Muoe Binti yako ukae naye mwenyewe full stop.
Tabia ya kufuatilia maisha ya familia ya Binti yako haifai, kashaolewa mwache aijenge familia yake.
Baada ya kuona usumbufu sana sana sana juu ya mke wangu toka kwa wazazi wake kila wakati wananiambia mruhusu Binti yetu aje atusalimie sisi wazazi wake , nikaona isiwe taabu nikampa nauli akaenda kwao, alipofika nikamwambia baba na mama kaeni naye hadi nitakapokuja kumfuata mimi mwenyewe, wakaichukulia kirahisi rahisi.
Wakashangaa miezi inakatika sitokei, kila wakipiga simu kuuluza baba unakuja lini kumfuata mwenzio nawajibu vuteni subira nitakuja. Miezi 11 ilikatika wife hadi alikata tamaa na kila tukiongea kwa simu namwambia ukae hadi hamu iishe ya kutaka kuwaona wazazi wako kila wakati.
Siku nimeenda ghafla tena bila taarifa, asubuhi na mapema haoooo na mke wangu safari. Tulipofika nyumbani mke wangu aliapa hatorudia tena

na hata wazazi wake walimwambia safari hii ukakae utulie na familia yako maana mmmmmh!
Ni upuuzi tu , mtu umeolewa badala ukae utulie na familia yako umekalia ujinga tu kila wakati unaomba nauli ukasalimie wazazi wako. Huyo mama yako anaenda kusalimia kwao mara ngapi kwa mwaka? au yeye hana wazazi?
Unaacha mji wako inakuwa taabu, vimiradi vidogovidogo vinayumba kwa kukosa usimamizi, watoto wa shule inakuwa taabu mama hayupo baba muda mwingi yupo kuhangaika, nyumba ovyo ovyo eti kisa kaenda nyumbani kusalimia!
Halafu ni gharama , nauli ya kwenda na kurudi, bado mahitaji ya kuwapelekea baba na mama, zawadi zao, matumizi.
Kwenda ni muhimu lakini sio lazima na isiwe kila wakati, iwe kwa kiasi