Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 37,136
- 55,605
- Thread starter
- #41
Kwa mfano akienda bila kutoa taarifa, utamfanyaje?NaNUKUU..... napitia hapa kwa baba mara moja... mwisho wa kunukuu...!! NDIYO RUHUSA YENYEWE
Kwa mfano akienda bila kutoa taarifa, utamfanyaje?NaNUKUU..... napitia hapa kwa baba mara moja... mwisho wa kunukuu...!! NDIYO RUHUSA YENYEWE
Absolutelykwa hiyo mkuu, Mahari ni sawa na kumuuza binti?
Zingatia maandiko ukiona unaumia au utaumia basi usimruhusu kuolewa, mbona rahisi tu hiyo na ukubali kulea wajukuu hapo kwako.Umepambana kumlea na kumsomesha mtoto wako wa kike, mpaka akafikia hatua fulani ya elimu; iwe cheti, diploma, degree, masters, PhD, au u-profesa. Baada ya hapo, akaolewa na akawa na mji wake.
Changamoto: Leo hii unataka binti yako aje akusalimie nyumbani; itamlazimu mpaka aombe ruhusa kwa mumewe, na amruhusu, ndio aweze kufika, asiporuhusiwa hatokuja kukujulia hali.
Swali: Hii kwako unaichukuliaje, ukiangalia wewe ndio mzazi, uliyemlea na kumgharamikia elimu; lakini cha ajabu, leo mtu baki ndio anayempangia aje akuone ama asije kukuona?
Kama uchumi uko vizuri, ni bora ulee wajukuu tuZingatia maandiko ukiona unaumia au utaumia basi usimruhusu kuolewa, mbona rahisi tu hiyo na ukubali kulea wajukuu hapo kwako.
Kama hujui maana ya send-off maana yake hata maana ya kitchen party hujui.Tupe maana
Ikitokea binti yako amezuiwa na mumewe kuja kukuona, utamfanyaje?Kama hujui maana ya send-off maana yake hata maana ya kitchen party hujui.
Kuolewa siyo lazima, usikubali kuolewa kama unataka uhuru wako kamili
Kwanza ndowa haitaki debate kila kitu unataka haki huwezi kukaa kwenye ndoa, nakushauri tafuta baharia sperm donor akupe mtoto tu mambo ya ndoa waachie wengine wewe huna upako huo.
Kama haiingilii ratiba yetu yoyote anaweza kwenda tu, naamini ataniletea salamu za wazazi. Mfano mnaishi Kimara na wakwe zako wako wanaishi hapo Ubungo na mkeo anafanya kazi City Center, anaweza kupitia atokapo kazini na kuniletea salamu zao, na ikawa poa tu.Kwa mfano akienda bila kutoa taarifa, utamfanyaje?
Ina maana hutokuwa na cha kufanya, zaidi ya kupokea ujumbe wa huko alikotoka ?Kama haiingilii ratiba yetu yoyote anaweza kwenda tu, naamini ataniletea salamu za wazazi. Mfano mnaishi Kimara na wakwe zako wako wanaishi hapo Ubungo na mkeo anafanya kazi City Center, anaweza kupitia atokapo kazini na kuniletea salamu zao, na ikawa poa tu.
Huo sasa ni ugomvi maana huyo mkwe ni mwanangu pia. Kumkataza mkewe asinisalimie ni sawa na kwamba yeye mwenyewe mkwe hataki kunisalimia. Hilo linapaswa kushughulikiwa kama mgogoro.Ikitokea binti yako amezuiwa na mumewe kuja kukuona, utamfanyaje?
Umeshasikia watu wanapigwa kwenye ndoa na mzazi huwezi mfanya kitu mumewe..!?? Hivi kwenye jamii yetu hii, mzazi umekusanywa na wazee halafu mnajadili kesi ya mwanao anakimbilia kwako kila siku bila ruhusa, unadhani kuna mzee atakuelewa?Kwa mfano akienda bila kutoa taarifa, utamfanyaje?
Sasa, hapo ndipo unarudi kwenye mada husikaHuo sasa ni ugomvi maana huyo mkwe ni mwanangu pia. Kumkataza mkewe asinisalimie ni sawa na kwamba yeye mwenyewe mkwe hataki kunisalimia. Hilo linapaswa kushughulikiwa kama mgogoro.
Ujumbe gani tena. Mtu akiniambia "nimepita kwa baba, hawajambo wanakusalimu", kuna nini cha ziada? Na tena siku hizi kuna simu, anaweza kunipigia hata akiwa nao "Baba T niko hapa kwa baba nimepitia mara moja kuwaona, hawajambo", nami nitaomba hiyo simu niwasabahi. Shida iko wapi?Ina maana hutokuwa na cha kufanya, zaidi ya kupokea ujumbe wa huko alikotoka ?
Tunajipaga imani tu kwamba si kumuuza..!! In reality ndo hivyo..!! Kama kununua chochote unafanya negotiations kama unazofanya wakati wa kukubaliana mahali, then what is the difference?kwa hiyo mkuu, Mahari ni sawa na kumuuza binti?
Hujafa hujaumbika. Unaweza kuwa na bilioni 10 benki lakini huna uwezo wa kwenda kwenye ATM kuchukua elfu 10 ya kununulia maziwa (unaumwa miguu, mgongo, kiuno, huoni vizuri au una dementia)mzazi kumlea kumsomesha mtoto ni wajibu sio ombi ila mtoto sio wajibu wake kukulea ww ulikua wapi kutafuta mali zako uje utoe macho uzeeni kweny mali ya mtoto wako
Suluhisho hapa ni kutokupokea mahari ili binti awe huru anapokuwa kwenye ndoaTunajipaga imani tu kwamba si kumuuza..!! In reality ndo hivyo..!! Kama kununua chochote unafanya negotiations kama unazofanya wakati wa kukubaliana mahali, then what is the difference?
KIFUPI TUNACHOKIFANYA KWENYE KULIPANA MAHALI NI KUWA WE HAVE DECIDED TO CALL A SPOON A SPADE
Hakuna mwanaume mwenye akili timamu atamzuia mtoto kwenda kusalimia kwao, lakini hizi ndoa za binti kwao ubungo halafu kaolewa kimara zina matatizo sana, mabinti wanajisahau kama wameolewa mara kwa mara wanataka wakapige story na mama zao kitu ambacho si sahihi na hakuna mwanaume yeyote anaweza kukubaliana na upumbavu huo.Ikitokea binti yako amezuiwa na mumewe kuja kukuona, utamfanyaje?
Na asipomruhusu kuolewa, WANANZEGO TUTAYASEMA YETU.. bingwa anakula kuku na mayai yake. Na hasa kama kila akiletwa mchumba kutambulishwa mwamba anakaba hadi penati..!!Zingatia maandiko ukiona unaumia au utaumia basi usimruhusu kuolewa, mbona rahisi tu hiyo na ukubali kulea wajukuu hapo kwako.
Mada inafikirisha sanaHujafa hujaumbika. Unaweza kuwa na bilioni 10 benki lakini huna uwezo wa kwenda kwenye ATM kuchukua elfu 10 ya kununulia maziwa (unaumwa miguu, mgongo, kiuno, huoni vizuri au una dementia)
Usiadhani mahari ndo inatoa mandate kwa mume kuwa mume. Ni ile hali ya wewe kusema nenda kaishi naye, full stop. Otherwise tungekuwa na fixed figure ya mahali. Ndiyo maana kuolewa, mahali inaanzia 0 hadi mamilioni ya fedha, lakini mume atapewa nafasi ile ile regardless of the amount ya mahaliSuluhisho hapa ni kutokupokea mahari ili binti awe huru anapokuwa kwenye ndoa