusema pamekosewa,ndipo nilipogundua wakti wengine wabunge wanapitisha hoja bila kupingwa bila kuangalia kiundani
 
Last edited by a moderator:
Nch nchi hii haitapata kuendelea kama vilaza wanakaa mbele na wenye akili na ujuzi wanawekwa nyuma yao. Uzoefu wa miaka 50 hamsini umeonesha ni namna gani usawa wa binadamu hauwezi kuendekezwa katika kuendeleza nchi hii. Ni lazima tutoe nafasi wataalamu washike hatamu na watu wenye upeo wa kutosha kufanya maamuzi. Sasa nimeelewa ni kwanini ccm inafanya vituko. Tafsiri mbovu sana ya usawa wa binadamu. Livingstone, jah people, azzan na wengine hawana ubavu wa kupeleka mbele gurudumu la maendeleo ya nchi hii. Kuongoza sio kupiga kelele kuliko wengine au kuhimili kadamnasi . Ccm think twice, we are loosing at the expense of your bogus politics
 
Kilaza mwingine yuko mrogoro mjini. Vyuo vikuu viwili sua na muslim. Lakini abood kamtoa baruti prof wa sua. Sera mbovu za ccm hizi. Hawa umande wamaukimbia lakini wananga'ang'ania nafasi kubwa sijui tuwaeleweje?
 
Tatizo hata mwanamke wake ambae ni mbunge wa chadema grace kiwelu hajaenda shule pia unategemea kuna kushauriana kuhusu kuongeza elimu kweli hapo????​


naomba cv
 
Watu kama hawa wakiwa bungeni watachangia kama ifuatavyo:
Asante sana mh. spika, kabla ya yote napenda kutoa shukurani zangu za dhati kabisa kwa Mh.W/M, mtukufu Rahisi, wabunge wote wa chama changu, Mwisho shukurani ziende kwa mke wangu, watoto wangu wa kike na wa kiume mmoja anaitwa Mh. Jingine yuke pale Juu hapa katika ukumbi wa Bunge

Baada ya kusema hayo hoja ya waziri ina mapungufu 1,2,3,3..... naunga mkono Hoja 100%.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…