Hii kauli ya mke wangu ina maana gani?

kyagata

JF-Expert Member
Oct 18, 2016
6,528
12,622
Hello watanzania wenzangu!

Ebana kabla ya kwenda kwenye point naomba nidiklee interest kuwa mimi nimeoa,nina mtoto mmoja and I am responsible father for 100%.

Sasa bana, mimi ni mzee wa tungi ingawa sio wale wa kunywa hadi kubebwa,na nakunywa bia tu sio hizi double kick.

So last weekend wife alitoa kauli flani ambayo ingawa nilikua nimelewa ila ilinifikirisha sana,wife alisema kwamba hataki mtu mlevi ndani kwake. Na ikumbukwe hapo ndani mnywaji ni mimi tu.

Nikaona kabla ya kumzaba makofi niwaulize wadau, huyu mke wangu alikua na maana gani hivi?
 
Da kazazi hiki ko kila ukionyesha msimamo kama mwanaume kwa mke wako unagongewa. Bac wanaume tuwe mazuzu ili tusigongewe daa
Msimamo wa kung'ang'ania kuwa mlevi huo siyo msimamo ni upumbavu,misimamo yenye tija ndani ya nyumba ni kama “nimesema huyu mtoto atasoma shule fulani,nimesema nyumba hii ni gharama sana lazima tujibane na sisi tujenge yetu,gari kwa sasa bado wakati wake kununua etc”.

Wakati wote ukishakuwa mume unatakiwa uwe na hoja kumzidi mkeo utashangaza umati mkeo kukukalisha vikao kwa ndugu akilalamikia tabia zako za ulevi na wewe kuonyesha kuridhika nazo ila ikiwa ni vikao kuhusu misimamo yako ya kimaendeleo hakuna atakayemsikiliza.
 
Back
Top Bottom