Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,865
- 12,297
Habari zenu wanaJF wenzangu,
Wakuu.... wengi wetu hapa JF na nchini kwa ujumla, tunajua kwamba raisi wa JMT mh Samia S. Hassan anapambana usiku na mchana, ili kuhakikisha serikali yake inaleta maendeleo katika wilaya, mikoa na nchi yote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Lakini kama ilivyo desturi ya sisi binadamu unapokuwa na mambo, vitu au watu zaidi ya watatu ubavuni kwako, ni wazi kuwa hautoweza kubalance upendo wako kwao yani iwe mia kwa mia kwa kila mtu au kitu. Ni lazima mtu au kitu kimoja utakipenda zaidi ya kiingine.
Hili hutokea hata kwa mzazi mwenye watoto mfano wa5 hujikuta anampenda mtoto mmoja au wawili zaidi ya awapendavyo waliobaki, japo kama mzazi huwa haoneshi moja kwa moja upendeleo wake huo kutokana na kutaka wale wengine wasijisikie kubaguliwa nk.
Hivyo basi hata raisi wetu, ni raisi wa nchi nzima, lkn ukweli ni kwamba kuna baadhi ya mikoa ambayo amekuwa akionesha kuipenda na kuijali zaidi ya mikoa mingine, na hili limekuwa likionekana kupitia miradi mbali mbali kabambe aliyoielekeza katika mikoa hiyo hata kama anajaribu kutokuonesha kuwa ana baze zaidi huko, lkn wafuatiliaji tunaona wenyewe kwa macho yetu na kusikia pia kwa masikio yetu.
Mikoa hiyo ambayo inabahati mno na serikali hii ni 👇
1. Dodoma.
Mkoa huu pamoja na kwamba raisi aliekuwepo madarakani hayati John P. Magufuli aliupenda na kuelekeza zaidi macho yake huko, pia umeendelea kuneemeka na uongozi huu wa awamu ya 6 chini ya raisi Samia na kupelekea miradi mingi ya maendeleo kupelekwa huko.
Nafikiri haya yamesababishwa na hadhi yake kama mji wa serikali na makao makuu ya nchi.
2. Kigoma.
Mkoa wa Kigoma pia unazali na uongozi huu wa raisi Samia. Japo mkoa huu una kiongozi mmoja mkubwa wa chama cha upinzani, na historia yake ya baadhi ya vijana kushikiwa akili na kupenda kuunga mkono wapinzani mbali mbali, lkn raisi Samia hakujali hayo.
Ameelekeza nguvu na miradi katika mkoa huo kuliko kiongozi mungine yoyote aliewahi kutawala kabla yake. I hope hiyo miradi ikikamilika basi Kigoma itakuwa Small "Chicago", achilia mbali zile stori za mh Kikwete kwamba angeigeuza Kigoma kuwa Dubai kwa maneno tu matupu bila vitendo wala kutoa hela za miradi husika.
3. Mbeya.
Huu mkoa nao ni miongoni mwa mikoa inayofaidika kwa kasi kupitia uongozi huu wa awamu ya tano. Kabla ya hapo mkoa huo ni kama vile ulikuwa umesahaulika kimtindo, maana hata miundo mbinu ya mkoa huo kwa upande wa barabara, shule, hospital nk vilikuwa hovyo, ila toka raisi Samia aingie amekuwa akionesha kushirikiana na mbunge Mbeya mjini ambae pia ni spika wa bunge kuleta maendeleo ya kweli katika mkoa huo.
Kwa kuonesha kuwa anaupenda mkoa huo kwa vitendo, serikali ya raisi Samia tayari imeshatoa mamilioni ya miradi kwa ajili ya shule, barabara nk. Japo kuna baadhi ya watumishi wa serikali kutoka mkoa huo wanaonekana kutohitaji maendeleo katika mkoa huo kwa kutafuna mamilioni ya baadhi ya miradi kama alivyosema raisi Samia alipokuwa ziarani mkoani huko, lkn ni kama vile bado hajachoka kuendeleza miradi katika mkoa huo, bila kujali baadhi ya wapinzani ambao wao wanachotaka ni kuingia bungeni tu bila kujali maendeleo anayowaletea raisi Samia katika mkoa wao.
Baadhi ya wanasiasa wenye familia zao Ulaya na Marekani ambao kiasili hawatoki katika mkoa huo, wamekuwa wakiwahadaa vijana ambao wengi wao walikimbia shule mkoani hapo, wapinge miradi hiyo ya maendeleo ili uchaguzi mkuu utapofika wachaguliwe wao tu na vyama vyao.
4. Mwanza.
Mkoa wa Mwanza pia ni kama Dodoma. Ulikuwa na zali chini ya serikali ya awamu ya 5 ya hayati Magufuli, na bado umeendelea kuwa na bahati pia chini ya serikali hii ya awamu ya 6 ya raisi Samia.
5. Mtwara....
6. Lindi....
Kama kuna mikoa mingine ambayo imeneemeka na uongozi wa raisi Samia alaf sikuiandika basi ndugu msomaji unaweza kuiandika hapo chini....
Karibuni.
Wakuu.... wengi wetu hapa JF na nchini kwa ujumla, tunajua kwamba raisi wa JMT mh Samia S. Hassan anapambana usiku na mchana, ili kuhakikisha serikali yake inaleta maendeleo katika wilaya, mikoa na nchi yote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Lakini kama ilivyo desturi ya sisi binadamu unapokuwa na mambo, vitu au watu zaidi ya watatu ubavuni kwako, ni wazi kuwa hautoweza kubalance upendo wako kwao yani iwe mia kwa mia kwa kila mtu au kitu. Ni lazima mtu au kitu kimoja utakipenda zaidi ya kiingine.
Hili hutokea hata kwa mzazi mwenye watoto mfano wa5 hujikuta anampenda mtoto mmoja au wawili zaidi ya awapendavyo waliobaki, japo kama mzazi huwa haoneshi moja kwa moja upendeleo wake huo kutokana na kutaka wale wengine wasijisikie kubaguliwa nk.
Hivyo basi hata raisi wetu, ni raisi wa nchi nzima, lkn ukweli ni kwamba kuna baadhi ya mikoa ambayo amekuwa akionesha kuipenda na kuijali zaidi ya mikoa mingine, na hili limekuwa likionekana kupitia miradi mbali mbali kabambe aliyoielekeza katika mikoa hiyo hata kama anajaribu kutokuonesha kuwa ana baze zaidi huko, lkn wafuatiliaji tunaona wenyewe kwa macho yetu na kusikia pia kwa masikio yetu.
Mikoa hiyo ambayo inabahati mno na serikali hii ni 👇
1. Dodoma.
Mkoa huu pamoja na kwamba raisi aliekuwepo madarakani hayati John P. Magufuli aliupenda na kuelekeza zaidi macho yake huko, pia umeendelea kuneemeka na uongozi huu wa awamu ya 6 chini ya raisi Samia na kupelekea miradi mingi ya maendeleo kupelekwa huko.
Nafikiri haya yamesababishwa na hadhi yake kama mji wa serikali na makao makuu ya nchi.
2. Kigoma.
Mkoa wa Kigoma pia unazali na uongozi huu wa raisi Samia. Japo mkoa huu una kiongozi mmoja mkubwa wa chama cha upinzani, na historia yake ya baadhi ya vijana kushikiwa akili na kupenda kuunga mkono wapinzani mbali mbali, lkn raisi Samia hakujali hayo.
Ameelekeza nguvu na miradi katika mkoa huo kuliko kiongozi mungine yoyote aliewahi kutawala kabla yake. I hope hiyo miradi ikikamilika basi Kigoma itakuwa Small "Chicago", achilia mbali zile stori za mh Kikwete kwamba angeigeuza Kigoma kuwa Dubai kwa maneno tu matupu bila vitendo wala kutoa hela za miradi husika.
3. Mbeya.
Huu mkoa nao ni miongoni mwa mikoa inayofaidika kwa kasi kupitia uongozi huu wa awamu ya tano. Kabla ya hapo mkoa huo ni kama vile ulikuwa umesahaulika kimtindo, maana hata miundo mbinu ya mkoa huo kwa upande wa barabara, shule, hospital nk vilikuwa hovyo, ila toka raisi Samia aingie amekuwa akionesha kushirikiana na mbunge Mbeya mjini ambae pia ni spika wa bunge kuleta maendeleo ya kweli katika mkoa huo.
Kwa kuonesha kuwa anaupenda mkoa huo kwa vitendo, serikali ya raisi Samia tayari imeshatoa mamilioni ya miradi kwa ajili ya shule, barabara nk. Japo kuna baadhi ya watumishi wa serikali kutoka mkoa huo wanaonekana kutohitaji maendeleo katika mkoa huo kwa kutafuna mamilioni ya baadhi ya miradi kama alivyosema raisi Samia alipokuwa ziarani mkoani huko, lkn ni kama vile bado hajachoka kuendeleza miradi katika mkoa huo, bila kujali baadhi ya wapinzani ambao wao wanachotaka ni kuingia bungeni tu bila kujali maendeleo anayowaletea raisi Samia katika mkoa wao.
Baadhi ya wanasiasa wenye familia zao Ulaya na Marekani ambao kiasili hawatoki katika mkoa huo, wamekuwa wakiwahadaa vijana ambao wengi wao walikimbia shule mkoani hapo, wapinge miradi hiyo ya maendeleo ili uchaguzi mkuu utapofika wachaguliwe wao tu na vyama vyao.
4. Mwanza.
Mkoa wa Mwanza pia ni kama Dodoma. Ulikuwa na zali chini ya serikali ya awamu ya 5 ya hayati Magufuli, na bado umeendelea kuwa na bahati pia chini ya serikali hii ya awamu ya 6 ya raisi Samia.
5. Mtwara....
6. Lindi....
Kama kuna mikoa mingine ambayo imeneemeka na uongozi wa raisi Samia alaf sikuiandika basi ndugu msomaji unaweza kuiandika hapo chini....
Karibuni.