Hii kwako unaichukuliaje?

Hii kwako unaichukuliaje?

Suluhisho hapa ni kutokupokea mahari ili binti awe huru anapokuwa kwenye ndoa
Kuolewa siyo lazima, simama na msimamo wa kutoolewa uwe huru kabisa ukitaka kukesha club hata siku mbili mfulululizo ruksa, kwa nini ujibane na ndoa?.
Kwa akili hizi usithubutu kuolewa unaweza kwenda kuuwawa kabisa, kuna wanaume hawana muda wa kubishana na Mwanamke mjuwaji.
 
Usiadhani mahari ndo inatoa mandate kwa mume kuwa mume. Ni ile hali ya wewe kusema nenda kaishi naye, full stop. Otherwise tungekuwa na fixed figure ya mahali. Ndiyo maana kuolewa, mahali naanzia 0 hadi mamilioni, lakini mume atapewa nafasi ile ile regardless of the amount ya mahali
Ikitokea binti yako anazuiwa na mumewe kuja kwako, na ni miaka 5 imepita hamjaonana; utamfanyaje?
 
Dawa kumtoza mtu ng'ombe hata 50 usimpeleke binti yako kihasara wapigwe mahari kubwa urudishe hata robo ya pesa uliyotumia kumlea.
 
Kuolewa siyo lazima, simama na msimamo wa kutoolewa uwe huru kabisa ukitaka kukesha club hata siku mbili mfulululizo ruksa, kwa nini ujibane na ndoa?.
Kwa akili hizi usithubutu kuolewa unaweza kwenda kuuwawa kabisa, kuna wanaume hawana muda wa kubishana na Mwanamke mjuwaji.
Ndipo unasikia binti yako uliyemgharamia, ameuliwa na mumewe; utamfanyaje huyo mumewe?
 
Ikitokea binti yako anazuiwa na mumewe kuja kwako, na ni miaka 5 imepita hamjaonana; utamfanyaje?
Mwamba hapo huna cha kufanya zaidi ya kuomba vikao vya suluhu tu..!! Maana mpaka ugomewe hivyo, kuna jambo, si bure. Mwombe mkweo ikishindikana shirikisha wazazi wake..!
 
Kuolewa siyo lazima, simama na msimamo wa kutoolewa uwe huru kabisa ukitaka kukesha club hata siku mbili mfulululizo ruksa, kwa nini ujibane na ndoa?.
Kwa akili hizi usithubutu kuolewa unaweza kwenda kuuwawa kabisa, kuna wanaume hawana muda wa kubishana na Mwanamke mjuwaji.
Yana mwisho hayo..!! Kila kitu kina umri. ATafikia tu umri wa kujutia maamuzi yake..!!
 
Kwani Kuna mtu alikutuma umpeleke mashule ya gharama kiasi kwamba hadi ukashindwa kufanya mambo yako. Ndio amesha olewa hivo mzee move on jipange na Maisha ya uzeeni
 
Dawa kumtoza mtu ng'ombe hata 50 usimpeleke binti yako kihasara wapigwe mahari kubwa urudishe hata robo ya pesa uliyotumia kumlea.
Na hapa ndipo mnapowaloga mabinti zenu. Pesa inauma na atakayeumia hapo ni binti yako sio wewe. Mbona mme kamchukua binti bila wazazi wabinti kutoa kitu. Hamna bora kati ya mme wala mke wote ni binadamu, sasa wewe jikweze uje umuharibia binti yako. Nachakufikirisha zaidi, mara myingi mwanaume anakuwaga financially stable zaidi kumzidi mwanamke kwasababu mwanamke hakubali kuolewa na wachini wa level yake. Pesa sio gharama ya maisha ya mtu, tutawaaribu mabinti zetu na kusingizia utandawazi. Kweli dunia imebadilika.
 
Ndipo unasikia binti yako uliyemgharamia, ameuliwa na mumewe; utamfanyaje huyo mumewe?
Wewe ulikuwa wapi mpaka akauliwa. Maana ukichunguza matukio yote yamauaji kuna tabia chafu zilikuwa zinaendelea na hamna hata mmoja aliyezishughurikia. Leo kauawa ndio unajifanya baba mwema, msiingilie ndoa za watoto wenu kwavitu vya kiutandawazi actually kwalengo laufeminist, mtazivunja ndoa kabisa na watoto wakike wabaki kuchezewa.
 
Umepambana kumlea na kumsomesha mtoto wako wa kike, mpaka akafikia hatua fulani ya elimu; iwe cheti, diploma, degree, masters, PhD, au u-profesa. Baada ya hapo, akaolewa na akawa na mji wake.

Changamoto: Leo hii unataka binti yako aje akusalimie nyumbani; itamlazimu mpaka aombe ruhusa kwa mumewe, na amruhusu, ndio aweze kufika, asiporuhusiwa hatokuja kukujulia hali.

Swali: Hii kwako unaichukuliaje, ukiangalia wewe ndio mzazi, uliyemlea na kumgharamikia elimu; lakini cha ajabu, leo mtu baki ndio anayempangia aje akuone ama asije kukuona?​

Kama hupendi hivyo usikubali aolewe mwache akae hapo kwako tu itapendeza
 
Muoe Binti yako ukae naye mwenyewe full stop.

Tabia ya kufuatilia maisha ya familia ya Binti yako haifai, kashaolewa mwache aijenge familia yake.

Baada ya kuona usumbufu sana sana sana juu ya mke wangu toka kwa wazazi wake kila wakati wananiambia mruhusu Binti yetu aje atusalimie sisi wazazi wake , nikaona isiwe taabu nikampa nauli akaenda kwao, alipofika nikamwambia baba na mama kaeni naye hadi nitakapokuja kumfuata mimi mwenyewe, wakaichukulia kirahisi rahisi.

Wakashangaa miezi inakatika sitokei, kila wakipiga simu kuuluza baba unakuja lini kumfuata mwenzio nawajibu vuteni subira nitakuja. Miezi 11 ilikatika wife hadi alikata tamaa na kila tukiongea kwa simu namwambia ukae hadi hamu iishe ya kutaka kuwaona wazazi wako kila wakati.

Siku nimeenda ghafla tena bila taarifa, asubuhi na mapema haoooo na mke wangu safari. Tulipofika nyumbani mke wangu aliapa hatorudia tena na hata wazazi wake walimwambia safari hii ukakae utulie na familia yako maana mmmmmh!

Ni upuuzi tu , mtu umeolewa badala ukae utulie na familia yako umekalia ujinga tu kila wakati unaomba nauli ukasalimie wazazi wako. Huyo mama yako anaenda kusalimia kwao mara ngapi kwa mwaka? au yeye hana wazazi?

Unaacha mji wako inakuwa taabu, vimiradi vidogovidogo vinayumba kwa kukosa usimamizi, watoto wa shule inakuwa taabu mama hayupo baba muda mwingi yupo kuhangaika, nyumba ovyo ovyo eti kisa kaenda nyumbani kusalimia!

Halafu ni gharama , nauli ya kwenda na kurudi, bado mahitaji ya kuwapelekea baba na mama, zawadi zao, matumizi.

Kwenda ni muhimu lakini sio lazima na isiwe kila wakati, iwe kwa kiasi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom