Hii ndio picha halisi ya Yesu

Hii ndio picha halisi ya Yesu

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
8,988
Reaction score
11,862
Watu wengi hutamani kumuona Yesu. Wanajiuliza, “Alikuwa na sura gani? Alionekana vipi? Alikuwa mtu wa namna gani?” Wengine hujaribu kutengeneza picha kwa mawazo, ndoto au sanaa. Lakini kuna njia moja ya uhakika ya kumuona Yesu kwa macho ya kweli ya rohoni kupitia Neno lake.

Ni kama vile unavyosoma riwaya nzuri: kadri unavyosoma, unamjengea mhusika sura kichwani mwako. Unaweza kumjua tabia yake, namna anavyotembea, anavyocheka, anavyopenda au kuchukia yote haya yanajitokeza kupitia maneno.

Hali ni hiyo hiyo kwa Yesu.

Ukisoma Biblia kwa moyo wa kujifunza na kuelewa, utamwona Yesu ndani ya kila ukurasa. Si kwa macho ya nyama, bali kwa macho ya roho. Utaanza kuona:

1. Yesu mwenye huruma kwa walioteseka

2. Yesu mwenye msamaha kwa waliomkosea

3. Yesu mwenye nguvu dhidi ya dhambi na kifo

4. Yesu mwaminifu, mpole, na mwenye mamlaka

Na mwisho wa yote, picha hiyo itaanza kuchorwa pia ndani ya moyo wako.

Yesu si simulizi tu, ni Neno hai. Ukisoma Biblia, si tu unamjua bali unamwona, unamgusa kwa imani, na maisha yako hubadilika milele.

“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu...” (Yohana 1:14)

Leo, chukua muda wako. Fungua Biblia. Mkaribishe Roho Mtakatifu. Na utamwona Yesu sura yake, tabia yake, na upendo wake.

Picha ya Yesu haijachorwa kwa mikono ya binadamu, bali ndani ya Neno la Mungu.
 
Watu wengi hutamani kumuona Yesu. Wanajiuliza, “Alikuwa na sura gani? Alionekana vipi? Alikuwa mtu wa namna gani?” Wengine hujaribu kutengeneza picha kwa mawazo, ndoto au sanaa. Lakini kuna njia moja ya uhakika ya kumuona Yesu kwa macho ya kweli ya rohoni kupitia Neno lake.

Ni kama vile unavyosoma riwaya nzuri: kadri unavyosoma, unamjengea mhusika sura kichwani mwako. Unaweza kumjua tabia yake, namna anavyotembea, anavyocheka, anavyopenda au kuchukia yote haya yanajitokeza kupitia maneno.

Hali ni hiyo hiyo kwa Yesu.

Ukisoma Biblia kwa moyo wa kujifunza na kuelewa, utamwona Yesu ndani ya kila ukurasa. Si kwa macho ya nyama, bali kwa macho ya roho. Utaanza kuona:

1. Yesu mwenye huruma kwa walioteseka

2. Yesu mwenye msamaha kwa waliomkosea

3. Yesu mwenye nguvu dhidi ya dhambi na kifo

4. Yesu mwaminifu, mpole, na mwenye mamlaka

Na mwisho wa yote, picha hiyo itaanza kuchorwa pia ndani ya moyo wako.

Yesu si simulizi tu, ni Neno hai. Ukisoma Biblia, si tu unamjua bali unamwona, unamgusa kwa imani, na maisha yako hubadilika milele.

“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu...” (Yohana 1:14)

Leo, chukua muda wako. Fungua Biblia. Mkaribishe Roho Mtakatifu. Na utamwona Yesu sura yake, tabia yake, na upendo wake.

Picha ya Yesu haijachorwa kwa mikono ya binadamu, bali ndani ya Neno la Mungu.
Weka picha yake
 
"ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba";

Huyo ndiye Yesu!
 
Setfree nakualika humu thibitisha hili
Meneja Wa Makampuni amefanya kazi nzuri sana ya kukusaidia uichore wewe mwenyewe picha ya Yesu ndani ya moyo wako kwa kutafakari hizo points.

Ni kweli, Yesu hakuwa na sura nzuri. Picha tunazoziona leo zikidaiwa ni za Yesu, zimebuniwa tu.
Haya ni maelezo ya Biblia ya jinsi sura ya Yesu ilivyokuwa:
Isaya 53:2
"...Hakuwa na umbo wala sura ya kutupendeza, wala hakuwa na uzuri wowote wa kutuvutia. Alidharauliwa na kukataliwa na watu, alikuwa mtu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mtu kinyaa kwa watu; alidharauliwa na tukamwona si kitu. Lakini alijeruhiwa kwa sababu ya dhambi zetu, aliumizwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuadhibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

cc: Kelvin35
 
Meneja Wa Makampuni amefanya kazi nzuri sana ya kukusaidia uichore wewe mwenyewe picha ya Yesu ndani ya moyo wako kwa kutafakari hizo points.

Ni kweli, Yesu hakuwa na sura nzuri. Picha tunazoziona leo zikidaiwa ni za Yesu, zimebuniwa tu.
Haya ni maelezo ya Biblia ya jinsi sura ya Yesu ilivyokuwa:
Isaya 53:2
"...Hakuwa na umbo wala sura ya kutupendeza, wala hakuwa na uzuri wowote wa kutuvutia. Alidharauliwa na kukataliwa na watu, alikuwa mtu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mtu kinyaa kwa watu; alidharauliwa na tukamwona si kitu. Lakini alijeruhiwa kwa sababu ya dhambi zetu, aliumizwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuadhibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
AMINA
 
Watu wengi hutamani kumuona Yesu. Wanajiuliza, “Alikuwa na sura gani? Alionekana vipi? Alikuwa mtu wa namna gani?” Wengine hujaribu kutengeneza picha kwa mawazo, ndoto au sanaa. Lakini kuna njia moja ya uhakika ya kumuona Yesu kwa macho ya kweli ya rohoni kupitia Neno lake.

Ni kama vile unavyosoma riwaya nzuri: kadri unavyosoma, unamjengea mhusika sura kichwani mwako. Unaweza kumjua tabia yake, namna anavyotembea, anavyocheka, anavyopenda au kuchukia yote haya yanajitokeza kupitia maneno.

Hali ni hiyo hiyo kwa Yesu.

Ukisoma Biblia kwa moyo wa kujifunza na kuelewa, utamwona Yesu ndani ya kila ukurasa. Si kwa macho ya nyama, bali kwa macho ya roho. Utaanza kuona:

1. Yesu mwenye huruma kwa walioteseka

2. Yesu mwenye msamaha kwa waliomkosea

3. Yesu mwenye nguvu dhidi ya dhambi na kifo

4. Yesu mwaminifu, mpole, na mwenye mamlaka

Na mwisho wa yote, picha hiyo itaanza kuchorwa pia ndani ya moyo wako.

Yesu si simulizi tu, ni Neno hai. Ukisoma Biblia, si tu unamjua bali unamwona, unamgusa kwa imani, na maisha yako hubadilika milele.

“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu...” (Yohana 1:14)

Leo, chukua muda wako. Fungua Biblia. Mkaribishe Roho Mtakatifu. Na utamwona Yesu sura yake, tabia yake, na upendo wake.

Picha ya Yesu haijachorwa kwa mikono ya binadamu, bali ndani ya Neno la Mungu.

🙏
 
Miaka 12 yumo hekaluni akiwafafanulia waandishi, makuhani, wazee, na wenye hekima habari za Mungu (in fact zake). Na elimu zao walipigwa KO. Huyo ndiye YESU waliyemdhania ni mwana wa seremala. Maskini, hawakujua hata mimba yake haikuwa kwa ngono! Hawakujua mwanamwali bikira alibeba mimba!
 
Meneja Wa Makampuni amefanya kazi nzuri sana ya kukusaidia uichore wewe mwenyewe picha ya Yesu ndani ya moyo wako kwa kutafakari hizo points.

Ni kweli, Yesu hakuwa na sura nzuri. Picha tunazoziona leo zikidaiwa ni za Yesu, zimebuniwa tu.
Haya ni maelezo ya Biblia ya jinsi sura ya Yesu ilivyokuwa:
Isaya 53:2
"...Hakuwa na umbo wala sura ya kutupendeza, wala hakuwa na uzuri wowote wa kutuvutia. Alidharauliwa na kukataliwa na watu, alikuwa mtu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mtu kinyaa kwa watu; alidharauliwa na tukamwona si kitu. Lakini alijeruhiwa kwa sababu ya dhambi zetu, aliumizwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuadhibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

cc: Kelvin35
Mungu awatie nguvu katika kuieneza injili. Mada zenu hazitokuwa na komenti nyingi, lakini katika uchache wake,atakuwemo atakayemwamini YESU. Samson Ernest
 
Back
Top Bottom